Corona: Wazee na wenye magonjwa mengine tupaze sauti

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,854
35,862
Mabibi na mabwana hali inaendelea kuwa si hali. Sisi tulio hatarini sauti zetu lazima zisikike. Kwa mwelekeo uliopo ndiyo tumeshatolewa kafara hivyo.

Jana tumemzika kigogo wa BOT (Joachim Sayi Nsunga) RIP, huko Dutwa Bariadi, Simiyu. Huyu bwana alikuwa mhasibu mkuu BOT makao makuu, Dodoma.

Amefariki juzi pale Benjamin Mkapa. Hakuwa mtu mdogo kwani angalau aliweza kutumia ventilator.

Pana mwelekeo kabambe wa kudhibiti taarifa za vifo. Kuzifanya taarifa za vifo vya vigogo kuwa ni nyara za serikali.

Wazee na wenye magonjwa mengine, sisi pia kama walipa kodi ni muhimu sana tukapaza sauti zetu vilivyo. Hatustahili kutelekezewa janga. Tunayo haki ya kuishi kama ilivyo kwa watu wengine.

Sisi tunalipa kodi na wengine wetu tumelipa sana kodi labda kuliko hata hawa ambao leo wanawashwa sana na pilipili wasizo zila kutusemea sisi.

Propaganda za vijiweni kuwa ugonjwa huu hauuwi ila hofu. Ugonjwa huu tiba yake ni mazoezi. Ugonjwa huu tiba yake ni lishe, malimao na tangawizi. Ugonjwa huu tiba yake ni nyungu n.k.

Yote hayo tokea vijiweni hayatusaidii sisi tulio wahanga zaidi.

Wito kwa serikali:

"Sisi tulio wahanga wa kesho wa ugonjwa huu tunaidai haki yetu ya kuishi. Tunawaona wenzetu wanavyopukutika. Kama mnatu 'kana' tukiwa hai, nasi tuta 'wakana' ninyi tukiwa hai."

Tafadhalini sana waachieni wataalamu wa afya kushika hatamu za uongozi wa vita dhidi ya ugonjwa huu. Kwanini ombi hili ni kubwa mno kwenu?

Hadi tufe wangapi?

Kwanini nyie msiokuwa katika hatari ya ugonjwa huu mmekuwa sana wa kutusemea, hali kufa twafa sisi?

Mara ooh mliona wapi mwana michezo kafa kwa Corona? Jibu ni kuwa hatujui. Kwani hazipo takwimu hizo kama ambavyo hatujui pia kama kuna machangudoa wowote wamekufa kwa Corona.

Hivyo pia hatuwezi kusema kuwa uchangudoa ni kinga ya Corona.

Hivi ni wapi palipo na wana michezo wazee au wenye magonjwa mengine? Mbona kuchezana shere hivi?

Hebu tusitoane kafara mchana kweupe namna hii.

Ninawasilisha.
 
Hiyo sauti unaipaazia wapi, mbona siisikii?

Kaulize Dutwa kwenye msiba wa kigogo huyu.

Uliza kote nakopita.

Nimepaza sauti dhidi ya gonjwa hili baya kuliko jina lako tangia day 1:


Ulipendelea nipazie wapi ili usikie wewe?
 
Iko hivi, hatari inakuwa kubwa zaidi unapokuwa mzee au mwenye magonjwa mengine inakuja pale unapojichanganya masokoni, magulioni, kwenye ma dala dala, ma ferry, nk

Serikali itafute njia nyingine ya kuwahakiki wazee wanaostahili kupata NSSF yao na pensheni nyingine badala ya kuwataka wafike in person kuhakikiwa; ama sivyo tutapoteza wengi wa Wazee hawa kwa kuambukizwa haya maradhi kwenye dala dala na mwendo kasi!!
 
Mabibi na mabwana hali inaendelea kuwa si hali. Sisi tulio hatarini sauti zetu lazima zisikike. Kwa mwelekeo uliopo ndiyo tumeshatolewa kafara hivyo.
Mkuu muda huu wa mapambano sio muda wa kulalamika bali ni muda wa angalau kuchukua hatua binafsi wewe na familia yako;

1- Nawa maji tiririka nyumbani kwako, nunua senitizer na tembea nayo kila uendapo na itumie pale utakapona kuna hatari ya kuambukizwa kupitia mikono.

