UDINI! UDINI! UDINI! UDINI!! Mkuu udini utakuteketeza! Kama huwezi kusakata kabumbu kaa juu ya jukwaa upige makofi na kuwashangilia wanaume zako.
Kwani nini chanzo cha swali lako mkuuJamani bado nauliza CUF ina matatizo gani?
Acha visambaratike vibaki vikubwa viwili ili tupate nguvu kubwa ya kuiangusha CCM, by the way CUF sio chama cha kukitegemea tena ktk vyama vya upinzani. Kimeshapoteza mvuto kwa jamii, hasa Tanzania Bara, sijui visiwani labda bado wanakielewa.Siisikii CUF zanzibar na mikashikashi yake huku bara ndiyo kabisaa sijawahi waona huku mikoani tangu uchaguzi mkuu uishe zaidi ya uchaguzi wa Igunga walipopata aibu ya karne. Iko wapi ile CUF ya Mapalala iliyotingisha serikali bara na visiwani hadi kulazimika serikali kuingiza watu wao kuisambalatisha, ile CUF ya Seif imeenda wapi, labda sasa tutegemee hii mpya inayokuja ya Hamad Rashid. Hakika tunahitaji chama kingine cha tatu chenye nguvu baada ya CCM na Chadema.
Ha ha ha ha ha! Mbona bado kidogo sana; wako chini ya uangalizi maalumu wa daktari - complete bed rest. Mkuu bado kitambo kidogo sana utasikia vigelegele kama mtoto atafanana na baba au matusi na talaka kama atakuwa na nywele za singa.
Ultra sound imeonesha wana mimba ya pacha - CUF-HR (CCM-D) na CUF-SH (CCM-B original) ila mmoja kakaa vibaya, katanguliza masaburi. Kaa mkao wa kula.
Jamani bado nauliza CUF ina matatizo gani?