Ni kweli ktk tuhuma kuna mambo mawili yanatarajiwa ambayo ni kubainika kwa ukweli wa jambo au kutokuwa na ukweli wa jambo husika, ila ktk suala hili kama isipohusisha siasa za aliyeko juu mngoje chini, nyanya zakutazamwa ni
UHUSIANO - Hili la kwanza sababu liliweza kuwekwa bayana na vielelezo walivyoweza kuviwasilisha waungwana bila kujali walikovipata.
1)Elimu
2)Umri
3)uhalali wa vyeti vyako (uhalisia)
4)alama ktk usaili uliofanyika.
Kuna neno linatumika ktk matokeo yaliyokuwa yakitolewa kuwa waliochaguliwa ni kwa kuzingatia 1.jinsia 2.vipaumbele vya idara (hapa itabidi wavitaje sababu kwa wote walioitwa ktk usaili tayari wanavigezo laa pawepo na ufafanuzi wa kigezo hiki) 3.muungano (sina imani sana na kigezo hiki kwani mtanganyika na mzanzibari wanatofautiana elimu ktk level moja mf form six ya zanj iko tofauti na ya tanganyika?) 4. ufaulu (tunapongeza PCCB wao waliweka hadharani matokeo ya kila mmoja ya waliowasaili kwa alama alizozipata hapakuwa na shida)
Kama mungu tutamkuta kwa hili "KILA MMOJA ATAPATIWA HAKI YAKE KWA ALICHOKITENDA" vilio vya watanzania tulio wengi viko hapa juu ya haki itendeke na tunaimani za Katibu wa wizara kwa haya maamuzi ya awali aliyoyatoa ya kusitisha ili uchunguzi ufanyike.