David Kitundu Jairo atiwa mbaroni na TAKUKURU

David Kitundu Jairo atiwa mbaroni na TAKUKURU

Eddo mkweli

JF-Expert Member
Joined
Jan 13, 2014
Posts
475
Reaction score
37
Habari zilizotufikia hivi punde.

Aliyekuwa katibu wa wizara ya nishati na madini na baadae kufukuzwa kwa tuhuma za Ufisadi na kuhalamisha mchakato wa upitishaji wa Bajeti ya wizara ya Nishati na Madini Ndugu David Kitundu Jairo anashikiliwa na TAKUKURU wilayani Iramba kwa tuhuma za kugawa Fedha wakati huu wa mchakato wa kura za Maoni.

Jairo ni mgombea wa Ubunge kati ya watu wa nne waliojitokeza akiwamo Amon,Mwigulu na Kilimba.

Jairo anatuhumiwa kusambaza fedha tsh.30000 kwa kila balozi na makatibu wa Matawi ya CCM katika vijiji mbalimbali akiwamo Ujungu,Mtekente,Mtoa,Msai n.k

Ni takribani masaa 2 sasa anashikiliwa katika ofisi hizo za Takukuru wilayani Iramba,hatua za kumfikisha mahakamani kwa kujibu tuhuma hizo.
 
Mbona kuna mahali nilisoma kuwa hao kina Jairo & co wamejitoa kura za maoni na kumwachia Mwigulu!!!
 
Aliyetoa kakamatwa je waliopokea wako wapi? I just hate this hypocrisy....!!!!:A S angry::A S angry:
 
Rais wa Mawe aka Mwigulu amefanikiwa kutoa draw.hahaha!CCM kazi kweli kweli
 
TAKUKURU ni waigizaji tu. Huyu alitakiwa kuwa jela toka alipokuwa Katibu Mkuu. Walimuacha kwenye kashfa ya mamilioni wanakuja kutoa macho kwenye hii ya elfu 30 kwa wajumbe wa nyumba kumi? Upepo tu utapita.
 
Back
Top Bottom