Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Inanitatiza hapa. Inakuaje - katika vyama vikuu vya upinzani – CUF inaonekana kulala usingizi?
Hivi hili pingamizi Dr Slaa alilomuwekea JK kuhusu "hongo" kwa wafanyakazi CUF wao hawakuliona? Au ndiyo wanafanya kampeni zao za ki-uswahiba na CCM kufuatia "ndoa" yao (ya CCM na CUF) ya kule jikoni?
CUF wasijidanganye – CCM haina uswahiba kabisa na mtu hasa inapohusu kuachia madaraka.
Kule Visiwani, CUF wanakwepa kuweka pingamizi kuhusu ugombea wa Dr Shein pamoja na kwamba hana sifa za ugombea kule (chini ya Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar) kutokana na ukweli kwamba hakujiandikisha kama mpiga kura kule.
CUF watakuja juta. CCM na ZEC yake inaweza ikacheza rafu mbaya katika mchakato wa uteuzi wa wagombea katika uchaguzi huko, na CUF, kutokana na "ndoa" hiyo, wakashindwa kuweka pingamizi hivyo wagombea wa CCM wote wakapita bila kupingwa. Kwa nini CUF wanajibweteka kiasi hiki? CCM ina chembe gani ya uadilifu kukumbatiwa kiasi hicho?
Tuliona jinsi CUF, huku bara mwaka 2000 jinsi ilivyokuwa tishio kwa CCM hadi chama hicho tawala kikawa kinatumia mabavu kukikandamiza na kukisingizia kutega mabomu katika maeneo kadha jijini Dar. Lakini sasa hivi CCM haioni kama CUF ni tishio kwake na wao (CUF) wanalijua hilo.