Daraja la Nzali (Dodoma) lililogharimu Bilioni 14.5 laanza kutumika, ujenzi wafikia 98%

Daraja la Nzali (Dodoma) lililogharimu Bilioni 14.5 laanza kutumika, ujenzi wafikia 98%

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema Rais Samia Suluhu Hassan ameleta tabasamu kwa Wananchi wa Nzali na Itiso baada ya kuanza kutumika kwa Daraja la Nzali lililogharimu Shilingi Bilioni 14.5 ambalo limekuwa ni suluhisho la changamoto kubwa zilizokuwa zikiwakabili wananchi kwa miaka mingi, hususan wakati wa mvua.

Akizungumza katika hafla ya kuruhusu matumizi ya daraja hilo, Senyamule alisema kabla ya ujenzi wake wananchi walikumbwa na adha mbalimbali ikiwemo vifo vya watu na mifugo, kupotea kwa mali, wagonjwa kushindwa kufika hospitalini kwa wakati, watoto kukosa masomo na wakulima kushindwa kusafirisha mazao yao.

Pia soma ~ Bashungwa aagiza Daraja la Nzali-Chamwino kujengwa haraka

Alisema Rais Samia, kwa kujali maisha na ustawi wa wananchi, aliamua kupeleka fedha hizo Nzali ili kuhakikisha wananchi wanapata daraja litakalowawezesha kufanya biashara, kupata huduma za afya kwa wakati na watoto kuhudhuria shule bila vikwazo.
Daraja la Nzali.jpg

Daraja la Nzali1.jpg

WhatsApp Image 2025-12-22 at 17.09.25_8905678c.jpg
Aliongeza kuwa hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 98 na daraja limeanza kutumika rasmi huku kazi ndogondogo zikiendelea.

Senyamule aliwataka wananchi kutumia fursa ya uwepo wa daraja hilo kuchochea shughuli za kiuchumi kwa kusafirisha mazao na kuendeleza biashara, sambamba na kuwa walinzi wa miundombinu hiyo, akisisitiza kuwa Serikali itachukua hatua za kisheria dhidi ya watakaoharibu au kuiba miundombinu hiyo.
Daraja la Nzali445.jpg

Daraja la Nzali23.jpg
Kwa upande wake, Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Zuhura Amani, alisema ujenzi wa daraja hilo ulianza Novemba 15, 2024 na umehusisha daraja lenye urefu wa mita 60 na upana wa mita 11.4, makaravati manne pamoja na barabara ya maingilio yenye urefu wa kilomita 1.5.

Aliongeza kuwa Daraja hilo limefikia asilimia 98 huku asilimia mbili zilizobaki zikitarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 30 mwaka huu.
 
Africa tuna matatizo yaani kidaraja kama hicho ndio inakuwa habari
 
Liko wapi daraja la bilioni 14 hapo?? Uhuni mtupu
 
nimekokotoa 14 billion shillings to usd (exchange rate 1 usd = 2500tsh) nimepata kama 5.5 million usd, kwa hiyo hilo daraja ni zaidi ya 5 million usd kweli? ...

5.5 million usd ???
1766475316449.png
 
Upuuzi mtu, sifa zingine ni za kipuuzi, kwa daraja gani hapo la kutafuna 14 bilion!
 
Back
Top Bottom