2- Vaa barakoa katika mikusanyiko mikubwa kwani social distancing leo hakuna Mtz anayeitambua.

3- Kifungua kinywa kiwe Tangawizi nk, pia jaribu ku apply karafuu au Vicks (Camphor) mapuani angalau kudhibiti kama kutakuwepo na maambukizi.

4- Unapohisi dalili za mafua, kikohozi ikiambatana na homa, basi wahi kujifukiza maji ya Tangawizi yaliyochanganywa na vitunguu saumu, mchanganyiko huo usagwe kwa pamoja.

Mkuu, hii ni vita ya mtu mmoja mmoja japokuwa ni vita ngumu lakini Mungu atatia kudra yake kwa mtu anayejitahidi, ni bora kujitahidi kuliko kukaa tu kusubiri juhudi za serikali ya jiwe na kudra za Mungu.

Mungu atusaudie katika haya madhila. amin.
 
wewe baki nyumbani kwani unalazimishwa kutembea ukifa asala yako au ya jiwe mbona mnakua na akili ya nyumbu jiwe mnaona alisomeki afu mnaanza kulalamika .STAY HOME.
 
Angalau wangerejesha ile AMRI ya MA-CONDER kuwa kuvaa barakoa ni lazima ukiwa in public.

Unakuta kwenye mikusanyiko, daladala, nk hakuna aliyevaa barakoa sabb watu wamedanganywa wakaamini kuwa ugonjwa haupo!
Vaa barakoa wewe mwenyewe, hakuna mtu aliyekatazwa kuvaa.

Juu ya yote ukishikwa na hiyo Corona ni wewe pekee na nduguzo ndio mtahangaika.

Vaa barakoa katika mkusanyiko na tembea na sanitizer ya kujipaka mikononi.
 
Mkuu muda huu wa mapambano sio muda wa kulalamika bali ni muda wa angalau kuchukua hatua binafsi wewe na familia yako
Kwani kasema yeye binafsi hajilindi!? Tunataka kuona serikal inawajibika kwa upande wake lkn sio kupiga propaganda majukwaani. Serikal za nchi zingine zinaagiza chanjo kwa sasa, swala la kujua chanjo ni salama au la ni la serikal yenyewe.

Kama inashindwa kutambua chanjo ni salama basi haina uhalali wa kuendelea kuwepo madarakani. Au tuamini yale wasemayo baadhi kuwa serikali haitaki kutoa pesa?
 
Vaa barakoa wewe mwenyewe, hakuna mtu aliyekatazwa kuvaa.

Juu ya yote ukishikwa na hiyo Corona ni wewe pekee na nduguzo ndio mtahangaika.

Vaa barakoa katika mkusanyiko na tembea na sanitizer ya kujipaka mikononi.
Hawezi kuvaa Barakoa au kuosha mikoni eti mpaka aambiwe na Serekali! Kuna Watu Wana akili Kama za ngombe,hawezi kwenda zizini kwake hata Kama kiza kimeingi hadi achapwe mijeledi ndiyo anaongoza njia! Wanashindwa akili hata na Kuku wa kiyenyeji,akisha ona jua linaanza kuzama nae huyo hurudi zake bandani kwake hadi kesho yake alfajiri ndiyo anatoka tena.
 
Mkuu muda huu wa mapambano sio muda wa kulalamika bali ni muda wa angalau kuchukua hatua binafsi wewe na familia yako;

1---- Nawa maji tiririka nyumbani kwako, nunua senitizer na tembea nayo kila uendapo na itumie pale utakapona kuna hatari ya kuambukizwa kupitia mikono....

Mkuu hayupo mwenye uelewa aliye kaa kusubiri juhudi za serikali ya jiwe na kudra za mwenyezi Mungu pekee. Hivi sisi ambao haya ya mikusanyiko pia yanatuhusu:

IMG_20210214_214251_251.jpg


Nayo tunaiepuka je ndani ya mazingira magumu ambayo serikali inatuwekea?
 
