CUF tunakubalika bara na Zanzibar

Swali ambalo CUF wanatakiwa watujibu watanzania ni kwanini walikuwa wepesi kukubali kuungana na CCM kuunda serekali ya mseto Zanzibar na kuwa wepesi wa kutaka kujitoa kwenye umoja wa UKAWA ambapo ingekuwa rahisi kuiondoa CCM madarakani?.
busara zilitumika na sio fujo ndo maana ikawa rahisi
 

Cuf ngangari...haki sawa kwa wote!

chadema wanataka wasikilizwe wao tu

Kumbe.ni kweli.CUF wamejitoa UKAWA,nilikuwa nadhani ni tetesi
 
Tatizo ni RUZUKU.. Ama kweli mkombozi wa kweli ni wewe mwenyewe usimuamini mtu.
 
Kwa malumbano haya hakuna sababu ya kushirikisha vyama hivi pamoja ktk uchaguzi mkuu ( havipendani wala havitaeshimiana mbele ya safari)
 
Salum Mwalimu hawezi kuwa mgombea mwenza?

Wapo wengi tu wanaoweza kuwa wagombea ukiacha salim mwalimu, kwanza nadhani salim mwalim umri bado, na pia kama sikosei kachukua form ya ubunge jimbo gani sijui huko znz, majina ya huko nj shida kutamka, sijui makunduchi,
 
cuf kama mna kubalika bara msingekuwa na wabunge wa2 acha masihara wewe cdm wana vijana machachari hawawez kufanana na vilaza kama shaweji mketo na abdul kambaya

Bavicha katika ubora wao
 
Tunachotaka ni umoja kwa wapinzani tuingóe ccm,haijalishi unakubalika wapi achaneni na kujisifu kusikosaidia kumtoa mdudu anayetafuna mali zetu wa watanzania na kuzidi kuona askari wetu wakiuwawa vituoni na majambazi
 
Swali ambalo CUF wanatakiwa watujibu watanzania ni kwanini walikuwa wepesi kukubali kuungana na CCM kuunda serekali ya mseto Zanzibar na kuwa wepesi wa kutaka kujitoa kwenye umoja wa UKAWA ambapo ingekuwa rahisi kuiondoa CCM madarakani?.

Hata wewe cuf kama ji chama chako kama kilivyo chadema cha mtei utakubari wafuasi wako wajiunge na chadema ili wapate fursa ya kuwa wabunge wa viti maalumu au kiongozi wa chama chako arudishe card ajiunge na chadema ili awe mgombea mwenza?? Kitendo kile ni kuiua cuf haiwezekani kabisa.
 
Tatizo la chadema ni ubinafsi na udini,hawataki muislamu lipumba aongoze ukawa
 
Hapo ndugu umeongea hao CUF wamefanya makubalioano (muafaka) mara ngapi na CCM natuona wanavodanganywa na hao CCM? unakumbuka ule muafaka wa 1999 wa bwa Anyauku.
 
Sio suala la udini ndugu kwa kiasi Fulani CUF bara imekufa lazima hapa tuondowe ubinafsi wetu CHADEMA inakubalika zaidi bara na kama CUF wakijitoa UKAWA basi baada ya uchaguzi hata huko Zanzibar itasambaratika , na watu wake utaona jinsi watakavo kimbilia CHADEMA.
 
Swali ambalo CUF wanatakiwa watujibu watanzania ni kwanini walikuwa wepesi kukubali kuungana na CCM kuunda serekali ya mseto Zanzibar na kuwa wepesi wa kutaka kujitoa kwenye umoja wa UKAWA ambapo ingekuwa rahisi kuiondoa CCM madarakani?.
Wakijibu hili swali najitoa jf
 
Haki sawa kwa wote ..CUF msikubali mmepelekwe pelekwe
 

Cuf mnakubalika Zanzibar hilo hakuna ubishi lakini bata mmepoteza mvuto,kama mngekuwa na mawazo mazuri ungekubali kuwaachia cdm urais tz,na kwa kupitia kura za ukawa mngeweza kuongeza idadi ya wabunge bara na madiwani,lakini kwa ubishi wenu mwisho wenu naona mita chache kutoka buguruni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…