Covid-19 inawatesa hawa kiuchumi

Covid-19 inawatesa hawa kiuchumi

Kichumini

Member
Joined
Jun 7, 2016
Posts
90
Reaction score
106
Habari za jioni wandugu,

Wakati serikali ikiendelea kujitafakari hatua za kuchukua juu ya Corona, tayari kuna baadhi ya sehemu zimesha athiriwa moja kwa moja. Zifutazo ni baadhi ya sekta zinazolia na kuumizwa na huyu mgeni Covid-19.

1. SEKTA YA ELIMU
Wafanyakazi katika hii sekta, especially kwenye sekta binafsi tayari ni kilio. Kuna baadhi ya shule binafsi bila hata kujali mikataba ya wafanyakazi wao mwezi wa tatu hawakulipwa mshahara kabisa. Na hata baadhi waliolipa walilipa pungufu ya mshahara halisi. KILIO TAYARI HUMO .

2. SEKTA YA USAFIRISHAJI
Baada ya serikali kutangaza "level seat" kilio kimetanda katika sekta hii, baadhi ya wamiliki wa vyombo vya usafiri wa uma wameamua ku park vyombo vyao kutokana na mapato kiduchu. Hapa tayari tunaona ukosefu wa ajira kwa vijana wengi ambao walitegemea hii sekta kama chanzo cha ujira. MAJANGA

3. SEKTA YA UTALII
Huku bado tukijadili report ya CAG juu 2.5Bn bado kwenye sekta hiyo kuna kilio. Wadau wote i mean wote wa sekta ya utalii wamelizwa na Covid-19. Tulimsikia Manager wa TRA Kilimanjaro akisema wafanyabiashara zaido ya 600 wamepeleka maombi ya kufunga biashara na wengi ni wadau katika sekta ya utalii. Taifa lime na linaenda kupoteza mapato zaidi kama hali haitatengamaa. Ajira nyingi sana zinapotea na watu ni kilio tu. KIRUUU

4. SEKTA YA BURUDANI
Huku nako tayari ni kilio, Diamond tunajua alikatisha Europe tour yake coz ya Covid-19. Sekta hii imeajiri watu wengi sana, kwa sasa watategemea mauzo ya kazi kwa mtandao kupata hela. Lakini tunajua chanzo chao kikuu cha mapato ni shows. Covid-19 imezuia shows zote kufanyika na hii imeacha kilio kikubwa ndani ya sekta hii. KILIO

5.

Leteni nyingine ....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wazee wa mikeka tumepigika sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Majogoo wa anfield wamefanya kazi kubwa sana kuhakikisha wanautwaa ubingwa wa Epl.maskini kazi yao mbele ya covid 19,imekuwa Kama kuteka maji na kutaka kuijaza bahari.usishangae wazungu walivyochanganywa na hiii Corona wakatangaza aston Villa ya samata ndio mabingwa wapya wa kuteuliwa wa England.maana Mambo yakigeuka wa mwisho uwa wa KWANZA na Liverpool akawa Hana lake
 
Hayana kazi
IMG-20200402-WA0007.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
5. Michezo. Ligi nyingi zote zimeahirishwa, i feel sorry for Lebron and his Lakers, jamaa alikua ananusa MVP
 
kuna wanasayansi wengi wanasema hakuna Mungu ngoja Mungu anawaangalia wanavyotapatapa na corona ....
 
ndio maana halisi ya neno JANGA.

kila mmoja ataguswa either kwa ugonjwa wenyewe au madhara yake atayaonja.

mimi nilianza kuhisi maumivu baada ya kukuta hamna mechi ya kubeti jmosi moja.aisee niliichukia corona kwa mara ya kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viwanda vingi duniani vimefungwa,uchafuzi Wa hali ya hewa umepungua,watu tumejifunza ustarabu wa uwa wasafi maana kila kona tunanawa,so tumezuia magonjwa mengi sana ya kuambukiza,kuna baadhi ya bidhaa zimeuziga na hatukuzani hata siku moja kama zitakuwa na market hivi,tumejifunza ustarabu wa kukaa level seat(usicheze na nature ikiamua lake linakuwa) Zipo nyingi faida na hasara,ila msisahau kunawa mikono,na kama huna shuhuri ya kufanya tulia home, wafundishe wanao hesabu,maana katika maisha yako yote hukuwahi hata siku moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila Tanzania tunaelekea kuitokomeza, hivi karibuni maisha yatarudi kama kawaida
 
Back
Top Bottom