Dawa ya Deni Kulipa

Hmaster

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2010
Posts
346
Reaction score
86
Mdai: Hodi nyumbani!
Mtoto: Karibu!
Mdai: Hujambo?
Mtoto: Sijambo, shikamoo mgeni!
Mdai: Marahabaa, baba yako yupo?
Mtoto: Hayupo
Mdai: Sijamwona siku nyingi, kwani amekwenda wapi?
Mtoto: Subiri nikamuulize aniambie niseme amekwenda wapi!
Mdai: Ukamuulize nani?
Mtoto: Baba, kwa vile aliniachia maagizo kuwa mtu akija kumuulizia niseme hayupo lakini hakunipa maelezo niseme amekwenda wapi.
Palepale mzee nayedaiwa akajitokeza huku akivaa shati na kuanza kusema maneno ya kujikanyagakanyaga: mara ooh najisikia vibaya ndo maana nilikuwa nimejipumzisha, mara oh sijui nini. Kifupi alikamatwa. Kwa hiyo dawa ya deni kulipa.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…