Corona: Hongereni UDSM mmefanya lilo bora

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,948
35,948
Mabibi na mabwana kwa hakika hekima ni uhuru.

Bila ya kupepesa macho, inataarifiwa kuwa pale UDSM wamechukua hatua hii ya msingi sana:

IMG_20210206_044851_342.jpg


Japo pale #5 mwishoni mwishoni pana ka ukakasi, ni hatua kama hizi tunazoihitaji pia serikali kuzichukua. Hasa hasa kudhibiti mikusanyiko ya watu na kuwahami wale walio kwenye hatari zaidi.

Hayo yapo mikononi mwa serikali na mwenye dhamana nayo ni wao.

UDSM wameonyesha njia. Wenye macho hawaambiwi tazama.

Serikali nanyi fanyeni kama hayo muone kama hatutawapongeza kwa bashasha. Zaidi sana kabidhini jukumu la vita hivi dhidi ya ugonjwa huu kwa wataalamu wetu wa afya. Kwa hakika watatuvusha.

Ni hatua njema kukiainisha ki usahihi chuo hiki kutoka katika dhana ya jalala inayoendelea kumea kwa kutokukemea yaliyo ndivyo sivyo.

Hilo likikihusu chuo hiki kikongwe moja kwa moja na ma alumni wake wote popote kule waliko.

Nani ajuaye kama uthubutu wa wana Dar es salaama kwenye kujitambua una mchango gani kwenye hili?


Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. La UDSM tumelisikia, tunawasubiria na wengine wote wenye kufanana nao. Hasa hasa tunaisubiria serikali kufanya sehemu yake.

Kila dakika inayopita bila ya kuchukua hatua ni dakika iliyopotea kwenye jitihada za kuokoa maisha.

Ninawasilisha.
 
Kwahiyo UDSM wameamua kupingana na wizara ya afya? Naibu waziri kasema hakuna Corona Tanzania.

Naona sasa inaibuka vita ya wanasiasa na wataalam.

Sisi raia wema na wapenzi wasikilizaji tunaendelea kuufanyia kazi ushauri wa Rais Mstaafu JK..."Akili za kuambiwa, changanya na zako"
 
Nilipoona kichwa cha habari nilitabasamu na kshusha pumzi nikitegemea kuwa wamekuja na suluhisho! Hakuna jipya. Nilidhani wamegundua dawa/tiba au chanjo kumbe ni yale yale.cHakuna jipya.

Mkuu process ya kugundua dawa au chanjo si mchezo:


Beberu mwenyewe kama unavyomwona na umahiri wake angali anacheza makida makida.

Avumbue nani dawa, UDSM? Thubutu!

Bupeji au Covido eti dawa? Bandugu tutofautishe baina ya dawa na juice za Jambo - JAMUKAYA tokea kanda pendwa.

Dawa au chanjo haviji kwa kuoteshwa!
 
Mkuu heri ya nusu shari kuliko ya shari kamili.

Tukishindwa kupongeza kwa machache hata mengi hatutaweza. Tushukuru hata kwa machache tunapoendelea kuchagiza kwa mengine zaidi.
This is an academic Institution, tena a renowned higher learning Institution, wanapofanya ujinga, let us not spare them!
 
Kwahiyo UDSM wameamua kupingana na wizara ya afya? Naibu waziri kasema hakuna Corona Tanzania...

Naona sasa inaibuka vita ya wanasiasa na wataalam....

Sisi raia wema na wapenzi wasikilizaji tunaendelea kuufanyia kazi ushauri wa Rais Mstaafu JK..."Akili za kuambiwa, changanya na zako"
Hivi mnaotaka Serikali iseme kuna CORONA mnaotaka iweje?baadhi wanataka Serikali ikiri na kuchukua hatua kali km lockdown na tuletewe misaada/kukopeshwa chanjo.Hatua ya Serikali kutokukir ni bora zaid.KAMA mtu anataka Karantin ajiweke mwenyewe.
 
Ningewapongeza zaidi kama wangefunga chuo kwa mda mpaka pale itakapojiridhisha kuwa tuko salama kama nchi vinginevyo bado siwaelewi kama taasisi kuu ya wasomi kutoa vipeperushi vya kiwoga woga kama hichi.
 
Nilipoona kichwa cha habari nilitabasamu na kshusha pumzi nikitegemea kuwa wamekuja na suluhisho! Hakuna jipya. Nilidhani wamegundua dawa/tiba au chanjo kumbe ni yale yale.cHakuna jipya.
Neno jema haliwezi toka Nazareth
 
Maeneo yenye mikusanyiko mikubwa kama vyuoni ni lazima watoe tahadhari kama hizi, nategemea na vyuo vingine navyo vitachukua hatua, Corona ipo tusidanganyane.
 
Kwahiyo UDSM wameamua kupingana na wizara ya afya? Naibu waziri kasema hakuna Corona Tanzania.

Naona sasa inaibuka vita ya wanasiasa na wataalam.

Sisi raia wema na wapenzi wasikilizaji tunaendelea kuufanyia kazi ushauri wa Rais Mstaafu JK..."Akili za kuambiwa, changanya na zako"
Ni wapi UDSM wamepingana na Wizara ya Afya kwamba Corona ipo? Hata hivyo katika bandiko hili sijaona kipya.
 
Ningewapongeza zaidi kama wangefunga chuo kwa mda mpaka pale itakapojiridhisha kuwa tuko salama kama nchi vinginevyo bado siwaelewi kama taasisi kuu ya wasomi kutoa vipeperushi vya kiwoga woga kama hichi.

Haba na haba hujaza kibaba.

Ungewapongeza zaidi - haiyumkiniki kwa maneno yako sasa unawapongeza mdogo mdogo.

Pole pole ndiyo mwendo.
 
Mkuu process ya kugundua dawa au chanjo si mchezo:


Beberu mwenyewe kama unavyomwona na umahiri wake angali anacheza makida makida.

Avumbue nani dawa, UDSM? Thubutu!

Bupeji au Covido eti dawa? Bandugu tutofautishe baina ya dawa na juice za Jambo - JAMUKAYA.

Dawa au chanjo haviji kwa kuoteshwa!
Sasa Daktari wa JF tupe dawa yako kama hizo hazifai.

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Tangu Corona ilipoonekana Kwa mara ya Kwanza China mwanzoni mwa mwaka 2020 Hadi leo, hakujawahi kuwa na njia Bora yenye uhakika wa kuiepuka Corona kama si kudra pekee za Mungu.

Njia sahihi ambayo hata hao UDSM wameionyesha ni Ile no 5#

Vinginevyo Vyote ni kuendelea kupiga kelele zisizosaidia, hata hizo chanjo zibazoendelea kupigiwa upatu, bado hata hao waliozitengeneza hawatupi uhakika wa 100%

Mashaka yanaanzia pale unapokuwa ni lazima mtu achanjwe, swali ni... Mtu akichanjwa Maana yake hawezi kuambukizwa tena huo ugonjwa, sasa Kwa nini wanataka watu wote wachanjwe Wakati Mimi kama sijachanjwa siwezi kumwambukiza aliyechanjwa?
 
Back
Top Bottom