TUPAMBANE SANA
Member
- Nov 21, 2018
- 29
- 26
Dunia kwa sasa imepigwa na bumbuazi kutokana na virus wanaoitwa Corona. Wapo wanaodai huenda vikawa ni mambo ya kuharibiana kibiashara kwa kuamini ya kwamba huenda ikawa Corona ilitengenezwa na Wamarekani ili kuchafua biashara ya China na wapo wanaoamini ya kwamba ni miongoni mwa mapigo ya Mungu tu kwa watu wake.
Twende kwenye pointi husika ya kafara la nchi. Siku chache zilizopita kumetokea na wenzetu waliopo China kuomba Serikali iwarudishe nyumbani.
Hali kadhalika kiuhalisia hata ndugu zao wanatamani kuona watoto wao wanarudi nyumbani na kwa sasa inavyosemekana China imefunga mipaka yake kwa maana hakuna watu kusafiri kwenda au kuingia kwa baadhi ya sehemu.
Sasa hao ndugu zetu watarudi vipi? Na je serikali itachukua hatua gani kwa hao watu kwa maana nchi kama China kushindwa kupambana na Corona mpaka kufikia watu zaidi ya 1000 kufa ni dhahiri shahiri ya kwamba ukifika Tanzania ni zaidi ya watu waliokufa china itatokea kutokana na miundombinu ya nchi yetu kuwa mibovu na undugu wa kushikana shikana. Yote hayo tumwombe Mungu aepushie mbali.
Kuhusu hao ndugu zetu watarudi? Je, tuna chombo cha kupima afya zao? Je, tuna chombo cha kufuatilia afya zao? Nionavyo mimi hawa watatolewa kafara la nchi kukomboa wengine dhidi ya Corona.
Kiukweli inauma na itaendelea kuuma kuona mwanao yuko anaomba msaada wa mzazi kumsaidia lakini anashindwa kutokana na taratibu za nchi.
Je, wandugu serikali ifanye nini juu ya hao wenzetu?
Twende kwenye pointi husika ya kafara la nchi. Siku chache zilizopita kumetokea na wenzetu waliopo China kuomba Serikali iwarudishe nyumbani.
Hali kadhalika kiuhalisia hata ndugu zao wanatamani kuona watoto wao wanarudi nyumbani na kwa sasa inavyosemekana China imefunga mipaka yake kwa maana hakuna watu kusafiri kwenda au kuingia kwa baadhi ya sehemu.
Sasa hao ndugu zetu watarudi vipi? Na je serikali itachukua hatua gani kwa hao watu kwa maana nchi kama China kushindwa kupambana na Corona mpaka kufikia watu zaidi ya 1000 kufa ni dhahiri shahiri ya kwamba ukifika Tanzania ni zaidi ya watu waliokufa china itatokea kutokana na miundombinu ya nchi yetu kuwa mibovu na undugu wa kushikana shikana. Yote hayo tumwombe Mungu aepushie mbali.
Kuhusu hao ndugu zetu watarudi? Je, tuna chombo cha kupima afya zao? Je, tuna chombo cha kufuatilia afya zao? Nionavyo mimi hawa watatolewa kafara la nchi kukomboa wengine dhidi ya Corona.
Kiukweli inauma na itaendelea kuuma kuona mwanao yuko anaomba msaada wa mzazi kumsaidia lakini anashindwa kutokana na taratibu za nchi.
Je, wandugu serikali ifanye nini juu ya hao wenzetu?