CRDB Is this stupidity or lack of caring?

Harafu ukienda na ATM card ya CRDB kwenye ATM ya NBC hairudi tena. NBC hawatakupa. Inabidi urudi tawi lako la CRDB wakupe card mpya ambayo ukiwa na bahati inachukua week mbili

Inaelekea kuna makubaliano bank hizi mbili kutoruhusu kadi ya mwenzake kwenye ATM zake. Watuweke wazi tusihangaike kupata kadi mpya kila wakati.

Angalau kwa NBC replacement ya kadi haichukui zaidi ya nusu saa.

Sasa tufike mahali kama wenzetu huko mbeleni ATM wala hazina nembo ya bank yoyote. Kila mtu anatumia bila kujali bank yake
This is bull shit men...inabidi tufike pahala hata ATM card tusitumie....unaingiza tu namba za siri.....
 
Haya ndiyo yaliyonikuta kutoka CRDB bank, wasichukie ila wajaribu kuelewa kuwa tukiandika na kuanika mabaya tunayoyapata kutoka kwa Service Desk, Customer Care teams, Customer Service Reps ndio itakayopelekea wao kujirekebisha na kutoa huduma bora hapo baadae.

Matatizo kama haya huwa tunayapata kutoka yale makampuni yenye wateja wengi kuliko yale yenye wateja wachache.

Nimekuwa na tatizo na visa card yangu ya bank kwa mda mrefu, nilikuwa nashindwa kufanya manunuzi online, nashindwa ku-link card yangu na paypal na sio kama mimi ni mgeni katika hili. hivyo usije niambia process za kulink ni hizi na hizi.

Ok nielezee tu baada ya kushindwa kuitumia card yangu online nikapiga simu kwenye number ambazo zipo kwenye card yangu ( contact customer care ) kuelezea tatizo langu nilijaribu kujielezea kwa umakini sana kuhusu tatizo langu na yeye akanijibu kuwa anachukua maelezo yangu na anayafikisha kwa idara inayohusika na nitajulishwa kwa njia ya sms punde tatizo langu litakapotatuliwa.

Nikamwambia kama anaweza akanipa namba ya hiyo idara ili niwaelezee hili tatito, akanijibu kwa ufupi tu hapana na akakata simu.


Nikapiga tena ikapolelewa na supervisor mwingine, ambae aliweza kutatua tatizo langu ndani ya dakika 3 tu, aliniambia subiri usikate simu na akaniweka on hold kidogo nafkiri labda alikuwa anawasiliana na hiyo idara, alirudi online na kuchukua maelezo ya ziada na akaniambia account yangu haina hela hivyo niongeze halafu nijaribu kufanya manunuzi tena online pamoja na ku link card yangu na paypal.

Baada ya kuweka kiasi fulani cha hela mambo yakawa sawa na nililipia service ya dola xx na ikakubali na hapohapo nikapata sms ya muamala nilioufanya kutoka crdb bank.

Nikajaribu ku link card yangu na paypal nayo ikakubali. Baada ya siku nikapata tena muamala kutoka crdb ukionyesha kuwa nimefanya muamala na kama sitambui huo muamala nipige simu ili nieleweshwe, nikapiga simu na wakanieleza kuwa ule muamala nilioufanya ndio umekamilishwa leo na wamenitumia hiyo sms kunijulisha na huo ndo mchanganuo katika Tsh, nikawaambia ok ila mbona muamala umekuja kwa mfumo wa USD na sio Tsh? wakasema hiyo ni Tsh na sio USD.

Basi nikawaelewa na kuwashukuru wakaniuliza kama nina swali lingine nikawaambia sina, Cha kushangaza nilipotaka kufanya manunuzi mengine tena card yangu ikakataliwa kama ilivyokuwa awali, japo kulikuwa na balance kubwa tu ila ilikuwa inakataliwa, nikaongeza hela, hali ikawa hivyo hivyo.

Safari hii nikaamua kwenda moja kwa moja kwenye tawi langu na kuijaribu card yangu kwenye ATM, napo ikagoma ikaleta ujumbe unaosomeka "sorry this transaction has declined", nikaingia ndani kwenye desk customer service, wakasema nijaze form halafu nilipie sh 5,900/= ili wa-reset password yangu, nikaambiwa baada ya hapo kilakitu kitakuwa sawa.

Baada ya kufanya hayo yote nikaambiwa nitapata sms kwenye simu halafu niingie kwenye ATM niweke password mpya nitakayotumiwa, sikupata sms wala nini na muda ukawa unazidi kwenda almost 2hrs, wakasema nijaribu hivyohivyo kwenye ATM na nikiulizwa password niweke 1234, nikafanya hivyo lakini bado nikawa napata ujumbe "sorry this transaction has declined".

Nikarudi tena ndani na yule alienihudumia mara ya kwanza akawa anamuhudumia mteja mwingine aliekuwa pembeni yake akaniuliza nikamwambia ujumbe ninaoupata kwenye ATM.

Akachukua card yangu na kuikagua kwenye computer yake na kunieleza kuwa card yangu imefungiwa hivyo lazima nijaze form ili waweze kuifungua,
nilifanya kama alivyonielekeza na akaniambia nimwone meneja ili aweze kuidhinisha, muda ukazidi kwenda na baada ya lisaa wakasema niende nirudi tena baada ya siku tatu.

Nilivyorudi tena baada ya siku tatu sikumkuta tena yuke meneja nikamkuta meneja mwingine, nikaanza kumwelewesha pale tulipoishia kabla ya yeye. achachukua card yangu na kuikagua tena kwenye pc yake, akasema card yangu imefungiwa walihisi ilitumika online pasipo idhini yangu tarehe zile ambazo mimi nilifanya muamala.

Nikamwambia ni mimi nilifanya huo muamala na kwanini waliifunga wakati sikulalamila?

Kwa ushauri wake akasema nijaze form ili waweze kuifungua na wakachukua namba yangu ya simu ili wanijulishe. Nikawauliza labda itachukua muda gani ili niweze kujua na nikiona siku zimepita niweze kuja tena, akaniambia we nenda tu tutakujulisha.

Cha kunishangaza wiki mbili zimepita bila kupata sms kutoka kwao, nikaamua kwenda tena kwenye tawi langu na nikamkuta yule meneja wa mwanzo kabla ya huyu alieniambia nisubiri sms kutoka crdb. Nikamkumbusha pale tulipoishia. Akasema nijaze form ili nipate card mpya, safari hii nikawa mkali nikamwambia wiki mbili zilizopita nilikuja nikakukosa ila nilimkuta meneja mwingine nae akasema nijaze form nikajaza nikaambiwa nisubiri nitatumiwa sms kutoka crdb, lakini ni wiki mbili sasa sijapata sms kutoka crdb ndo nimeamua kuja tena wewe unaniambia nijaze tena form nipate card mpya mbona kila nikija mnasema nijaze tu form hii ni safari ya tatu najaza form, na nikijaza kwaajili ya card mpya nayo nitaambiwa nisubiri tena wiki mbili, mbona siwaelewi?

Nikawauliza hivi ningekuwa na mamilioni kama Reginald Mengi ningekuwa nasumbuliwa hivi?

Nikawaambia Rais anaposema watu hawafanyi kazi hajakosea, mshahara wako unatoka kwa wateja kama sisi, sasa mimi nikifunga account yangu na mwingine kwa maudhi kama haya akafunga, huoni kuwa mtapoteza wateja na hivyo kupelekea kwenu kutoona hela? Halafu mtasema Magufuli kabana sana hakuna hela, kumbe ni ninyi hamtaki kufanya kazi.

Basi kwa maneno hayo akainua simu yake ya mezani na kuongea na idara inayohusiana na matatizo yangu na kisha kuniambia nisubiri kidogo. Kwa kuwa leo ilikuwa siku ya jmosi nikaona niwape muda, nikawaambia sina muda wa kusubiri naenda nitarudi jtatu na kama hawatakuwa na muafaka na card yangu basi nachukua fedha zangu zote nafunga account, nikaondoka.
Pole sana mkuu, lakini inaelekea CRDB hawana umakini.
Mimi nina huduma kama hiyo Exim Bank, hamna tatizo.
 
Daah yaani CRDB ni bureee kabisa aisee ni wa kuachana nao tuu, Mimi nlitoa hela kutoka kwenye M pesa katika ATM ya CRDB pesa hazikutoka kwenye mashine huku mpesa wakituma sms kuwa hela imeenda CRDB, sasa kuwasiliana nao wakajibu ndani ya saa 72 pesa itarudi ila sasa ni mwezi na hela hazijarudi na kila ukiwasiliana na customer care kupitia call center ni viswahili kila leo, mara tatizo lako litashughulikiwa ndani ya siku 10, mara mwengine tatizo lako halijaripotiwa mara mwengine tutakupigia simu kabla ya saa kumi, wengine kampuni inayohusika na kurudisha izo hela ipo kenya so mpaka waconfirm, yaan hawajielewi na hawajui nn wanafanya... kama mimi ndo ningekua na hela zao nawazungusha mwezi mzima wangenielewa? CRDB waache kufanya kazi kwa mazoea izo ni pesa za watu na mpaka mtu anafuata huduma kwao ujue anadharula
 
Pole sana, hao ni kama tigo, customer service ni zero, tigo niliwahama nikatumia halotel, CRDB nikahama nipo exim now, makato makubwa kidogo kuliko CRDB lakini huduma afadhali.... Funzo:Tusiwe wagumu kubadilisha brand kwa faida yetu.
 
Nimekuwa na tatizo kama hilo hilo na niliteseka sana, shida ni kwamba CRDB hawaweki watu sahihi mahali sahihi, hao wote waliokuwa wanakujibu hao wenyewe hawajui, so ni changamoto kwa kweli, hizo mambo kuna watu wachache sana kwenye main branch yao dar ambao wanakushugulikia mara moja, ila mpaka uwapate ni balaa!

USHAURI KWA CUSTOMER CARE WA BANK ZOTE, KAMA HUJUI KITU MWAMBIE MTEJA NA UMUELEKEZE KWA MTU SAHIHI NA SIO KUMPA MOYO.
Huu uozo sio CRDB tu, mimi nimekutana nao TRA Mwenge. Nimeenda kuulizia taratibu za kufanya De registration ya chombo cha moto. Mama niliyemkuta Inquiry Desk akaniuliza kwa kustaajabu...'de registration?, ndio nini sasa?' in such a way watu wawili wakaniuliza kwa pamoja 'au umekosea kutamka kaka?' Aliponishangaza, alinipuuza na kuendelea na watu wengine. Nikamsisitiza huo utaratibu upo na hata kwenye tovuti yenu upo ila page ni nzito sana haifunguki, hapo ndio akaniambia basi nenda dirisha la magari ukaulize huko
 
Imenipa hasira..manake si CDRB tu,kila pahala pana aina ya huo usumbufu,
 
Nimekuwa na tatizo kama hilo hilo na niliteseka sana, shida ni kwamba CRDB hawaweki watu sahihi mahali sahihi, hao wote waliokuwa wanakujibu hao wenyewe hawajui, so ni changamoto kwa kweli, hizo mambo kuna watu wachache sana kwenye main branch yao dar ambao wanakushugulikia mara moja, ila mpaka uwapate ni balaa!

USHAURI KWA CUSTOMER CARE WA BANK ZOTE, KAMA HUJUI KITU MWAMBIE MTEJA NA UMUELEKEZE KWA MTU SAHIHI NA SIO KUMPA MOYO.
Unprofessional workers is the big challenge to our giant bank here in Tanzania.
 
Mimi mwenyewe nina tatizo kama hili,nimeshajaza fomu zaidi ya mara tano kwa kupewa ahadi nitapata ujumbe kwenye simu lakini halitokei,mara ya mwisho niliambiwa anayeshughulikia kaenda kula,nilikaa masaa mawili hakutokea nikaamua kuondoka baada ya kuahidiwa nitapata ujumbe kwenye simu,crdb ina ubunifu ila hakuna watendaji!customer care ni mbovu kuliko maelezo!niliacha kutumia huduma yao kwa muda baada ya kupata ujumbe kwenye simu kuwa nimetoa hela kwenye akaunti wakati sikufanya hivyo na kadi nilikuwa nayo,niliwapigia customer care wakanijibu labda nimempa mtu kadi au mke wangu kaniibia#?&€pumbaf zao,nilimuuliza ni atm gani inatoa chenji yenye point(556,420.16) akanijibu nicheki vizuri lazima itakuwa imetolewa na mtu wangu wa karibu
Kwa haya majibu uliyoyapata kiongozi pole sana.
Inatia hasira mi nimekusoma tu nimekasirika je wewe ilikuaje!?
 
Pole sana mkuu.

Mimi ni mteja wa CRDB wa muda mrefu.

Ni kweli inabidi wajiimarishe. Kuna vijana wadogo wadogo wameajiriwa, nafikiri wanafanya business as usual.

Zamani nikitoa hela ATM nilikuwa napokea sms kuonyesha muamala uliofanyika. Ila kwa sasa wamesitisha.

Nilienda bank husika kuulizia, wakaniambia ni kweli wamesitisha ila wameanza kurejesha kwa baadhi ya watu.

Nikamwambia nahitaji hiyo huduma ili hata kama kadi ikiibiwa, ni rahisi kujua kinachoendelea.

Jibu nililopewa ni kwamba nisubirie wakati wangu.

KUMBUKUMBU.

Nakumbuka kipindi cha nyuma nilikuwa na account St****c. Nikawa nimejiunga kwamba hela ikitolewa kwenye ATM napata notification.

Baadaye nikawa sipati hiyo huduma. Nikaenda kama mara kumi kuulizia mbona sipati notification, wakawa wanapromise nitaanza kupata.

Mwishowe nikakata tamaa. Siku moja nikaenda kuchukua bank statement ili kufanya reconcilliation. Ahhh nikakuta madudu madudu.

Kumbe wale vijana walikuwa wanachomoa hela kidogo kidogo, kiasi kwamba hata kutambua ni vigumu, lakini mwisho wa siku wakitoa kwenye account kama mia au hamsini, basi wana hela ndefu.

Ilibidi kusitisha account yangu pale

He, yaani nimetokewa na exactly scenario kama yako na wamenijibu hivyo hivyo. Kwa hiyo ndivyo wanavyokula? Wanaiba hela yetu kidogo kidogo na kusitisha kutuma taarifa drawing inapofanyika! Mbona at time 'T' watakamatwa tu? Labda washirikiane na audit team.
Kaaazi kweli kweli, ukienda ku draw hela yako wawatonye majambazi, hela yetu wadokoe mh
 
Tatizo wanapeana ajira kwa kujuana bila kujali professional ya mtu ndo chanzo chanzo cha hayo yote
 
Sasa ulilipwa mkuu?
Ofcourse, walitaka kunipiga dana dana za sijui eti network ya kuangalia statement hakuna, ooh sijui andika barua, ooh sijui kamuone manager, ooh sijui manager hayupo.., ghafla wakashangaa macho yangu yanaanza kuwa mekundu, ghafla nikaanza kuwa mwekundu mwili mzima na kuhema kwa spidi sana.., niliwaka kidogo nimchomoe yule jamaa wamapokezi nimtoe nje tukaongee vizuri, bila kuwafanyia fujo watakuzungusha hadi basi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom