Mkuu, kwa swali lako kuna mabo mengi sana. Ntachambua kwa uchache.
1. Ukisoma Clinical medicine, just know utakapomaliza, utasubiri sana kupata chaka maana wako wengi na pia ni ngumu kujiajiri. Lakini kama una mpango wa kuwa daktari bingwa ni njia nzuri, cha muhim uwe na hela ya kutosha kujisomesha mpka kuwa specialist maana wataalam wanapungua zaidi as kiwango cha elim kinavoongezeka
2. Nursing, ni kozi nzuri, lkn ukitaka ajira uishie diploma tu. But kaa ukijua nchi yetu hii bado nurse anachukuliwa poa sana. Yaan anaonekana mtu ambae sio muhim kiutawala so kutumwa ni kawaida (kumradhi)
3. Kama lengo lako ni kufanikiwa mapema, soma course za afya ambazo unaeza kujiajiri kwa mfano radiology, maabara, pharmacy.
4. Tofaut na hapo kasome course kama za macho na anaesthezia, hapo koas flan unakua kwenye market maana hao wataalam sio wengi kiivo.