Dada yangu ndoa yake ina mgogoro 4 2months, wana 12yrs, ndoa yakikristo, 3kids ke 10yrs, me 8yrs, me 4yrs. chanzo ni uzinzi wamume uliokithiri, anazini na wanafunzi, wanawake wamtandaoni, karibu kila kona anahawara, mara yamwisho dada alifuma sms kwenye simu ya shem, inasema,
''mke wangu nakumiss sana napanga nije tena Arusha tumtafutie Bryan mdogo wake amekua sana, mke huyo akamjibu we mi naogopa usije ukanitelekeza tena.''
Dada akamuuliza kumbe una hawara hadi umezaa nae? Mume kawa mkali anadai dada hana adabu kwanini apekuepekue simu yamumewe? Mke akalia sana mume hajali, sasa hawasemeshani kilammoja anafanya lake, mke anajiendeleza chuo, hutoka asubuhi anarudi jioni kimya, jana kaja kwangu tumeshinda kanisani maombi, kufika kwake ugomvi ukatibuka mume anadai J4 ataenda kumpa talaka mahakamani sababu anakiburi eti watu huishi nawanaume malaya nakuwaheshimu, kwanini ye hamheshimu kaambiwa awaache watoto kwamume, namali zote haziache nizawatoto, mume ataziangalia, dada anataka wanae na mali.
Je, atapewa wanae namali kweli?
1. Mahakama pekee ndo chombo cha kisheria kuvunja ndoa.
NOTE: Kuvunja ndoa maana yake ni MAhakama inatoa TALAKA.
NOTE: Spouse yeyote (me au ke) anaweza kwenda mahakamani kuomba kuvunja ndoa.
2. Ili ndoa ivunjwe, (yaani mahakama iridhike na ushahidi na kutoa TALAKA), inabidi wanandoa wapitie kwanza kwenye Baraza la Usuluhishi la Ndoa (Marriage Reconciliation Board) ili wasuluhishwe kwanza. Suluhu isipopatikana hapo, ndo suala linakuwa referred to Court ambapo huko sasa itafunguliwa kama kesi ya kawaida ya madai, na muombaji-talaka atatakiwa kutoa ushahidi wake as to why anaomba ndoa ivunjwe.
NOTE: Hizo marriage reconciliation boards ni: Baraza la Kata and/or Baraza la Kanisa (hii ni kwa wakristo); BAKWATA (hii ni kwa waislamu)
3. NDOA ikishavunjwa rasmi (yani TALAKA ikitolewa), kuna mambo makuu matatu hufuatia:
(a) Distribution of Matrimonial Properties - Mgawanyo wa mali za ndoa.
(b) Custody of children - Kwamba ni nani (kati ya baba au mama) atakaa na watoto.
(c) Maintenance of children - Kwamba ni nani (kati ya baba au mama) ataprovide matunzo kwa watoto, bila kujali wanakaa kwa yupi.
NOTE: Hapo kwenye (a), matrimonial properties ni zile mali ambazo zimechumwa/zimepatikana kwa juhudi za pamoja (jointly acquired) ndani ya ndoa yenu, yaani ni zile ambazo zimepatikana kuanzia ile tarehe mlipofunga ndoa rasmi. Hata kama zilipatikana jointly ila
kabla ya kufunga ndoa, basi uwe na ushahidi wa kuthibitisha hilo ili upate haki yako.
NOTE: Hapo kwenye (a), sheria inatambua uwepo wa mali binafsi katika ndoa, yaani kila mwanandoa anaweza kumiliki mali zake yeye mwenyewe binafsi, separately na zile mali za ndoa. Mali hizi za umiliki binafsi huwa hazijumuishwi kwenye mgao wa mali za ndoa. So hapo pia ni suala la ushahidi ili usidhurumiwe.
NOTE: Hapo kwenye (b), Kisheria, mtoto mwenye umri chini ya miaka 7, inatakiwa akakae kwa mama. Cha msingi hapa ni kwamba katika kuamua mtoto akakae kwa aidha mama au baba, Mahakama huzingatia zaidi maslahi bora na ustawi wa mtoto (the best interest of the child) mfano uwezekano wa kupata malezi bora ya kimaadili, elimu, n.k. Mfano: mama kama ana tabia za ulevi wa kupindukia, au labda mama huwa ana matatizo ya akili, au labda ni mtu wa kusafiri-safiri sana, au labda ana tabia chafu na ushahidi ukatolewa, basi Mahakama is likely kumnyang'anya/kumnyima mtoto. Pia katika hili, mtoto mwenyewe huulizwa kwamba je anapenda akae na nani.
NOTE: Hapo kwenye (c), kisheria, baba (biological father) ndo mwenye responsibility kubwa katika matunzo ya mtoto/watoto, regardless wanakaa kwa yupi. So, ata kama mahakama ikaamua kwamba watoto wakakae kwa mama, still baba anabanwa kisheria kuprovide full matunzo kwa watoto. Endapo baba hajiwezi kiuchumi ama hajiwezi kivyovyote vile, basi mama pia ana responsibility ya kutoa matunzo kwa mtoto/watoto. So, jukumu la matunzo kwa watoto ni la wote baba & mama.
Mkuu
cloudear, hopefully umepata majibu ya hoja yako kwenye maelezo hayo mafupi.
-Kaveli-