Kaizer
Platinum Member
- Sep 16, 2008
- 25,320
- 17,823
1.
6.
Namshukuru Manani, himeni yangu salama,
Hadi huko mwakani, haitotiwa alama,
Wala siweki sokoni, yake wangu kujinoma,
Dedilaini mwakani, ndoa lazima nifunge
Malenga ninawaita, hima nisaidieni,
Nimeupata utata, kuifahamu himeni,:coffee:
Nakaribia kudata, japo ni wa kiumeni,
Nawasihi mnijuze, himeni ni kitu gani?
Miss ninakupongeza, kwa kweka hadharani,
Ndoa umeitangaza, umechoka upwekeni,
Ila umenishangaza, umeitaja himeni!:shock:
Nawasihi mnijuze, himeni ni kitu gani,
Mnijuze sifa zake, hadi mtu ajinome,
Kama dau niliweke, ili nami nijinome,
Sokoni nijipeleke, madukani nijitome,
Nawasihi mnijuze, himeni ni kitu gani?
Nakuita Klorokwini, waifahamu himeni?
Butege na Sipirini, mewahi kuioneni?
Maguluma na Amani, tafadhali nijuzeni,
Nawasihi mnijuze, imeni ni kitu gani?
Na Kaizer K. Kaizer