DED mteule wa Kilolo si ndiye mwenye kesi ya TAKUKURU kule Nzega?

Hapa kazi tu, Kama anaweza kazi basi amna shida hayo ya rushwa tegemea kujibiwa kuwa " HIZO NI SIASA"
 
Hii ni kazi ya waandishi wa habari ila hizi ajira za ukuu wa wilaya zinadhoofisha sana hii taaluma!
 
Who cares?

Cha maana awe na shati la kijani na suruali nyeusi (kada) kwa sasa hiyo ndo sifa ya kwanza....
 
Ni kweli, ndo mwenyewe. Sasa alipata vipi huu ukurugenzi..!!! Soon jipu litatumbuliwa
 
Kama sikukosea huyu DED mteule wa Kilolo DC Aloyce Kwezi, siyo yule aliyekuwa Afisa Utumishi wa Halamshauri ya Nzega na sasa Halmashauri ya Bunda na kesi ya TAKUKURU kule Nzega.

Kumbe hata wenye kesi za TAKUKURU nao wanapata uteuzi. Kama siyo yeye basi naomba samahani.

DHRO wa Bunda Aloyce Kwezi kortini kwa tuhuma za rushwa
Ina maana alikuwa na kesi ya rushwa Nzega akahamishiwa Bunda na sasa ni DED Kilolo?
 
Si Ushasikia mkuu kasema alijiridhisha na alifanya uchunguzi kwa muda wa Miezi minne... Pia Alisikitishwa kwa kuchelewa kwake kuwapata maana wamebakiwa na miaka minne na miezi kadhaa waachie utawala mwingine... Jamaa sijui ameshajitabiria muda wake wa kuongoza nchi!! najiuliza tu
 
Hamchoki na umbea? yule Luhende ameenda wapi? kila siku mnaumbuliwa lkn bado hamchoki kuzusha
 
Duu?? Wakuu mpo vizuri kwa data. Ama kweli hiki ni kisiwa cha takwimu. Kumbe huyu jamaa alikuwa noma kwa wadada. Nadhani atakuwa ameacha hizo tabia
 
Sasa inamaana kukesha kote kule hakuna alichoambulia.Maana jamaa amesema alikuwa halali,-hatembei
 
Ndio yy na ni ndg yangu yupo alikuwa afisa utumishi halmashaur ya wilaya ya bunda mji. Na hajamaliza muda mrefu hata mwaka cdhan kama umeisha na amekuwa akikaa hotelin hata nyumba alikuwa hajatafutiwa.
 
Back
Top Bottom