Mhhh, hii habari naikubali na kuikataa nusu kwa nusu kwasababu moja kuu nilioipitia mimi mwenyewe sijaona au kuambiwa na mtu.
Kuna wakati familia yangu ilisambaratika nikabakia peke yangu nyumbani, loooo hakuna ambacho sijujaribu kufanya ili kujinasua. Nguvu ya kukubaliana na jambo lile ilikuwa robo tu so nikakwama, tv, simu, laptop, kuchukua mademu hakukunisaidia chochote.
Mambo yalipokuja kukaa sawa sikujua hata ile hali iliondokaje, namshukuru Mungu.
Kukubaliana na huo upweke kuwa sawa nimekubali mimi ni mpweke na kuna maisha mapya yanaweza kuendelea ni kuhama kutoka upweke kwenda kwenye uendawazimu, ni kujibadilishia mwenyewe aina ya matatizo ktk akili yako.