DC Chuachua: Marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini Mbeya

Acheni mila za kale kwanza mnachafua mazingira misiba wenu unahusu nini wengine jamani.
Mkuu hakuna ishu ya ukale wala usasa, gari ya matangazo ni mazoea halafu huwa haileti jam kama waongeza chumvi wengi walivyochangia hapo


Halafu Mbeya sisi tunajuana maeneo mbali mbali, gari ya matangazo husaidia pia kutoa taarifa kwa wale ambao hawajapata
 
Huwa yanaudhi sana. Namsapoti 100%

Ujinga unashabikia. Au kwa vile wanatumia magari. Ninatoka usukumani, misiba hutangazwa kwa jembe tena siku hizi ni kwa bodaboda.

Kutaarifu msiba imekuwa na sisi siku nyingi. Wewe huenda ni mtoto. Watu wazima watakumbuka RTD (Radio Tanzania Dar es Salaam) walikuwa na taarifa za misiba kwa dakika 5 mara baada ya taarifa ya habari saa 2 usiku (prime time)!!

Hata usipotangaza msiba, taarifa za msiba zitasambaa au kutokana na umaarufu wa marehemu, au ukaribu wa marehemu na watu maarufu.

Unasemaje sasa kuhusu misiba ya wakuu wa mikoa, mawaziri na wakubwa wa nchi kupitia runinga?? Nayo waache??

Crap!! Nchi ya kushughulika na vitu vidogo vidogo huku vya maana tukiviweka kando!
 
Ujinga unashabikia. Au kwa vile wanatumia magari. Ninatoka usukumani, misiba hutangazwa kwa jembe tena siku hizi ni kwa bodaboda.

Kutaarifu msiba imekuwa na sisi siku nyingi. Wewe huenda ni mtoto. Watu wazima watakumbuka RTD (Radio Tanzania Dar es Salaam) walikuwa na taarifa za misiba kwa dakika 5 mara baada ya taarifa ya habari saa 2 usiku (prime time)!!

Hata usipotangaza msiba, taarifa za msiba zitasambaa au kutokana na umaarufu wa marehemu, au ukaribu wa marehemu na watu maarufu.

Unasemaje sasa kuhusu misiba ya wakuu wa mikoa, mawaziri na wakubwa wa nchi kupitia runinga?? Nayo waache??

Crap!! Nchi ya kushughulika na vitu vidogo vidogo huku vya maana tukiviweka kando!
Kula like mkuu, huu mfumo wa elimu ya mzungu unafanya waafrika tukatae vyetu kwa kisingizio cha ukale

Mimi kama mwanambeya sioni tatizo lolote kuhusu magari ya matangazo, DC katukosea
 
Miaka mingi sio leo Wala Jana .Ni desturi yao sijui mwaka gani lakini iko miaka

Na wakazi hawana shida nayo .Mnyakusya akifa Ni kawaida yao kuuliza maswali kibbao kuwa aliyekufa nani anatoka ukoo gani alikuwa Nani nk halafu hutungua kilio wakijua Ni wa kwao

Maiti huwa hawapendi kuipitisha kimya kimya

DC kawakosea watu wa Mbeya Ni Kama pwani uswahilini ukikuta watu wamefunga turubai katikati ya barabara wamefiwa hutakiwi kuwabughudhi Wala kuuliza mna kibali Cha kuweka turubai au kufunga barabara tafuta njia nyingine wao mtaa mzima Wala hawana shida

Tatizo Ni hao watu wa kuja toka mikoa mingine wanaona Ni public nuisance.Ukifika kwa watu wewe DC heshimu desturi za watu hata weather ukifa matangazo yatakuwa kila Kona ndio maana hata Raisi akifa radio na TV zote huwa Ni kutangaza kifo tu

Huyu DC baadaye atadai kuwa watu wakienda kuzika makaburini waombe kibali Traffic wakibeba jeneza kwenda kuzika mabegani wakiwa wanatembea barabarani sababu barabara Ni ta magari si ya watembea kwa miguu wabeba jeneza kwenda makaburini

Kuna vitu kiongozi anatakiwa kupotezea sio kila kitu unachonga mdomo tu
Nchi yetu ina tatizo moja. Inaongozwa kwa kauli za wanasiasa. Sheria, kanuni na miongozo yote imelala. Ni kama haipo. Wanasiasa ndiyo wamegezwa kuwa sheria, kanuni na miongozo. Tunaongozwa kama watoto wa chekechea. Watoto wa chekechea ndiyo husimamiwa kwa kuongozwa.
 
