Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, Naibu Kamishna wa Polisi ,(DCP) David Misime ameeleza kuwa jukumu la kulinda amani ni la kila Mtanzania, kwani vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani vinafanywa na watu waliopo katika jamii
Misime amebainisha hayo katika Kongamano la Wanawake wa Dar es salaam, linalofanyika leo Oktoba 26, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa DYCCC, Chang'ombe mkoani Dar es Salaam
"Suala la ulinzi na usalama katika jamii si suala la polisi pekee bali ni suala la jamii nzima", amesema DCP Misime.
Amewasihi wanawake Kutumia sauti zao kuwakemea wanafamilia katika mambo yanayoweza kuvunja amani ili kuhakikisha amani inaendelea kutawala na kuhamasisha watu katika jamii kujitokeza kupiga kura
Kongamano hilo linaangazia faida na madhara ya uchaguzi likiwa na kaulimbiu, 'usipomchagua unayemtaka, utachaguliwa usiyemtaka"
Chanzo: Jambo TV
Misime amebainisha hayo katika Kongamano la Wanawake wa Dar es salaam, linalofanyika leo Oktoba 26, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa DYCCC, Chang'ombe mkoani Dar es Salaam
"Suala la ulinzi na usalama katika jamii si suala la polisi pekee bali ni suala la jamii nzima", amesema DCP Misime.
Amewasihi wanawake Kutumia sauti zao kuwakemea wanafamilia katika mambo yanayoweza kuvunja amani ili kuhakikisha amani inaendelea kutawala na kuhamasisha watu katika jamii kujitokeza kupiga kura
Kongamano hilo linaangazia faida na madhara ya uchaguzi likiwa na kaulimbiu, 'usipomchagua unayemtaka, utachaguliwa usiyemtaka"
Chanzo: Jambo TV