Covid haikupiga kura wala haitishiki na raisi sijui serikali. Hivi ni vita vya raia mmoja mmoja. Jilinde, chukua hatua. Usisuburi serikali ambayo inaishi mazingira tofauti kabisa na wewe raia wa kawaida. By the way, inawezekana viongozi wanachukua tahadhari zote kujikinga.
 
Pole Sana Mzee.

Ni kwamba Corona sasa hivi sio ugonjwa wa mlipuko tena.

Maana sifa moja wapo ya ugonjwa wa mlipuko ni kuja na kupotea.kama kipindu pindu na ebola.

Hii Ngoma imeshakuwa ni MKAZI WA KUDUMU..

Anza kufanya mema.maana haitakuacha
 
Hizo barakoa huko zinapotengenezwa.
Huu ugonjwa unawatesa vibaya mnoo.
Na barakoa wanatengeneza wenyewe
Angalau wangerejesha ile AMRI ya MA-CONDER kuwa kuvaa barakoa ni lazima ukiwa in public.

Unakuta kwenye mikusanyiko, daladala, nk hakuna aliyevaa barakoa sabb watu wamedanganywa wakaamini kuwa ugonjwa haupo!!!
 
Hizo barakoa huko zinapotengenezwa.
Huu ugonjwa unawatesa vibaya mnoo.
Na barakoa wanatengeneza wenyewe
Kwa hiyo unafikiri kila fundi selemara ana kitanda na kiti kizuri ndani?

Vipimo vyetu vya utetezi vingine hata havieleweki.

Haya mambo kabla hayajakukuta, utakua shujaa sana. Yakikufika hapo ufahamu na tafakari chanya hurejea. But too late.

Ukifika wakati utaitafuta hewa ya kutosha, unafika hospitali unaambiwa "saini hapa, hali yako ikibadilika zaidi hatuna cha kufanya. Machine zote za kusaidia kupumua zimejaa."
 
Hawezi kuvaa Barakoa au kuosha mikoni eti mpaka aambiwe na Serekali! Kuna Watu Wana akili Kama za ngombe,hawezi kwenda zizini kwake hata Kama kiza kimeingi hadi achapwe mijeledi ndiyo anaongoza njia! Wanashindwa akili hata na Kuku wa kiyenyeji,akisha ona jua linaanza kuzama nae huyo hurudi zake bandani kwake hadi kesho yake alfajiri ndiyo anatoka tena!!

Acha kujitia ujuaji wakati mwenye akili za ng'ombe ni wewe! Hivi katika mazingira haya ng'ombe wewe, walio hatarini wajiepushe vipi?

IMG_20210214_214251_251.jpg
IMG_20210214_214251_251.jpg


Mbona ng'ombe nyie mnajidhania mna akili mno kuliko hata binadamu wenye kujitambua?

Kama nyie hamko kwenye makundi haya hatarini kwanini mnataka kutusemea sisi?

Kwanini hamtaki kutuelewa?

Tunayo haki yetu ya kuishi ambayo tafadhalini hatuhitaji michango yenu hata ya mawazo kama nia yenu ni kuona tunaangamia tu.
 
Tatizo sio vipimo.
Bali hizo barakoa maana tangu mwaka Jana mwezi wa kwanza zimeanza kutumika dunia nzima.lakini bado watu wanaambukizwa.na namba zinaongezeka.umuhimu wa barakoa upo wapi?

Kwani vyandarua havitumiki na watu wanapata malaria? Kwa hiyo waache kutumia? Reasoning jamani kha!
 
Tatizo sio vipimo.
Bali hizo barakoa maana tangu mwaka Jana mwezi wa kwanza zimeanza kutumika dunia nzima.lakini bado watu wanaambukizwa.na namba zinaongezeka.umuhimu wa barakoa upo wapi?

Kwani watu hawatumii vyandarua na bado wanapata malaria?
Kwa hiyo waache kabisa?
Reasoning zetu, khaaa!!
 
Back
Top Bottom