Corona imetuepusha na magonjwa ya mlipuko

Corona imetuepusha na magonjwa ya mlipuko

kyarluta

Member
Joined
Oct 28, 2019
Posts
24
Reaction score
12
Leo nimeongea na rafiki yangu ambaye ni daktari. Yuko wilaya ya Bukombe na anamiliki hospitali. Katika kipindi chote cha Corona, hospitali yake haijawahi kupokea mgonjwa mwenye viashiria vya korona. Kule kwa korona haipo.

Ametoa ushuhuda kwamba, utaratibu wa kunawa mikono Mara kwa mara, umepunguza magonjwa. Amenitajia magonjwa kama Kuhara, kipindupindu na magonjwa ya macho.

Anasema kuwa hata mapato yake yamepungua kutokana na wagonjwa wa aina hiyo kupungua.

Huu ni ushindi mkubwa kwa walio wengi. Kinachotakiwa ni kutolegeza juhudi hii ya usafi wa mikono wa mara kwa mara. Hakuna asiyejua kwamba gharama za matibabu ziko juu. Magonjwa yanapunguza uchumi wa familia. Tukishinda magonjwa haya itabakia issue moja ambayo haiepukiki nayo ni kuhudumia wajawazito.
 
Kuna siku nilikuwa namwambia mtu huu utaratibu utapunguza magonjwa yanayotokana na uchafu hasa kuhara,matumbo na kipindupindu. Ni vema madaktari wakaja na matokeo rasmi ili huu utaratibu uendelee moja kwa moja km itathibitika.
 
Pamoja na hayo pia corona imesaidia watu sasa wanakula vizuri (chakula bora) mboga za majani na matunda pia wanakunywa juice hivyo kinga za mwili zimeimarika maradufu
 
Back
Top Bottom