CUF wakubali kutoa mgombea mwenza UKAWA

CUF wakubali kutoa mgombea mwenza UKAWA

AirTanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2011
Posts
1,139
Reaction score
1,040
Vikao vya CUF vimemalizika na wamekubalia kuwa CUF watatoa mgembea mwenza na CHADEMA watoe mgombea urais.

Juma Duni ndie atakaye kuwa mgombea mwenza kupitia CUF. Kutokana na CHADEMA kutoa Mgombea urais sheria inasema pia mgombea mwenza atoke chama hicho hicho kinachotoa rais.

CUF wamekubali mgombea wao kujiunga na CHADEMA na kuwa mwanachama wa CHADEMA kwa muda ili aweze kuteuliwa kuwa mgembea mwenza kupitia chama hicho.

Mazungumzo baina ya Lowassa na CHADEMA bado yanaendelea
 
Safi Sana CUF Kwa Ukomavu . Tumechoka na Kupewa Kanga na Kofia za Misisiem. Umoja ni Ushindi Viva UKAWA.
 
Hii iko poa sana. Masaa 24 ya uanachama yanatosha kabisa kuteuliwa.
 
Nauliza hivi, mbona viroba vya konyagi vimepanda bei kinyemela?

Demand imekuwa kubwa. Supplier wachache. Ila kama vp kunywa nzagamba , banana ., Tingisha. Kama upo dar nitafute mitaa ya Goba eneo linaitwa mtaa wa zambi.
 
Nina wasi wasi na hii thread, kama yanayosema ni kweli. Kama ni kweli KUDOS, CUF
 
Kwahiyo mgombea mwenza akiamia chadema cuf itanufaika na nini?
 
Nina uhakika EL ataleta shida kubwa sana ndani ya CCM
 
Nimeamini CUF wameonyesha ukomavu mkubwa kwa ajili ya mustakabali wa Taifa hili. Hongera CUF na Prof Lipumba kwa kuweka pembeni maslahi binafsi
 
hongereni sana cuf. tuiondoe kwanza ccm madarakani hayo mengine ni madogo sana kulinganisha na hili, ninahakika hayatawashinda viongozi wetu wa ukawa kuyaweka sawa, japo tutegemee vijidhoruba vya hapa na pale baada ya ushindi
 
mtatuua na tetesi mwaka huu. bora cdm wakate tena jina lake
 
firaha yangu ni slaa na duni.. lowasa awe mwanachama tu..
 
Back
Top Bottom