Clara Luvanga aweka rekodi ya usajili ghali zaidi duniani

Clara Luvanga aweka rekodi ya usajili ghali zaidi duniani

Miss Halima

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2026
Posts
302
Reaction score
643
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Clara Luvanga (21), ameweka rekodi ya dunia ya kuwa mchezaji ghali zaidi katika historia ya mpira wa miguu wa wanawake baada ya kusajiliwa na klabu ya Washington Spirit inayoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake nchini Marekani (NWSL), akitokea Al Nassr ya Saudi Arabia.

1789131240627.png
Luvanga ameweka pia historia ya kuwa Mtanzania wa kwanza kusajiliwa na kucheza katika Ligi Kuu ya Wanawake Marekani (NWSL), baada ya kujiunga na Washington Spirit kwa mkataba wa miaka minne hadi mwaka 2029.

Usajili huo umefanyika kwa ada ya uhamisho ya €1.70M/$2.3M sawa na Tsh. Bilioni 6.081 ambapo msimu wa 2025/26 aliibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Saudia akifunga magoli 24 kwenye mechi 14 na kutwaa Golden Boot.

Ilikuwa ndoto kukutana nae na kupiga picha hatimae ndoto yangu imetimia Nina furaha sana kukut...jpg

Orodha ya wachezaji 10 wa mpira wa miguu wa wanawake waliosajiliwa kwa ada kubwa zaidi duniani (kulingana na picha hizo):

Na.MchezajiKutokaKwendaAda ya Uhamisho
1Clara LuvangaAl-NassrWashington Spirit€1.70M
2Grace GeyoroPSGSan Diego Wave€1.65M
3KerolinManchester City 🏴󠁧󠁢󠁥Barcelona€1.50M
4Felicia SchröderBK HäckenReal Madrid€1.50M
5Lizbeth OvalleTigres UANLOrlando Pride€1.30M
6Olivia SmithLiverpool 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿Arsenal 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿€1.27M
7Alyssa ThompsonAngel CityChelsea 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿€1.24M
8Jaedyn ShawSan Diego WaveNJ/NY Gotham FC 🇺🇸€1.07M
9Naomi GirmaSan Diego WaveChelsea 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿€1.07M
10Melvine MalardManchester United 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿Chelsea 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿€1.00M

Luvanga anaondoka Al-Nassr baada ya kushinda mataji sita, yakiwemo matatu ya ligi mfululizo, pamoja na Saudi Women's Cup, Super Cup na WAFF Women's Clubs Championship.

Washington Spirit imesema Luvanga ameongezwa kwenye kikosi ili kuongeza chaguc katika safu ya ushambuliaji, huku klabu hiyo ikijiandaa kwa hatua ya playoffs ya NWSL.
 
Nyota wa Kimataifa Kutoka Tanzania Clara Luvanga ametangazwa kuwa mchezaji mpya wa Washington Spirit inayishiriki Ligi Kuu ya Marekani akitokea Al Nassr ya Saudi Arabia

Clara amesaini mkataba wa miaka minne mpaka mwaka 2029 na Ada ya uhamisho huo inaripotiwa kuwa Dola Milioni 2 ambayo itakuwa rekodi ya uhamisho wa kihistoria wa dunia kwa soka la wanawake.

Clara Alikuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Saudia msimu uliopita akifunga magoli 24 kwenye mechi 14.
IMG-20260910-WA0051.jpg
 
Ilikuwaje akakosekana timu ya taifa twiga stars katika michuano ya wafcon mwezi uliopita morroco
Na msimu uliopita ulikuwa bora sana kwake
Yatakuwa ni majungu tu

Hongera zake nyingi mtoto wa (Nyabula, Mlolo, Pawaga) Iringa zilikotapakaa koo za akina Luvanga.
 
Watz waliongoza kampeni ya kumsema mwaka flani kuwa sio dada
Napenda namna asivyohangaika na team ya bakari shime
 
Nyota wa Kimataifa Kutoka Tanzania Clara Luvanga ametangazwa kuwa mchezaji mpya wa Washington Spirit inayishiriki Ligi Kuu ya Marekani akitokea Al Nassr ya Saudi ArabiaClara; amesaini mkataba wa miaka minne mpaka mwaka 2029 na Ada ya uhamisho huo inaripotiwa kuwa Dola Milioni 2 ambayo itakuwa rekodi ya uhamisho wa kihistoria wa dunia kwa soka la wanawake.

Clara Alikuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Saudia msimu uliopita akifunga magoli 24 kwenye mechi 14.
View attachment 3667094
Wampekenyue vizuri huyu...pengine anayo mashine!... sura tu inajionyesha
 
Back
Top Bottom