Ebana kipindi cha hivi karibuni nimejikuta nimemaliza mwezi mzima bila kuona kina mama wengi wa mtaa wa pili wakipita wamebeba maji, nikahisi labda wamejiunga na DAWASA.
Ebana kumbe sio, ni kwamba dawasa sasa hivi wanatoa maji usiku wa manane , sijajua kama ni maeneo yote au laa na by saa 12 asubuhi wanakata.
Ndio nikakumbuka kumbe ndio maana kila kila niki flash maji yanatoka mara moja yanaisha.
Sasa najiuliza DAWASA wanamtolea maji nani usiku huo ili hali wanajua uhalisia wa maisha ya watanzania, wengi wanategemea wakateke maji kwa jirani.
Usiku huo wanateka maji vipi?
Hebu DAWASA njooni hapa mseme mnapotoa maji usiku wa manane huwa mnamlenga nani?
Sijajuaga tatizo ni nini eti mpaka miaka hiyo Daslam kuna shida ya maji, mito yote tuliyonayo bado kuna shida ya maji? Hao Dawasa wafumuliwe tu wanacheza tu hawako serious