Ndugu wanaJF na wapenda maendeleo, jana (April 25, 2011) nilikuwa Kimanzichana (Wilaya ya Mukuranga) na nilipanda Hiace moja inayoitwa BABYLON T 932 BHE (mali ya Othman M Hassan PO Box 273, Zanzibar) kwenda Dar es Salaam.
Tulipokaribia Mbagala Rangi Tatu (kwenye saa mbili hivi usiku) kulikuwa na foleni ya magari lakini ilikuwa inaenda taratibu. Ilikuwa kama nusu kilomita hivi kufika kituoni Mbagala Rangi 3. Kilichofanyika dereva alisimamisha gari na kutuambia tuteremke huku akisema anataka kwenda kupaki gari na haendi sehemu yoyote zaidi ya pale aliposimamisha gari. Alisema dereva ndiye anayeamua wapi awateremshe abiria na kama tunataka kwenda kushtaki polisi twende hana wasiwasi kwani hata akienda ndani hatakaa muda mrefu na amezoea hali hiyo.
Baadhi ya abiria (hasa wale ambao walikuwa wamefika na pengine hawakuwa na mizigo mizito waliamua kushuka) na abiria watano hivi tuliamua kubaki na kuendelea kudai atufikishe kituoni kuliko kutuacha mbali vile maana wengine walikuwa na mizigo mizito. Hata kama wasingekuwa na mizigo mizito utaratibu ni kufika kituoni na si sehemu dereva anayoamua awateremshe abiria. Tulijaribu kumwelemisha kuwa tulipopanda gari na kulipa nauli 2,000/- tuliingia mkataba kutoka ituo cha Kimanzichana hadi cha Mbagala Rangi 3 tu.
Kulikuwa na mabishano sana kati ya dereva + konda wake upande mmoja na sisi abiria tuliokuwa tumebakia ndani ya lile gari. Kisha kwa shingo upande akaamua kutusogeza mbele kidogo na kusimama katikatika ya maji machafu akidai atatupeleka hadi kituo cha Mbagala Rangi 3 pale foleni itakapopungua.
Tulibaki pale kwa muda wakati magari mengine yalikuwa yakipita. Alifanya hivyo makusudi kutukomesha kwa vile aliona tunadai atende haki na siyo kutumia lugha mbaya na mabavu kwa vile tumeishalipa nauli. Baadaye alilitoa gari kwenye yale matope na kupaki sehemu kavu na akasema kama tunataka kubaki ndani tubaki na yeye haendeshi gari tena. Muda huo foleni ilikuwa imeshaanza kupungua.
Kwa kweli mimi niliumia sana hasa kuona kuwa abiria tunanyanyasika kwa namna ile, Kisha lisema hatuna hela kama tungekuwa na hela tusingepanda daladala.
Nilitaka kupiga simu kwa mwenye gari kulalamika lakini tiketi tulizopewa hazikuwa na namba ya simu ila jina na anwani yake tu. Kwa vile sisi wanaJF tunapenda maendeleo katika nchi yetu na pia tunapenda wanaofanya biashara wafanye kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa, naomba kama kuna mwanaJF anamfahamu mwenye daladala hii ya BABYLON amjulishe kuwa dereva na konda wake ni wahuni watamharibia biashara. Ni afadhali aweke watu wastaarabu na siyo wahuni kwa vile wanalipwa kidogo.
Naomba wanaJF tuisusie Hiace hii kwa sababu ya dereva na konda wake kutumia lugha chafu na ya kudhalisha dhidi ya abiria badala ya kutumia lugha ya kistaarabu na inayowafanya abiria wapende huduma za gari hili. Naomba maoni yenu.
Tulipokaribia Mbagala Rangi Tatu (kwenye saa mbili hivi usiku) kulikuwa na foleni ya magari lakini ilikuwa inaenda taratibu. Ilikuwa kama nusu kilomita hivi kufika kituoni Mbagala Rangi 3. Kilichofanyika dereva alisimamisha gari na kutuambia tuteremke huku akisema anataka kwenda kupaki gari na haendi sehemu yoyote zaidi ya pale aliposimamisha gari. Alisema dereva ndiye anayeamua wapi awateremshe abiria na kama tunataka kwenda kushtaki polisi twende hana wasiwasi kwani hata akienda ndani hatakaa muda mrefu na amezoea hali hiyo.
Baadhi ya abiria (hasa wale ambao walikuwa wamefika na pengine hawakuwa na mizigo mizito waliamua kushuka) na abiria watano hivi tuliamua kubaki na kuendelea kudai atufikishe kituoni kuliko kutuacha mbali vile maana wengine walikuwa na mizigo mizito. Hata kama wasingekuwa na mizigo mizito utaratibu ni kufika kituoni na si sehemu dereva anayoamua awateremshe abiria. Tulijaribu kumwelemisha kuwa tulipopanda gari na kulipa nauli 2,000/- tuliingia mkataba kutoka ituo cha Kimanzichana hadi cha Mbagala Rangi 3 tu.
Kulikuwa na mabishano sana kati ya dereva + konda wake upande mmoja na sisi abiria tuliokuwa tumebakia ndani ya lile gari. Kisha kwa shingo upande akaamua kutusogeza mbele kidogo na kusimama katikatika ya maji machafu akidai atatupeleka hadi kituo cha Mbagala Rangi 3 pale foleni itakapopungua.
Tulibaki pale kwa muda wakati magari mengine yalikuwa yakipita. Alifanya hivyo makusudi kutukomesha kwa vile aliona tunadai atende haki na siyo kutumia lugha mbaya na mabavu kwa vile tumeishalipa nauli. Baadaye alilitoa gari kwenye yale matope na kupaki sehemu kavu na akasema kama tunataka kubaki ndani tubaki na yeye haendeshi gari tena. Muda huo foleni ilikuwa imeshaanza kupungua.
Kwa kweli mimi niliumia sana hasa kuona kuwa abiria tunanyanyasika kwa namna ile, Kisha lisema hatuna hela kama tungekuwa na hela tusingepanda daladala.
Nilitaka kupiga simu kwa mwenye gari kulalamika lakini tiketi tulizopewa hazikuwa na namba ya simu ila jina na anwani yake tu. Kwa vile sisi wanaJF tunapenda maendeleo katika nchi yetu na pia tunapenda wanaofanya biashara wafanye kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa, naomba kama kuna mwanaJF anamfahamu mwenye daladala hii ya BABYLON amjulishe kuwa dereva na konda wake ni wahuni watamharibia biashara. Ni afadhali aweke watu wastaarabu na siyo wahuni kwa vile wanalipwa kidogo.
Naomba wanaJF tuisusie Hiace hii kwa sababu ya dereva na konda wake kutumia lugha chafu na ya kudhalisha dhidi ya abiria badala ya kutumia lugha ya kistaarabu na inayowafanya abiria wapende huduma za gari hili. Naomba maoni yenu.