Wakuu mweka hii mada amekosea kujumuhisha watanzania wote USA.Atambue state zingine kuna jumuia zao pia na zipo safi hakuna tatizo.Kwanza naomba niweke wazi kuhusu huu uchaguzi wa kumtafuta kiongozi wa jumuia ya watanzanzania [Maryland,washington dc na virginia].Hawa wagombea uongozi wote katika nafasi ya urais walikuwa kambi moja uchaguzi katika miaka miwili iliyopita.Mmoja amabye alishakuwa rais anaitwa IDD SANDALY na ambae hajawahi kuwa rais ni Liberatus Mwang'ombe.Kwa ufupi nilichoona hapa ni ulevi wa madaraka.Jamani kuna vijana wengi sana smart wanaweza kutuongoza sio lazima tuendelee na mtu mmoja yule yule mwenye idea ile ile na mbinu zile zile.Tuwe na taratibu kuangalia mwingine ata inject mipango ipi katika jumuia huku akichukua yale mazuri aliyoyaweka aliyepita.Na tuendelee na taratibu hii ya kushindani kuweka mikakati na mbinu mpya kwenye jumuia ,kwa kweli kwa miaka sita ijayo jumuia itakuwa mbali sana na strong.Kwa mfano tumejifunza kutoka kwenye jumuia za wenzetu kama waiethiopia na wamexico wapo very smart kuchangia maendeleo ya kwa kuchangia pesa moja kwa moja kwenye mfuko maalum.Ndio maana umeona wa ethiopia wamejenga Dam kubwa ya kufua umeme.Ule ni mchango wa waethiopia walio diaspora.Sasa sis kama watanzania tulio nje tunajifunza nini kutoka kwa wenzetu?hata vifaa vya hospital vinatushinda?.Nimeona sera za Liberatus kwa kweli kwa upande wangu nimekubali ,kwani ameshaonyesha alifanya nini huko nyumbani katika kusaidia jamii na atafanya nini.Huyu kiongozi aliyepita bado hadi sasa ajasema sera zake ,ila ninachoona ni maneno yanarushwa huku na kule.ambayo hayasaidii kitu tunataka useme ulifanya nini na utafanya nini basi lakini propaganda za kizamani tumeshachoka nazo.Naomba tubadilike tuwe positive katika issues za maendeleo ya nchi yetu.Mungu wabariki watanzania wa diaspora na wa Nyumbani.