Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 9,502
- 19,302
Huyo ameshakuwa gaidi, mark my words. Soon atamwona Somalia na alshabab.Dada yangu 49 years now ameajiriwa kwenye Hospitali Binafsi kubwa sana hapa Dar , ana kijana wake wa kiume ambae ndio alitegemea aje hata aonyeshe njia maana watoto wake wengine ni tia maji wote wanamsumbua huyu ndio alijua atakuja kumfuta machozi, Cha kwaza kijana wakati yupo form six tu walifukuzwa shule yeye na wenzake 4 sababu ya kuanzisha makundi ya kidini yenye misimamo isiyoeleweka na kufanya vurugu, ikabidi Dada amtafutie shule nyingine private kwa garama kubwa kumnusuru.
Dogo akamaliza Advance akaaply Chuo cha udaktari Tanga huko hali ilivyokuwa ngmu maana Baba yake hakuwa na msaada wowote Dada akakopa sh milioni 5 pale kazini kwake kwa ajili ya kumsomesha tena hiyo milioni 5 ilikata ikabidi awe anapambana kuongezea hela sehem nyingine, Dogo akapiga kitabu akamaliza kwa tabu sana.
Mwaka 2020 Dada kwa sababu ni Mkongwe pale kwenye Hosptitali anayofanya kazi akafanya juu chini kumuombea nafasi na moja kwa moja Dogo akapata nafasi ya kuajiriwa kama Daktari
Balaa likaanza Dogo baada ya kujiriwa tu akawa anakuja kazini Amevaa Nusukanzu,Kobazi na Kibarakashia huku Anafuga Ndevu kama Osama, hadi akawa anatisha waajiri wake ikabidi Sister aitwe haraka sana akaambiwa kuwa Huyu kama ni mwanao basi kaa nae umkanye mara moja kuwa Yale hayakuwa mavazi sahihi kwa mafanyakazi akashauriwa kuwa avae mavazi official ambayo yapo kwenye muongozo kwa mujibu wa kazi
Sister ikabidi amuite Dogo amkanye kuwa Uongozi pale wamemkanya ajirekebishe ile ni Hospitali kubwa na ni lizima afuate miongozo, Dogo akawa mbishi na alipoona anazongwa sana kwa lile swala akaacha kazi kabisa kwa Hasira akaenda mikoani huko akawa anajihusisha na mambo ya kidini
Kuanzia kipindi hicho Dada yangu ni presha za kupanda tu na kushuka, Juzi kati hapa hadi akazimia maana kijana alikengeuka akawa hamuheshimu na hama maisha ya kueleweka tena na ukiangali amechoma zaidi ya milioni 7 kumsomeaha na hadi leo hii hana kiwanja wala nyumba amepanga