Dawa ya kansa inapatikana!!!

Dawa ya kansa inapatikana!!!

Mkuu! Kwa vile bado upo katika kutafuta uhalali wa tiba yako, Kwa nini usitibu bure kwa sasa? Yani unampata Mgonjwa, unaweza kumpiga mpaka picha na video kabla ya kuanza kutumia dawa na pia baada ya kupona, na imani itawafanya watu wakuamini hata ukipeleka report yako kunapohusika wakuelewe!

Sote tunajua Cancer haina dawa, wapo watu wanateseka na Cancer Ma hospitalini, wakisubiri siku ya kufa Tu, sidhani Kama itakua shida kwao au kwa ndugu zao kuruhusu.

Fanya bure Mzee na baadaye dawa yako ikiidhinishwa na Taasisi husika then ndo unaweza kuja hapa kifua mbele na Ku charge pesa!

Habari za Mchana,,

Huwa natoa dawa bure kwa dosi mbili za kwanza ili Mgonjwa akiri kwamba zinamsaidia ndo anaruhusiwa kununua Dawa zinazofuatia.

Na nimeshajaribu kwa watu ishirini kwa Dar es Salaam, Mbeya na Arusha na wameshanipa Doctors Report kuwa wamepona.

Lakini sasa inatakiwa nipate Doctors report nyingi zaidi kama 50-70 au 100 ili niweze kuaminiwa na uma mwingi zaidi, na niweze kuzipeleka pale TFDA, BARAZA LA TIBA ASILIA NA Kwengineko ili niweze kupata Ruksa kubwa ya kuaminika na watu wote kwamba dawa hizi zinatibu Kansa na Kisukari.


Tafadhali naomba mfahamu kwamba Mimi sio tapeli na nina ajira yangu ambayo nalipwa mshahara mzuri. Nafanya haya kwa sababu nina Moyo wa huruma na wa kutoa msaada kwa jamii zote zinazonizunguka hapa Tanzania kwa sababu ninaipenda nchi yangu na sipendi kudhulumu watu.

Kama kweli kuna Mtu anashida tafadhali mwambie apate dawa bure na ajionee mafanikio yake mwenyewe kuliko kuishia kuteseka au kukatwa kiungo kwa kutojua kwamba kuna watu wanazo Dawa za Kansa na Kisukari ila ndo bado Nipo kwenye hatua za awali za kujitangaza na kupata publicity,,,

Nadhani mpaka sasa mtakua mmenielewa...
Na kwa maelezo zaidi nibeep ili nikupigie na nikueleze zaidi na kujibu maswali yako yote ambayo unayo...

Asanteni.
 
Kansa haina dawa mkuu zaidi ya kukata kiungo ambacho kimezurika na ukichelewa ni kusubir kifo tu

Habari za mchana Jojilo,

Usikubali kila kitu madakri wanachokuambia,, mimi ninayo dawa ya kansa ambayo nimesha wapa watu na wakapona,,

Nimesha sema na nitaendelea kusema kwamba sitozi pesa kwa mtu yeyote mpaka aijaribu dawa kwanza na kama itamsaidia na akaipenda basi ndo aweze kununua dozi zinazofuatia.

Nadhani umenielewa bro,,,
 
Mkuu nenda "ocean road hospital" wagonjwa wapo wengi, kawaponye kwanza wale ndo tuanzie hapo.

Habari za mchana Nando,

Nimesha kwenda Ocean Road ila wakawa hawataki kuniruhusu kuwatibu hata wagonjwa ambao wako mahututi kitandani na hata wale wanao subiri siku ya kufa,,

Sasa nadhani umenielewa kuwa magumu gani ambayo nimeyapitia,,

Kama ningekua nimeruhusiwa kuwatibu wagonjwa wa Kansa pale Ocean Road mbona wangepona na Leo ningekuwa mbali sana,,,

Hapo nadhani umenielewa,,,
 
Yaani una dawa ya kansa na kisukari alafu unasuasua kukarabati ofisi???? you can't be serious! Si ungekuwa ushahamia muhimbili?

Habari za mchana,

Una maana gani tena,, si ndo kwanza nimeanza kujitangaza, na hayo mafanikio nitayapataje kama sijulikani kwa watu wengi,,?

Ndo maana nimekuja huku JF ili nifahamike kwa watu wengi ili niweze kutoa huduma,,,.

