Hiyo sheria ipo toka zamani ingawa ilikuwa haitekelezwi. Tofauti ni kwamba hapo awali kila shirika lilipaswa kuchangia 10% ya FAIDA yake kwa mwaka, ikaonekana mashirika mengi yana declare faida kidogo kwa kutumia mbinu za kihasibu (creative accounting or earnings management), ndo maana sasa wameamua kuicharge kwenye MAPATO GHAFI. Angalia repoti za CAG miaka iliyopita. Mashirika kamaTANAPA, EWURA, TCRA n.k yanapata hela nyingi sana, matokeo yake wanaishia kujipangia posho kubwa za vikao vya board na perdiems na safari za nje kibao. Wakati rate za posho za kujikimu za juu serikalini ni 80,000, yapo mashirika wajumbe wake wa board wanalipwa hadi 450,000 per day na bado analipiwa tiketi ya ndege, malazi, chakula na vinywaji. Posho za vikao zinafikia hadi 1,000,000 per sitting. Naunga mkono uamuzi wa serikali