Nyakijooga
JF-Expert Member
- Dec 9, 2018
- 506
- 806
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kenani Kihongosi, amekagua ujenzi wa Daraja la Kamishango lililopo katika Kata ya Ikondo, Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera. Mradi huo umetajwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 12.5.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Kihongosi amesema fedha zilizotumika kujenga daraja hilo zimetolewa na Serikali ya Tanzania, akibainisha kuwa licha ya kutajwa kuwa na ufadhili wa Benki ya Dunia, bado ni mkopo ambao taifa litalazimika kuurejesha.
Kihongosi ameeleza kuwa daraja hilo ni mkombozi kwa wananchi wa Muleba, likirahisisha usafirishaji, kukuza uchumi wa eneo hilo, na kuokoa maisha ya wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za kuvuka eneo hilo.
Aidha amewataka wananchi kushirikiana na serikali pamoja na CCM katika kulinda na kutunza miundombinu hiyo dhidi ya vitendo vya uharibifu na wizi wa vifaa, kama taa na mifumo ya nishati ya jua. Pia amesisitiza umuhimu wa kuzingatia matumizi sahihi ya daraja hilo ili lidumu kwa muda mrefu.
Itakumbukwe mwazoni mwa Mwezi January 2026 Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kagera, Mhandisi Julius Ryoba Festo alieleza kuwa daraja la Kamishango lina mita 45, upana mita 11.1 ambapo lilikuwa limefikia asilimia 97 ya ujenzi.
Pesa za ujenzi huo ulianza kufuatia ufadhiri wa Benki ya Dunia kupitia mpango wa dharura (CERC PROJECTS ) ambapo ilitangazwa kutolewa kiasi cha Shilingi Bilioni 45.6 kwa ajili ya kutekeleza miradi mitano ikiwemo Daraja la Kamishango ambalo limetajwa kugharimu Bilioni 12.5.
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Kihongosi amesema fedha zilizotumika kujenga daraja hilo zimetolewa na Serikali ya Tanzania, akibainisha kuwa licha ya kutajwa kuwa na ufadhili wa Benki ya Dunia, bado ni mkopo ambao taifa litalazimika kuurejesha.
Kihongosi ameeleza kuwa daraja hilo ni mkombozi kwa wananchi wa Muleba, likirahisisha usafirishaji, kukuza uchumi wa eneo hilo, na kuokoa maisha ya wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto za kuvuka eneo hilo.
Aidha amewataka wananchi kushirikiana na serikali pamoja na CCM katika kulinda na kutunza miundombinu hiyo dhidi ya vitendo vya uharibifu na wizi wa vifaa, kama taa na mifumo ya nishati ya jua. Pia amesisitiza umuhimu wa kuzingatia matumizi sahihi ya daraja hilo ili lidumu kwa muda mrefu.
Itakumbukwe mwazoni mwa Mwezi January 2026 Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Kagera, Mhandisi Julius Ryoba Festo alieleza kuwa daraja la Kamishango lina mita 45, upana mita 11.1 ambapo lilikuwa limefikia asilimia 97 ya ujenzi.
Pesa za ujenzi huo ulianza kufuatia ufadhiri wa Benki ya Dunia kupitia mpango wa dharura (CERC PROJECTS ) ambapo ilitangazwa kutolewa kiasi cha Shilingi Bilioni 45.6 kwa ajili ya kutekeleza miradi mitano ikiwemo Daraja la Kamishango ambalo limetajwa kugharimu Bilioni 12.5.