Nadhani utakua umenielewa,,!!!
 
sw ww usichukue pesa je acpopona c itakua umemlisha mngonjwa wng sumu pamoja na usumbufu km upo tyr tuingie mkataba acpopona utatoa fidia ya usumbufu na kutudanganya
Hiki kitu aisee hata hospitali za kisasa kabisa hakipo. Unataka jamaa achukue role ya Mwenyezi MUNGU! We jamaa unavituko!
 
Mkuu mi naomba tu unipe ufafanuzi namna ulivyoithibitisha dawa yako kama yatibu kansa na sukari. Na pia huo muda ulioutaja umejuaje.

Nimejua kwa sababu nimeshawapa watu hizi dawa na nikaona mafanikio yake,,,
 
mkuu mtumie bradley uingereza ...anasubiri kufa

Unamba unipe contacts zake ili niweze kumtumia kwa sababu kuna ndugu zangu wako Uingereza nitawapa alafu watampelekea,,

Chakufanya wewe nipe hizo contacts za brafley alafu mimi ntampelekea,,,
 
mkuu mtumie bradley uingereza ...anasubiri kufa
Habari za Mchana fazam,,

Bado nasubiri hizo contacts za bradley sababu nilikua nachat na kaka yangu ambaye yuko Yorkshire na ameniambia yuko tayari kumpelekea huyo bradley hizi dawa, sasa ww nitumie hizo contacts za Bradley alaf mi nitamtumia dawa kwa DHL.
 
Habari za Mchana fazam,,

Bado nasubiri hizo contacts za bradley sababu nilikua nachat na kaka yangu ambaye yuko Yorkshire na ameniambia yuko tayari kumpelekea huyo bradley hizi dawa, sasa ww nitumie hizo contacts za Bradley alaf mi nitamtumia dawa kwa DHL.
search online mkuu lkn bradley ni fan wa sunderland aliyeomba wish za merry christmass wakati akisubiri ahadi yake itimie....xo akienda sunderland atampata easy
 
mashaka yangu ni hizo Id zenu zenye kuakisi imani fulani ili kumvuta mteja/mnunuzi. tumia majina halisi yasiyokuwa na kionjo cha imani ya wengi ili mteja akihiari asisingizie nilimfuata mpendwa ktk imani

Habari za Mchana Robert,

Kwanini nijifiche jina langu na niandike jina ambalo sio langu eeh,,?

Hilo hapo ndo jina ambalo nimepewa na wazazi wangu, kwa hiyo unataka nilikatae kwa sababu sasa ninataka kufanya biashara au,,,? Tafadhali naomba unisaidie kwasababu dawa zangu nimeshawapa watu wa dini na imani tofauti tofauti na wala hawakuhoji kuhusu jina langu.

Na kama unataka uhakika hadi (National ID) Kitambulisho cha taifa ntakuonyesha,,,!!!
 
Wewe doctor ! no Tabibu .... nani vile.... siku...no...wiki - no karne? yani doctor ngwara.... amekuthibiti kule back plan clinic umeibukia huku kivingine kuwatusua Watanzania ?
 
search online mkuu lkn bradley ni fan wa sunderland aliyeomba wish za merry christmass wakati akisubiri ahadi yake itimie....xo akienda sunderland atampata easy

Aaah,!! Basi mi nlifikiri bradley ni ndugu yako ambaye yuko England.

Sasa mimi ninatoa msaada kwa waTanzania wenzangu tu,, na sio waingereza,, kabda kama unamfahamu mtu yoyote mtaani ambaye anaumwa kansa basi ntampa dawa bure bila malipo kwa miezi mmoja hadi miwili mpaka atakapoona mafanikio na ndio anaruhusiwa kununua dozi zinazofuatia,,,


Nadhani hapo utakuwa umenielewa,,?
 
Mmmh hapa kuna harufu ya utapeli, peleka Wizara ya afya ikapimwe na ipelekwe WHO na mashirika mbalimbali kama TFDA kabla haijaanza kutumika

Why kila kinachofanywa na mtanzania kinakuwa utapeli??
 
Wewe doctor ! no Tabibu .... nani vile.... siku...no...wiki - no karne? yani doctor ngwara.... amekuthibiti kule back plan clinic umeibukia huku kivingine kuwatusua Watanzania ?
Wala hata sikuelewi unachozungumza,,?

Mimi ndo kwanza nimeanza kujitangaza wala sikuwahi kuwa na hospitali yeyote,,

Na huyo doctor Ngwara ndo kwanza namsikia kwako,,

kama kweli unataka msaada basi njoo usaidike, lakini si vizuri kusingizia watu ili waonekane matapeli,, sio vizuri hicho kitu unachokifanya,,,!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom