Dada huyu anaomba ushauri wenu tafadhali

Dada huyu anaomba ushauri wenu tafadhali

KIBURUDISHO

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2011
Posts
1,002
Reaction score
278
Nina umri wa miaka 28,mwaka huu mwezi wa nane nimehitimu diploma ya uuguzi ktk chuo fulani hapa nchini.Kitu kilichopelekea kuja hapa kuwaombeni ushauri ni juu ya ni mwanaume gani atakayenifaa juu ya suala zima la ndoa kwa maana imefika muda sasa ninahitaji kuwa ndani ya ndoa.Tatizo linakuja hivi mimi kiumbo ni mrefu hivyo moja ya sifa ambayo nilijiwekea ya mwanaume wa sifa zipi nitapendezwa nae atakayenioa ni awe mrefu kama mimi na sii mfupi hata tukitoka naona kama haitakuwa inapendezea.Sasa hivi karibuni kama mwezi mmoja uliopita nimekuwa nikiwasiliana kwa simu na mwanaume nisiyemfahamu hadi hapo alipojitambulisha kuwa aliniona kwenye mahafali yangu ya kuhitimu kwangu mwaka huu mwezi wa nane na aliyempa namba yangu ni mwanafunzi mwenzangu.Moja ya kitu alichonieleza ni kuwa alivutiwa/alipendezwa sana na mimi,na anahitaji sana kuwa kwa maana ya kuianzisha familia.Nilimjulisha kuwa kwa upande wangu nina mtoto mmoja wa miaka minne,aliniambia yeye ananipenda na anampenda pia mwanangu na kila anapopiga simu huniomba nimpe mtoto wasalimiane nae.Toka anapewa namba yangu hadi tunafanya mawasiliano sikuwa namfahamu au kuonana ana kwa ana yeye aliniambia yuko Songea hivyo aliniomba aje kunitembelea nilimkubalia,alikuja akafikia kwangu ila moja ya sifa ninazozihitaji hakuwa nazo yeye ni mfupi tukisimama naye ananifikia kwenye kifua.Sikutaka kuonyesha kuwa amekuwa kinyume na matarajio yangu nilimpa makaribisho vizuri ila hakulala kwangu alifikia hoteli.Kwa upande wake anasema anahitaji sana kuwa na mimi ndani ya ndoa ki umri yeye ana miaka 36.Kiukweli bado sijamwambia kuwa napenda kuolewa na mwanaume mrefu tunayelingana.Changamoto iliyo juu yangu nifanyeje ni ndani ya miezi miwili toka tumefahamiana ila yeye anahitaji kama ikiwezekana tuharakishe jambo hili ili niolewe naye.Naombeni mawazo yenu kwa kina ili nitakapofanya maamuzi yawe ya kweli na sahihi.
 
Asiwe na haraka,miaka 28 sio mingi kihivyo.
 
kama hana sifa unazozihitaji meleze ukweli usimpotezee muda
 
mh!MY DEAR
Urefu na ufupi ni mambo ya nje sana ambayo kiukweli sidhani kama i moja ya vigezo vya kukufanya uwe na ndoa bora!
ndoa ni kukamilishan wewe ni mrefu mkamilshe mwenzio kwa ufupi wake!
kwanza huo urefu unauona nje tu akiwa ndani huyo boooonge la tolu!
pili urefu wa mtu huanzia kiunoni kwenda juu chini wala poa tu!hebu jiachie mwanakwetu unless kama hujmpenda huyo kaka!
hizo nyingine story lakini la msingi ni hili
NDOA NI ZAIDI YA MAUMBILE YETU YA NJE!
 
Dada ndoa ni bahati, sasa chunga sana yawezaikawa hiyo ndio bahati yako kwasasa, unaweza ukapenda alafu we usipendwe!
 
mwambie ukweli tuu kuwa hapa umegonga mwamba....kwanza hao wafupi wakorofi balaaa.
another thing miezi miwili michache sana huyo atakuwa na lake jambo. mpotezee kabisa
 
"Mchagua nazi huambulia koroma". Pia kuwa makini usije ukaimbiwa ule wimbo....dada anaolewaaa, madunga embe yamebakiaa..
 
Mbona hata wanaume wafupi wanataka wanawake warefu? sasa itakuwaje kama na wanawake warefu hawataki wanaume wafupi?? Ukimkubalia halaf badae aje mwanaume mrefu itakuwaje?? mimi sidhani kama ni kigezo muhimu sana labda awe mfupi kupitiliza. Sifa za muhimu ni kama uaminifu, upendo na tabia
 
Vipi unahisi alivyo mfupi na nanihii yake itakua fupi??
 
Nenda Rwanda, wapo wanaume warefu sana.
 
mbona umejiita kiburudisho mpenzi?la pili ndoa ni zaidi ya urefu na ufupi mara nyingi watu tunapotaka kuolewa ama kuoa huwa tunaangalia mambo ya muda mfupi sana au vitu vya nje ukishaingia na kujifunza zaidi unagundua maisha ni zaidi ya uzuri wa nje ambao unaisha na kupotea baada ya muda.
 
namshauri amchunguze kwa kama 2years huyo mtu asije mwaribia maisha wengine majini ati au katumwa usimwamini kila mtu ndufgu yangu!!!!!!!
 
Mh acha usubiri warefu waje, kama hujaja mtafuta miaka 4 ijayo na ukamkuta akiwa na mke by that time...wengi wametokewa na bahat kama zko na kudeka na kuzitafuta bdae kwa udi, tena ushazaa na jamaa kafumbia macho we bado unaomba ushauri hapa, endelea kuomba na kwingne
 
NDOA HAINA TBS, WENGI TULIKUWA NA TBS ILA TUKA ZI ABANDON, 28 HALAFU UNA MTOTO bado una aply MS (MS=MAN STANDARDS) SUBIRI UTAPATA AMBAYE ANAKUFUKIA KWENYE KIUNO.
 
mhhh bado hujapenda wewe??? Ndio mana unapata nguvu ya kuzungumzia maumbile.
 
Maumbile syo chanzo cha kutompenda mwenzako mkubalie .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom