CRDB bank mbona mnatuibia sana wateja wenu?

CRDB bank mbona mnatuibia sana wateja wenu?

Taarifa zipi mkuu sidaiwi mkopo wowote na sikusoma kwa mkopo. Na kama ningekuwa nadaiwa ningeona kwenye bank statement?? Nami nimeshangaa huu mwezi japo sinaga kawaida ya kuangalia bank statement ya akaunti yangu, sasa jana nikataka kutoa M kadhaa nichukue kiwanja baada ya kutoa nikaomba risiti walai nilitaka kuzimia maana sio makato yale.

Na jumatatu nawaendea ofisini siwezi kuibiwa kiurahisi hivyo yaani. Na kama shida kuziona hela kwenye akaunti bora nihame bank au nihamishe namna ya kuhifadhi fedha zangu kwa kufungua NMB saving akaunti.

Nimecho kwa wizi huo na huenda nilikuwa naibiwa toka siku nyingi ila sikuwa na mazoea kuangalia au kuomba bank statement. Kuanzia sasa fedha zangu kwenye simu nitahamishia au kufungua akaunti bank nyingine.
Pole Mkuu,ila kwenye simu ni hatari zaidi
 
CRDB walishawajulia wabongo, wengi wanapenda jina na si huduma, ukimwambia mtu nina ac TPB anakushanga na kukuita mshamba, ukimwambia nina ac NMB/NBC wanakuita mkulima, eti CRDB ndio bank ya kijanja
Acha waendelee kuwaonyesha ujanja sasa
 
Tetesi zinasema jamaa mwanayumba sana kwa sasa,hali ni tetenangai sana,mikopo tu ya top up kutoa kwa watumishi hadi wiki 3,4

Ila mkuu fuatilia vizuri mi mwenyewe natumia hiyo benk sijawahi kukutana na makato ya hivyo mwaka wa 20 huu,kuna kitu hakipo sawa
 
Back
Top Bottom