Ila kati ya usafiri wa ilimradi ufike basi ni wa daladala,
Yaani upo ndani chini unaona lami,
Viti mobile, unatoka tabata upo nyuma unafika mjini upo mbele,
gari ikiingia kwenye shimo na wewe lazima uwende kwenye roof, ukishuka kiti kishaenda na mwenzako,
ukinunua maji hunywi mpaka ufike, au labda uinue shingo kama kuku, ukinunua karanga pact unafika umekula 2, nyingine zote zinapishana na mdomo,
Ikinyesha mvua unavujiwa,
Hapo hujapigwa Ndole, Wazee wa dunga dunga, huajamwagikiwa na Shombo ya Samaki..
Teja asipopewa 100 na konda, gari iking'oa anakulaba kibao.
Dar mtu akianza kununua gari kabla ya kujenga binafsi namuelewa.