Daraja la Ulongoni A limekatika

Daraja la Ulongoni A limekatika

JAKABWANA

Member
Joined
Aug 27, 2019
Posts
39
Reaction score
20
Wakati wa mvua kubwa kunyesha .Daraja la Ulongoni A limekatika na kuua mzee moja aliyebeba mzigo mgongoni akijaribu kuvuka. Tunaomba Serikali ya CCM itusaidie kulijenga kwani diwani wetu ni wa CHADEMA !!
 
Kama mlichagua chadema imekula kwenu. Jichangeni mtengeneze wenyewe. Hii nchi kwa sasa ni mali ya ccm na wanaccm. Kodi zenyewe wanakusanya za ccm tu. Wakikusanya kodi kwenu ujue wanafanya kujazia jazia tu
 
Wakati wa mvua kubwa kunyesha .Daraja la Ulongoni A limekatika na kuua mzee moja aliyebeba mzigo mgongoni akijaribu kuvuka. Tunaomba Serikali ya CCM itusaidie kulijenga kwani diwani wetu ni wa CHADEMA !!
Ulongoni A ni Moshi au wapi bwashee?!
 
Wakati wa mvua kubwa kunyesha .Daraja la Ulongoni A limekatika na kuua mzee moja aliyebeba mzigo mgongoni akijaribu kuvuka. Tunaomba Serikali ya CCM itusaidie kulijenga kwani diwani wetu ni wa CHADEMA !!

Hapo kunahitajika daraja kwa walipakodi,ungetaka kuzungumzia uchama ungeelezea mzee Alibeba mzingo alikuwa mwanachama wa Chadema au CCM.
 
Ahsante sana nafikiri we ndo mkurugenzi atakayetukoa .Ulongoni A iko Goms Dar es salaam ipo kati ya Goms na Kinyerezi
Kama mlichagua chadema imekula kwenu. Jichangeni mtengeneze wenyewe. Hii nchi kwa sasa ni mali ya ccm na wanaccm. Kodi zenyewe wanakusanya za ccm tu. Wakikusanya kodi kwenu ujue wanafanya kujazia jazia tu
Ahsante sana nafikiri we ndo mkurugenzi atakayetukoa .Ulongoni A iko Goms Dar es salaam ipo kati ya Goms na Kinyerezi
 
Kama mimi ni CCM na wengi hapa ulongoni ni ccm ,basi watujengee daraja letu watu wa ccm pekee yetu
 
Sasa ujengewe daraja kwakuwa wewe ni CCM au daraja lijengwe kwakuwa wananchi wanapata Tabu??
 
Mkuu unanionea bure. Nimewakilisha mawazo ya watawala (ccm). Kwani wewe huwasikii wanayohubiri na kutenda wakiwa majukwaani?
Hahaaaa!! Sorry mkuu!! Kwani wanatia hasira kweli utadhani ndio wenye uhalali na nchi hii, wengine ni ma foreigners!!
 
Yani daraja la ulongoni A,limekatika,la ulongoni B lina mwaka wa pili au wa tatu tangu likatike,la pugu lina mwaka wa pili nalo tangu likatike,na haya yote yanaunganisha ulongoni, kinyerezi na gongo la mboto.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati wa mvua kubwa kunyesha .Daraja la Ulongoni A limekatika na kuua mzee moja aliyebeba mzigo mgongoni akijaribu kuvuka. Tunaomba Serikali ya CCM itusaidie kulijenga kwani diwani wetu ni wa CHADEMA !!

Unamaanisha daraja la kwenye mteremko mkali karibu na kiwanda cha nguo
 
Umeandika kwa mihemuko ya kisiasa sana, hoja yako ingeweza kuwasilishwa bila hata siasa ndani yake. Ni haki ya wananchi kujengewa daraja lakini wewe umeandika kana kwamba serikali imekusudia kukata hilo daraja ili waliochagua CDM wapate tabu. Jifunze kuwa neutral unapowasilisha vitu vya msingi kama hivi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom