CRDB Mmeniweza. Nahama benki

CRDB Mmeniweza. Nahama benki

Selwa

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2010
Posts
671
Reaction score
699
Basi katika pita pita zangu nilikuwa mkoa flani weekend ya mwisho mwezi wa tano. Si unajua mambo ya furahi day nikaenda atm kutoa fedha nianze kuleta fujo mjini maana nilikuwa hata bati sina. Mimi ni mteja wa crdb so Nikaenda karibia ATM zao 3 mji mzima hazina network. kwa takribani maasaa 6. He... basi nikaona hebu nijaribu kutoa atm ya benki nyingine ya VISA. mdogo mdogo nikaenda NBC sasa baada ya kuweka kadi atm ikaandika 'Issuer not available' nikajua labda tatizo ni CRDB yenyewe ndo mana nikatulia nikarudi zangu home. hata dakika hazijapita niko njiani ikanijia messeji umetoa laki sita frm XXXX ATM. Heeee! mbona haikutoa hela? nikarudi ile atm na kweli ipo empty na sioni pesa yeyote nikamuuuliza mlinzi akasema inatokeaga ni mtandao piga hiyo namba kwenye msg (nilipiga ila haikupokelewa) basi kwasababu muda wa kazi ulikuwa ushapita nikaenda kesho yake kuripoti. Nikaandika details kiasi chenyewe, laki 6, Baada ya hapo ikawa ni kila siku kufuatilia ka miezi 6 napigwa tarehe tu . Mpaka meneja nikaenda kumwona wapiiiii. nimekuja kupewa jibu juzi kwamba Visa wameshindwa kunirudishia hizo hela kwasababu eti inaonekana nilizichukua? nikauliza imeonekana wapi??? mule kwenye atm hamna camera? maana kweli kwenye acount ilisema hela nimetoa wakati ile atm ilisema issuer not available.kibaya ilikuwa haina risiti!! nikawauliza hamuwezi angalia kwenye camera zao za security hao nbc au hata kuwaomba maana mimi ni mteja wenu na hio ni pesa yngu? wakasema hawawezi! nikabaki nimeduwaaa. laki sita mshahara wa mtu huo. lakini hamna shida. nimeamua kuhama tu benki na nawapa tahadhari na wenzangu kuhusu CRDB na VISA. me naona heri nihame benki tu. Mmezidi wizi.
 
pole mkuu. CRDB ina huduma mbaya sana siku hizi maana atm nyingi hazifanyi kazi.
huduma zao zimehamia kwenye fahari huduma ambako makato kwa mteja ni makubwa sana.
 
Basi katika pita pita zangu nilikuwa mkoa flani weekend ya mwisho mwezi wa tano. Si unajua mambo ya furahi day nikaenda atm kutoa fedha nianze kuleta fujo mjini maana nilikuwa hata bati sina. Mimi ni mteja wa crdb so Nikaenda karibia ATM zao 3 mji mzima hazina network. kwa takribani maasaa 6. He... basi nikaona hebu nijaribu kutoa atm ya benki nyingine ya VISA. mdogo mdogo nikaenda NBC sasa baada ya kuweka kadi atm ikaandika 'Issuer not available' nikajua labda tatizo ni CRDB yenyewe ndo mana nikatulia nikarudi zangu home. hata dakika hazijapita niko njiani ikanijia messeji umetoa laki sita frm XXXX ATM. Heeee! mbona haikutoa hela? nikarudi ile atm na kweli ipo empty na sioni pesa yeyote nikamuuuliza mlinzi akasema inatokeaga ni mtandao piga hiyo namba kwenye msg (nilipiga ila haikupokelewa) basi kwasababu muda wa kazi ulikuwa ushapita nikaenda kesho yake kuripoti. Nikaandika details kiasi chenyewe, laki 6, Baada ya hapo ikawa ni kila siku kufuatilia ka miezi 6 napigwa tarehe tu . Mpaka meneja nikaenda kumwona wapiiiii. nimekuja kupewa jibu juzi kwamba Visa wameshindwa kunirudishia hizo hela kwasababu eti inaonekana nilizichukua? nikauliza imeonekana wapi??? mule kwenye atm hamna camera? maana kweli kwenye acount ilisema hela nimetoa wakati ile atm ilisema issuer not available.kibaya ilikuwa haina risiti!! nikawauliza hamuwezi angalia kwenye camera zao za security hao nbc au hata kuwaomba maana mimi ni mteja wenu na hio ni pesa yngu? wakasema hawawezi! nikabaki nimeduwaaa. laki sita mshahara wa mtu huo. lakini hamna shida. nimeamua kuhama tu benki na nawapa tahadhari na wenzangu kuhusu CRDB na VISA. me naona heri nihame benki tu. Mmezidi wizi.

ilishawahi kunitokea mara mbili kwa crdb visa card kusoma muamala ambao sijaufanya baada ya kutumia atm za barclays..
at first transaction ilifeli ila nikakatwa elfu 60 niliyotaka kutoa... nlikuja kustuka late sana ikawa nimeliwa...miezi ya baadae kuna siku network ilikuwa down nkaenda kufyatua tena barclays.. muamala ukafeli ila nlistuka salio (laki) lilipigwa.. nkawapigia nikaambiwa niende tawi la bank la karibu.. nlienda kijitonyama.. NIKAJAZA CLAIM FORM.. ikinitaka nitaje tawi nlilotoa na kiasi cha miamala na pesa iliyokatwa kwa kila muamala..... (HILI LA KUDAI LINATAKIWA LIJAZWE NDANI YA SIKU 40 TANGU KULIMWA PESA YAKO)... luckily walinirudishia pesa yangu baada ya masiku kadhaa
 
CRDB siku hizi hamna kitu. Atm zao znasumbua kweli. Jaman jaribuni hata NMB na Posta. Zinasaidia sana wakat wa shida kama posta haina folen kabisa
 
kawaida bank ikishakuwa na wateja wengi haiwezi kuwahudumia vizuri
inadeal na corpote clients
 
Mleta mada...kama sijakosea kiwango kikubwa cha kutoa ni laki nne...kwa kila muamala.
Laki sita sijaelewa imekaa vipi mpaka upate hiyo meseji.
Pili inshu ya toka mwezi wa tano, ni vizuri ukafika katika matawi yao.
Wengine tunaishia kulalamika tu...
 
wana huduma mbovu sana awa ni kama kampuni flan la simu ukikosea tu kununua umeme wa Luku umeliwa hela yako utadai mwaka hawakupi muwe waangalifu na matapeli
 
Mleta mada...kama sijakosea kiwango kikubwa cha kutoa ni laki nne...kwa kila muamala.
Laki sita sijaelewa imekaa vipi mpaka upate hiyo meseji.
Pili inshu ya toka mwezi wa tano, ni vizuri ukafika katika matawi yao.
Wengine tunaishia kulalamika tu...

Good point. Hata yeye mwenyewe angekuwa nayo angeweza kuwabana juu ya huo muamala
 
Mleta mada...kama sijakosea kiwango kikubwa cha kutoa ni laki nne...kwa kila muamala.
Laki sita sijaelewa imekaa vipi mpaka upate hiyo meseji.
Pili inshu ya toka mwezi wa tano, ni vizuri ukafika katika matawi yao.
Wengine tunaishia kulalamika tu...

ATM za NBC unatoa mpaka laki 7 kwa mkwapuo. Kakaribu .soma hadithi vizuri
 
posta haipo sehemu nyingi mkuu...
ila kuhusu NMB kuwa seriaz

hahahahaa! NMB tatzo lake ni mwisho wa mwez tu hapo ndio kunakuwa na folen sana lakn sku za kawaida utawapenda. Posta ipo hadi vijijin na haina folen mule utawakuta wastaafu tu na wanajeshi wakiomba mikopo
 
Watu wengi walikimbilia CRDB kwa wingi sana wakijua ipo vzr na baada ya crdb kuchukua tenda ya kuwaingizia watumishi wa umma mishahara wamekuwa na huduma za hovyo sana.
 
Back
Top Bottom