Dr Matola PhD
Platinum Member
- Oct 18, 2010
- 61,429
- 108,577
Wivu kwa jambo gani?
Achana nalo jinga hilo Mwemkundu tangu akawa na akili?
Wivu kwa jambo gani?
Dada mimi sibishani ila sipendi tabia ya mtu kukurupuka na kuanza kulitolea maelezo au kupinga jambo hata asilolijua.
Ktk maisha yako epuka kutoa majibu ya jumla jumla,unajua clauds wana kanda ngapi za matangazo yao?
Ok,huku Arusha tangu jana ni miziki tu lete majibu kama unayo.
Kwani kila mkoa Clouds wana matangazo tofauti? Zile mitabend wanazotaja si frequency za kusikilizia tu ila matangazo ni mamoja?. Ndio maana huwa wanachangia watu wa mwanza,kigoma,tanga,arusha,iringa nk mada moja!
nimegundua wote wanaiponda clouds ndo wasikilizaji wakubwa wa redio hii....acheni unafki wa kuiponda clouds humu jukwaan wakati vyumbani mwenu mnasikiliza clouds.... CLOUDS FM The peoples station!..
nimegundua wote wanaiponda clouds ndo wasikilizaji wakubwa wa redio hii....acheni unafki wa kuiponda clouds humu jukwaan wakati vyumbani mwenu mnasikiliza clouds.... CLOUDS FM The peoples station!..
UMEMALIZA KILA KITU na HUO NDIYO UKWELI WENYEWE na TUACHE UNAFIKI na UZANDIKI. Radio Nyingi Zinasubiri Kwa Clouds FM Japo na Wao Wana Changamoto ambazo Zinarekebishika Endapo Na Wao Watakubali Kurekebishika na Tusisahau Kuwa Contents Nyingi Za Redio hii Ni Haswa Youth Oriented na Target Yao Kubwa Ni ktk Cities na Wamefanikiwa Sana. Mnasema Kuwa Redio Yenyewe ni Pro CCM mara Kibonde ni Mnafiki ila Naomba Mniambie ni Redio Gani hapa Tanzania Haijipendekezi Kwa Serikali au Waandishi Wake Hawana Kimbelembele Kwa Utawala Uliopo? Mbona Hamzungumzi Waandishi Wale wa Redio One Na Yule Wa Gazeti Walioteuliwa Wakuu Wa Wilaya? Je hao Hawajipendekeza Kwa Serikali? Tizama Kila Alhamisi Kipindi cha Kipima Joto ITV Na Angalia Studioni Wakiwemo Watu Hawa Fatma Almasi Nyangasa na Magreth Cosmas Kisha Akijitokeza tu Mtu Anaisema Vibaya Either CCM au Serikali Utawaona Wanavyowakatisha na Hata Kuwapiga Mkwara Wachangiaji Kwa Kuwaonya. Sidhani Kama Kuisema Pekee Clouds FM Kuna Tija Vinginevyo Ninachokiona Ni Unafiki na Chuki Zisizo na Mashiko Yoyote. Hakuna Media Hapa Tanzania Ambayo Haina Madhaifu Yake Ukianzia ktk Public Owned, Private Owned, Community Owned, Institution Owned na Structural Adjusted or Alternative Owned Radio Stations na Kama Wadau Tunachotakiwa Kufanya Ni Kuziunga Mkono Pale Zinapofanya Vizuri na Pia Ndugu Zangu Humu JF Hebu Tujifunze Kufanya Kitu Kiitwacho Critique Nikimaanisha Kwamba Tusipende tu Kukimbilia ktk Kutoa Kashfa badala Yake Tuelezee Mafaniko Ya Jambo au Kitu Fulani Lakini Palipo na Changamoto au Madhaifu Tuziseme Kwa Mtazamo wa Kujenga Zaidi na Si Kurudishana Nyuma. Ni Hayo Wana JF Wenzangu and I am Stand to be Corrected.