Mkuu hakuna ishu ya ukale wala usasa, gari ya matangazo ni mazoea halafu huwa haileti jam kama waongeza chumvi wengi walivyochangia hapo


Halafu Mbeya sisi tunajuana maeneo mbali mbali, gari ya matangazo husaidia pia kutoa taarifa kwa wale ambao hawajapata
Huu utetezi mwepesi sijawahi ona yani matangazo ya wafu ni kukosesha watu amani moyoni bana, Mimi sikubaliani nayo kijijini kwetu hata kulia kwa mayowe huwa hamna hicho kitu sikuhizi.
 
Hii ni kali. Sijawahi kusikia sehemu nyingine. Siyo tabia nzuri hata kidogo. Msiba siyo kitu cha kupitisha matangazo kama hayo hasa kipindi hiki ambacho kuna njia nyingi za mawasiliano
Kwa tamaduni zenu ni suala zito lakini kwa jamii zingine ni la kawaida tu tusilazimishe watu waishi kwa tamaduni ambazo siyo za kwao
 
Huyo mkuu wa wilaya anasema wenye magari wanazua taharuki wakati sio kweli yeye ndie anasua taharuki wana Mbeya Mjini hawaoni taharuki magari yakipita yakitangaza ila yeye kuzuia ndio analeta taharuki

Aulize mwenzie Chalamila aliyekuwa mkuu wa mkoa mbabe kupinga desturi hizo sababu kwao hazipo Sasa hivi Ni mkuu wa mkoa tena? Ukifika kwa watu heshima Mila na desturi zao usijifanye mjuaji kupitiliza kisa tu umeteuliwa na Raisi
 
Mbeya. Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk Rashid Chuachua amepiga marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini hapa baada ya kuchukua miili ya watu waliofariki dunia hospitalini, akisema yamekuwa yakileta hataruki kwa wananchi na kujenga hofu.

Chuachua amesema hayo leo Jumanne Agosti 10, 2021 huku akiiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya doria na kuwachukulia hatua wamiliki wa magari hayo watakaobainika.

"Kumekuwa na tabia ya familia za watu wanaopoteza maisha kukodi magari ya matangazo na kuanza kutangaza maeneo mbalimbali ya jiji na kutaja majina ya wapendwa wao, sasa kwa niaba ya mkuu wa mkoa nimepiga marufuku rasmi leo Agosti 10 2021,"amesema Dk Chuachua.

"Ikumbukwe agizo hilo la kupiga marufuku hata aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alikataza lakini sasa suala hilo limeibuka kwa kasi ya ajabu na kila baada ya dakika kadhaa unasikia tangazo la msiba, hivyo kusababisha shughuli za kiuchumi kusimama kwa muda."

Dk Chuachua amesema agizo hilo lianze mara moja na ndugu wanaofikwa na msiba, wawasiliane kifamilia kufanya taratibu za mazishi na kuhusu suala la matangazo kutoka hospitali mpaka kwenye maziko marufuku.

Amesema hata mikusanyiko ya watu haitaruhusiwa kwa kipindi hiki cha Covid -19 awamu ya tatu.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya ,Dourmohamed Issa amesema uamuzi wa mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ni sahihi kwa kuwa kumekuwa na taharuki kubwa kwa jamiii pindi magari ya matangazo na inayobeba miili ya waliopoteza maisha ikipita barabara kuu.

"Hata mimi nimewahi kupata mshtuko nikiwa naendesha gari nilikutana na magari manne yakitangaza na manne yakiwa yamebeba miili ya watu waliopoteaa maisha kimsingi ni hali inayotisha sana kwa Watanzania na hata wagonjwa wanaokuwa wamelazwa kwenye hospitali zetu,” amesema Issa.

Mkazi wa Mbeya, Rehema Mwanjonde amesema uamuzi huo wa Serikali ni sahihi kwa kuwa hata matangazo hayo yamekuwa yakiwarejeshea kumbumbuki watu waliowahi kupoteza ndugu zao.

