DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo mkoani Dar es Salaam, Wakili Albert Msando, amewataka wafanyabiashara wilayni humo na Watanzania kwa ujumla kuondoa hofu kuhusu taarifa za kuwepo maandamano Oktoba 29, akisisitiza kuwa siku hiyo kutakuwa na amani na shughuli zitaendelea kama kawaida.
Akizungumza Oktoba 19, 2025 katika mjadala wa Wana Vicoba wa Jimbo la Ubungo uliofanyika Landmark Hotel jijini Dar es Salaam, Msando amesema Serikali imejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unadhibitiwa kikamilifu.
Msando amesema hakuna Mtanzania atakayeandamana kwa sababu wanaotoa vitisho mitandaoni ni mtu mmoja anayemiliki kurasa nyingi kwa majina tofauti na hata hayupo nchini, na lengo lake ni kuwakatisha tamaa wananchi wasipige kura.
Ameongeza kuwa vitisho vinavyosambazwa mitandaoni ni mbinu za kizamani zinazotumiwa na watu wanaolenga kuvuruga amani ya nchi.
Msando amehoji kuwa wanaodai wataandamana Oktoba 29 mbona wanandika ujumbe wao usiku kwenye kuta badala ya mchana, akisisitiza kuwa anataka kumwona anayesema atatoka siku hiyo, huku akibainisha kuwa hakuna hata nywele ya Mtanzania itakayoguswa.
Ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji bila woga na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao.
Akizungumza Oktoba 19, 2025 katika mjadala wa Wana Vicoba wa Jimbo la Ubungo uliofanyika Landmark Hotel jijini Dar es Salaam, Msando amesema Serikali imejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao unadhibitiwa kikamilifu.
Msando amesema hakuna Mtanzania atakayeandamana kwa sababu wanaotoa vitisho mitandaoni ni mtu mmoja anayemiliki kurasa nyingi kwa majina tofauti na hata hayupo nchini, na lengo lake ni kuwakatisha tamaa wananchi wasipige kura.
Ameongeza kuwa vitisho vinavyosambazwa mitandaoni ni mbinu za kizamani zinazotumiwa na watu wanaolenga kuvuruga amani ya nchi.
Msando amehoji kuwa wanaodai wataandamana Oktoba 29 mbona wanandika ujumbe wao usiku kwenye kuta badala ya mchana, akisisitiza kuwa anataka kumwona anayesema atatoka siku hiyo, huku akibainisha kuwa hakuna hata nywele ya Mtanzania itakayoguswa.
Ametumia nafasi hiyo kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji bila woga na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu ujao.