CWT acheni kuwatisha waliokuwa wanachama wenu!

CWT acheni kuwatisha waliokuwa wanachama wenu!

Mnasihi

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2013
Posts
8,362
Reaction score
7,861
Kuna ziara zinafanywa na maofisa wa cwt kwenye matawi yao yaani mashuleni. Agenda yao kuu ni kutafuta maoni ya wanachama katika kuiwekea kiraka kama siyo viraka katiba yao baada ya walimu kujiunga ma chama kipya cha chakamwata! Katika moja ya changamoto ni hii wanayoinadi juu ya walimu wote wasio wanachama kukatwa ada ya agency fee ambayo inalingana na ada ya mwanachama (membership fee) ya 2%.

Hoja hapa ni kuwa, hivi ni halali kwa agency fee kulingana na membership fee? Kama ndiyo, huyu mwanachama anailipaje agency fee?

Changamoto hii imewakera walimu na kiukweli inahitaji marekebisho ili agency fee iwe na kiwango kidogo kuliko membership fee kwani siyo lazima mwalimu awe mwanachama wa cwt!

Walimu hawahitaji vitisho bali ushawishi wa kuwabakisha kwenye chama ambacho hakijawahi kuwasaidia kutatua changamoto zao.
 
Kuna ziara zinafanywa na maofisa wa cwt kwenye matawi yao yaani mashuleni. Agenda yao kuu ni kutafuta maoni ya wanachama katika kuiwekea kiraka kama siyo viraka katiba yao baada ya walimu kujiunga ma chama kipya cha chakamwata! Katika moja ya changamoto ni hii wanayoinadi juu ya walimu wote wasio wanachama kukatwa ada ya agency fee ambayo inalingana na ada ya mwanachama (membership fee) ya 2%.
Hoja hapa ni kuwa, hivi ni halali kwa agency fee kulingana na membership fee? Kama ndiyo, huyu mwanachama anailipaje agency fee?
Changamoto hii imewakera walimu na kiukweli inahitaji marekebisho ili agency fee iwe na kiwango kidogo kuliko membership fee kwani siyo lazima mwalimu awe mwanachama wa cwt!
Walimu hawahitaji vitisho bali ushawishi wa kuwabakisha kwenye chama ambacho hakijawahi kuwasaidia kutatua changamoto zao.
 

Attachments

  • 15356071544821789988541.jpg
    15356071544821789988541.jpg
    747.1 KB · Views: 38
Hapo umesaidia sana kuelimisha kwa kuiweka hii nakala ya sheria ya vyama vya wafanyakazi.
Wao cwt wanasema tofauti na sheria hii eti, ada ya dirisha la uwakala kwa asiye mwanachama ni sawa kabisa na ada ya mwanachama! Jambo hili limewatisha walimu waliojotoa uanachama kwa kuwa wameambiwa kuwa watakatwa asilimia tatu kwa maana ya 1% ya ada ya chakamwata na 2% ada ya dirisha la uwakala!
Siamini kama hawa cwt wameisoma sheeia hii na kuielewa na ama wanawatisha walimu ili waendelee kula pesa zao!
Nitoe rai kwa walimu waliochoshwa na wizi huu wa cwt wasiogope na wasisite kuikataa na kujiunga na chama wanachokiamini na chenye kukata 1% ili hiyo 1% inayobaki iwasaidie kwenye mahitaji mengine.
Cwt kimegeuka adui wa walimu kwa makato makubwa huku kikishindwa kumtetea mwalimu. Yaani hata katiba za chama wameshindwa kuzipeleka matawini licha ya michango mikubwa wanayoikata kwenye mishahara ya walimu! Nimemshauri mwanangu ajitoe kabisa na kujiunga na chakamwata ili hiyo1% inayobaki kwake anunulie japo bando!
 
Back
Top Bottom