Nyanswe Nsame
Senior Member
- Jul 9, 2019
- 158
- 175
DAS Nyamagana, Afisa Mtendaji Pamba, Diwani Chadema wapiga Tsh. Milioni 45 za shule ya Pamba
Pesa hizo zinatokana na kuuza eneo la wazi la shule kwa wafanyabiashara wakubwa
Katibu Tawala wilaya ya Nyamagana, Yonas Alfred, Afisa Mtendaji wa kata ya Pamba Jonas Mugisha na Diwani wa Kata ya Nyamanoro, Abubakar Kapera wanashirikiana kuuza eneo la shule ya sekondari Pamba kwa wafanyabiashara wakubwa jijini Mwanza.
Wafanyabiashara wanaouziwa eneo la shule hiyo ni wale ambao walikuwa na maduka katika soko kuu la Mwanza na wale waliokuwa jengo la Mwadeco.
DAS huyo na wenzake wanauza eneo hilo la shule ambalo lipo mbele ya geti la kuingia na kutoka shuleni hapo kwa wafanyabiashara ambao huingiza kontena hizo nyakati za usiku.
Jinsi wanavyouza eneo hilo ni kwamba wafanyabiashara wenye mitaji mikubwa wanauziwa eneo kuanzia Tsh. Milioni tatu hadi sita ili waweke makontena.
Wengine wanaoweka vibanda vidogo vya chuma wanauziwa kuanzia Tsh. Milioni moja hadi milioni Tatu kitendo ambacho wafanyabiashara wengine wameanza kugoma na kuomba kurudishiwa pesa zao.
Kontena kubwa ambazo zimewekwa eneo hilo la shule ya sekondari ya pamba zipo kontena sita huku vibanda vidogo vya chuma vipo 20.
Kwa hesabu za kawaida kontena hizo zote sita, zimeingiza kiasi cha Tsh. Milioni 20 huku vibanda vidogo vimeingiza Tsh. Milioni 25.
Jumla ya pesa zote ni Tsh. Milioni 45 ambazo zimeingia mifukoni mwa watu hao watatu licha ya watu wengine wakifichwa ambao ni mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba, Mwanasheria wa Jiji Bi. Maliam na Afisa biashara wa Jiji.
Kutokana na wafanyabiashara hao kuvamia eneo hilo na kuweka makontena yao kwa usaidizi mkubwa wa viongozi hao, taarifa zinasema tayari bodi ya shule ya Pamba imekutana.
Bodi hiyo ya Pamba imekutana jana na leo na kufanya kikao, wakihoji kwanini eneo lao la shule kuvamiwa na wafanyabiashara bila kushirikishwa na kwamba eneo hilo limekuwa likitumiwa na wanafunzi katika shughuli mbalimbali.
Bodi hiyo inadai kwamba kabla ya kukutana walipeleka malalamiko yao kwa mkurugenzi wa Jiji la Mwanza lakini hakuna hatua zozote ambazo zilichukuliwa na kuwalazimu kuandika barua kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella.
Bodi hiyo inasema barua ambayo imeandikwa kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, pia itaandikwa nyingne kwenda ngazi ya kitaifa kwa msaada zaidi.
Picha za kontena zilizowekwa hapo Pamba.
Pesa hizo zinatokana na kuuza eneo la wazi la shule kwa wafanyabiashara wakubwa
Katibu Tawala wilaya ya Nyamagana, Yonas Alfred, Afisa Mtendaji wa kata ya Pamba Jonas Mugisha na Diwani wa Kata ya Nyamanoro, Abubakar Kapera wanashirikiana kuuza eneo la shule ya sekondari Pamba kwa wafanyabiashara wakubwa jijini Mwanza.
Wafanyabiashara wanaouziwa eneo la shule hiyo ni wale ambao walikuwa na maduka katika soko kuu la Mwanza na wale waliokuwa jengo la Mwadeco.
DAS huyo na wenzake wanauza eneo hilo la shule ambalo lipo mbele ya geti la kuingia na kutoka shuleni hapo kwa wafanyabiashara ambao huingiza kontena hizo nyakati za usiku.
Jinsi wanavyouza eneo hilo ni kwamba wafanyabiashara wenye mitaji mikubwa wanauziwa eneo kuanzia Tsh. Milioni tatu hadi sita ili waweke makontena.
Wengine wanaoweka vibanda vidogo vya chuma wanauziwa kuanzia Tsh. Milioni moja hadi milioni Tatu kitendo ambacho wafanyabiashara wengine wameanza kugoma na kuomba kurudishiwa pesa zao.
Kontena kubwa ambazo zimewekwa eneo hilo la shule ya sekondari ya pamba zipo kontena sita huku vibanda vidogo vya chuma vipo 20.
Kwa hesabu za kawaida kontena hizo zote sita, zimeingiza kiasi cha Tsh. Milioni 20 huku vibanda vidogo vimeingiza Tsh. Milioni 25.
Jumla ya pesa zote ni Tsh. Milioni 45 ambazo zimeingia mifukoni mwa watu hao watatu licha ya watu wengine wakifichwa ambao ni mkurugenzi wa jiji la Mwanza, Kiomoni Kibamba, Mwanasheria wa Jiji Bi. Maliam na Afisa biashara wa Jiji.
Kutokana na wafanyabiashara hao kuvamia eneo hilo na kuweka makontena yao kwa usaidizi mkubwa wa viongozi hao, taarifa zinasema tayari bodi ya shule ya Pamba imekutana.
Bodi hiyo ya Pamba imekutana jana na leo na kufanya kikao, wakihoji kwanini eneo lao la shule kuvamiwa na wafanyabiashara bila kushirikishwa na kwamba eneo hilo limekuwa likitumiwa na wanafunzi katika shughuli mbalimbali.
Bodi hiyo inadai kwamba kabla ya kukutana walipeleka malalamiko yao kwa mkurugenzi wa Jiji la Mwanza lakini hakuna hatua zozote ambazo zilichukuliwa na kuwalazimu kuandika barua kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella.
Bodi hiyo inasema barua ambayo imeandikwa kwenda kwa mkuu wa mkoa wa Mwanza, pia itaandikwa nyingne kwenda ngazi ya kitaifa kwa msaada zaidi.
Picha za kontena zilizowekwa hapo Pamba.