COSAFA Cup, leo 18 Mei 2015: Tanzania vs Swaziland

COSAFA Cup, leo 18 Mei 2015: Tanzania vs Swaziland

mkolaj

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2014
Posts
3,023
Reaction score
1,092
Hukumu ya Mart Nooij na Taifa Stars kuanza leo;

Timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars" leo usiku itatupa karata yake ya kwanza dhidi ya Swaziland katika michezo ya mashindano ya COSAFA.

Taifa Stars inashiriki michuano hio kama timu mwalikwa ikiwa imepangwa kundi B pamoja na timu za mataifa ya Lesotho, Swaziland na Madagascar.

Stars inahitaji ushindi katika mechi ya leo ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kuibuka kinara wa kundi B na kupata tiketi ya kucheza robo fainali dhidi ya Ghana.

Mechi ya mwisho baina ya Taifa Stars na Swaziland ilimalizika kwa suluhu ya mabao 1-1. Bao la Taifa Stars lilifungwa na Thomas Ulimwengu ambae leo hatakuwepo katika mchezo huo.

Pambano la leo litachezwa kwenye uwanja wa Royal Bafokeng, likitarajiwa kuanza saa 2:30 kwa saa za Afrika Mashariki.

Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.

Kila la kheir Taifa Stars.

===================
===================


Matokeo ya Mwisho: Swaziland 1 - 0 Tanzania
 
Hiyo mechi ya mwisho kati ya hizi timu mbili ilikuwa ya kirafiki au ya madhindano?Kama ni mashindano ni yapi na mechi ilichezewa wapi.

Kwenye ranks za fifa nchi hizi zipo nafasi gani

Kwrnye vikosi vya timu zote mbili juna wachezaji wa kulipwa nje ya nchi zao?Kama wapo ni akina nani na wanacheza wapi.

Jazia nyama hizo mada yako.
 
Mtupe updates mtakaokuwa mnatazama huu mtanange laivu.
 
kuna channel ya kibongo itarusha mechi hii? Stars naipenda sana shida tuu inataka kunifanya Kama arsenal.
 
Tuko Pamoja wakuu leo tunaweka pembeni utani wetu
 
Hivi taifa stars ndo jkt ruvu.?samahani lakin.!!
 
Back
Top Bottom