Shigganza
Senior Member
- May 24, 2018
- 160
- 412
Wakala wa mabasi yaendayo haraka (Dart) umeanza kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Waziri wa TAMISENI Suleiman Jafo wakati alipotembelea mradi huo katika siku za hivi karibuni kufuatia malalamiko ya watumiaji wa usafiri huo,. Baadhi ya maagizo hayo ni pamoja na kutengeneza mabasi yote mabovu na kuzuia magari, pikipiki binafsi kupitia katika barabara hizo, kuchukua mabasi 10 yanayofanya safari mbezi kwenda kimara yabebe abiria wanaoanzia kimara kwenda kivukoni na kariakoo, kushirikiana na SUMATRA kuongeza daladala za kawaida zinazotoka mbezi kwenda Kate na makumbusho na kupeleka majina ya watendaji wanaohujumu mradi kwa katibu mkuu TAMISEMI.