Binadamu anauwezo mkubwa sana, ila anaelekeza nguvu na maarifa seheme isiyo sahihi? MF ni kama hii uliosema DSM kwa sisimizi ni kama ulimwengu mzima. Binadamu anaelekeza nguvu kubwa kutaka kujua vitu vilivyo mzunguka kuliko kujijua mwenyewe. Kumbuka asili ya vitu vyote ni moja tuu ambayo pia ndio asili ya binadamu. Binadamu akijua asili yake atajua asili ya kila kitu. Badala ya kuhangaika kujua tawi, majani na matunda ya mti atajua ni mbegu iliyooteshwa ardhini.
Kila ukionacho, ukisikiacho, ladha ya ukilacho tafsiri yake iko ndani yako. Tuna elimu kubwa sana ndani yetu ilatumeshindwa kuifikia. Hii Dunia ipo kwa sababu wewe upo, kinyume ya hapo Dunia haipo. Majibu ya mambo mengi yapo ndani tunatembea nayo, tunalala nayo, ktunaishi nayo. Inahitaji mwanzo na mwanzo ni kutafuta jibu la maswali yafuatayo;
1. Kwa nini upo hapa Duniani? Kufanya nini hasa?
2. Sababu ulizozania, ua ulizo ambiwa je zinamashiko?
3. Kama zina mashiko kwanini unaogopa kufa? Ilihali ukijua kuwa lazima utakufa, kulikuwa na hajagani ya uwepo wako wa wastani wa miaka 100 wakati dunia iko kwa million ya miaka? Ni kama nukta moja ya kuwa hai kwenye nukta billions
4. Popote uwapo utakuta kila kitu kina sababu ya uwepo wake, kuanzia na posensions zako, ulivimili kwa sababu maalumu, miti, majani, mvua, maji vyote utakuta kwa ajiri ya kusaidia wewe uishi, lakini wewe je? Unaishi kwa sababubu gani?
Maswali haya ni ufunguo wa tafakuli muhimu ndani yetu na upelekea mwanzo wa kujitambua na hatimaye kutambua ukweli wa sisi na maumbile mengine yaliotuzinguka na muumba wake.
Sent using
Jamii Forums mobile app