Source: Mwananchi
Dizaini kama wanaalika watu ili wakaongeze mzuka wa kulia msibani,ukiudhuria msiba wa mnyakyusa utastaajab na kuburudika wale watu wanajua kulia bana loh!!😆
 
Asante kwa ufafanuzi, lakini mfano kukiwa na misiba mitatu hali ya foleni inakuwaje kama ndo msafara mwendo wa madaha?!
Kuna wakati pale mwanjelwa Jam imeshika na hapo inapishana misiba, harusi na graduation. Mbeya mpaka graduation za darasa la saba wazazi wanawakodia watoto magari ya mziki wanavalishwa sare wanapitishwa mitaani na ukumbi wa sherehe wanachukua
 
Huyo mzee DC namjua vizuri kumbe kapelekwa huko Mbeya,Ngoja nimpigie simu atengue kauli yake.
 
Kwa hiyo hapo huyo mkuu wa wilaya ndio katatua kero za walio wengi hapo Mbeya mjini?

Huo ndio ubunifu wa juu was kutatua kero za wanna Mbeya Mjini? Kuwa kero kuu ya wanambeya mjini ilikuwa matangazo ya magari ya msiba?

Jamani haya hiyo ndio kazi iendelee?
 
Kuna wakati pale mwanjelwa Jam imeshika na hapo inapishana misiba, harusi na graduation. Mbeya mpaka graduation za darasa la saba wazazi wanawakodia watoto magari ya mziki wanavalishwa sare wanapitishwa mitaani na ukumbi wa sherehe wanachukua
Hahahaha, Mbeya nawasalimia sana! Kwa kweli mmetisha daa!
 
Mbeya. Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk Rashid Chuachua amepiga marufuku magari yanayofanya matangazo ya misiba jijini hapa baada ya kuchukua miili ya watu waliofariki dunia hospitalini, akisema yamekuwa yakileta hataruki kwa wananchi na kujenga hofu.

Chuachua amesema hayo leo Jumanne Agosti 10, 2021 huku akiiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama kufanya doria na kuwachukulia hatua wamiliki wa magari hayo watakaobainika.

"Kumekuwa na tabia ya familia za watu wanaopoteza maisha kukodi magari ya matangazo na kuanza kutangaza maeneo mbalimbali ya jiji na kutaja majina ya wapendwa wao, sasa kwa niaba ya mkuu wa mkoa nimepiga marufuku rasmi leo Agosti 10 2021,"amesema Dk Chuachua.

"Ikumbukwe agizo hilo la kupiga marufuku hata aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila alikataza lakini sasa suala hilo limeibuka kwa kasi ya ajabu na kila baada ya dakika kadhaa unasikia tangazo la msiba, hivyo kusababisha shughuli za kiuchumi kusimama kwa muda."

Dk Chuachua amesema agizo hilo lianze mara moja na ndugu wanaofikwa na msiba, wawasiliane kifamilia kufanya taratibu za mazishi na kuhusu suala la matangazo kutoka hospitali mpaka kwenye maziko marufuku.

Amesema hata mikusanyiko ya watu haitaruhusiwa kwa kipindi hiki cha Covid -19 awamu ya tatu.

Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya ,Dourmohamed Issa amesema uamuzi wa mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ni sahihi kwa kuwa kumekuwa na taharuki kubwa kwa jamiii pindi magari ya matangazo na inayobeba miili ya waliopoteza maisha ikipita barabara kuu.

"Hata mimi nimewahi kupata mshtuko nikiwa naendesha gari nilikutana na magari manne yakitangaza na manne yakiwa yamebeba miili ya watu waliopoteaa maisha kimsingi ni hali inayotisha sana kwa Watanzania na hata wagonjwa wanaokuwa wamelazwa kwenye hospitali zetu,” amesema Issa.

Mkazi wa Mbeya, Rehema Mwanjonde amesema uamuzi huo wa Serikali ni sahihi kwa kuwa hata matangazo hayo yamekuwa yakiwarejeshea kumbumbuki watu waliowahi kupoteza ndugu zao.

Source: Mwananchi
Yaaan msiba billa kuwa na mziki na gari ya matangazo huku mbeya ni Kama kukiuka utamaduni we2 na Kila jamii Ina utaratibu wake kama walivo wale jamaa wa kule nchini ghana
 
Back
Top Bottom