Chuo Cha Uhasibu Arusha Kugoma Na Kuandamana Hadi Dar.

Mtoto wa Mkulima

JF-Expert Member
Apr 12, 2007
681
126
Habari nilizopata jana kutoka chuo cha uhasibu Arusha ni kwamba. wanafunzi wa chuo hicho wanampango wa kugoma jumatatu na kuandamana hadi body ya mikopo Dar. Mtoa habari aliniambia kuwa wanafunzi hao wamefikia uamuzi huo baada ya kuishi kwa maisha magumu chuoni hapo bila kupata mkopo kutoka bodi ya mkopo kama walivyokuwa wameahidiwa. Aidha inasemekana kuwa mkopo umetolewa kwa baadhi ya wanafunzi wachache na wengine wengi bado hawajapata bila ya maelezo yeyote kutoka kwa uongozi wa chuo (ambacho kinamilikiwa na Hazina) na pia maelezo kutoka wizara ya elimu ya juu/body ya mikopo. Wanafunzi hao walijaribu kutumia njia nyingi za kiplomasia ikiwa ni pamoja na kuwatuma viongozi wao kwenda Dar kuonana na uongozi wa bodi ya mikopo bila ya mafanikio na ndio maana wameamua kufikia uamuzi wa kugoma.

Kwa wale walioko huko Tz hasa Arusha wanaweza kutupatia habari zaidi.


Mimi huwa naumia sana napoona kuwa serikali yetu haijali elimu. Vipaumbele vyetu vikowapi? vijana wanataka kusoma lakini wanashindwa sasa tusipoelimisha vijana wetu taifa la kesho litaendelea kuwa la wajinga na hatutaweza kuondoa umasikini kamwe.
 
na taarifa nilizopata toka jikoni hapa IAA NI KWAMBA KUNA MGOMO MWINGINE WA KUHITAJI MANAGEMENT YA CHUO IHAKIKISHE USALAMA WA WANAFUNZI WANAOISHI HOSTEL ZA NJE KWANIHOSTELI MOJA YENYEWANAFUNZI TAKRIBAN AROBAINI(40) WAMEVAMIWA USIKU WA KUAMKIA JANA IKIWA NI PAMOJA NA KUPIGWA MAPANGA YA VICHWANI NA KUNYANG'ANYWA FEDHA ZOTE WALIZOKUWA NAZO.HIVI SASA NINAVYOONGEA HAWAJUI WATAKULA NINI!!!
"HALI YA USALAMA KWA WANAFUNZI WANAOISHI HOSTELI ZA NJE IMEKUWA TATA SANA KWANI KUIBIWA MARA KWA MARA IMEKUWA NI KAWAIDA HUKU UONGOZI WA CHUO UKIKAA BILA KUCHUKUA TAHADHARI YOYOTE" ALISEMA MWANACHUO MMOJA.NIKAPATA MAELEZO TENA KUWA WAATHIRIKA HAO WANAISHI HOSTELI HIZO KWA KULIPA TSH LAKI TATU KWA AJILI YA HOSTEL TU HUKU NYAKATI ZA USIKU KUKIWA HAKUNA MLINZI NA WANAELEZWA WAJILINDE WENYEWE.
MPAKA SASA RAISI WA CHUO AMEONDOLEWA NA WANAFUNZI KWA KUKOSA IMANI NAYE NA SPIKA NDIO ANASHIKIRIA MADARAKA.
WANACHUO WAMEELEZA HALI MBAYA YA USALAMA INACHANGIA KUFANYA VIBAYA KIMASOMO.NITAENDELEA KUWALETEA KINACHOJIRI IAA ILI MCHANGIE NAMNA YA KUONDOA TATIZO.
 
Nimesikia kuwa wavulana wamevamiwa jana usiku ila sijapata taarifa zaidi. kama kuna mwenye taarifa watujulishe
 
Habari nilizozipata ni kuwa wanafunzi wavulana wa chuo jana usiku walivamiwa na watu wasiojulikana wakiwa na silaha mbali mbali na kuwajeruhi baadhi ya wanafunzi. Inasemekana kuwa wanafunzi hao wameibiwa kila kitu na wamebakiwa na nguo walizokuwa wamevaa tuu. Pamoja na haya nasikia wanafunzi hao kesho wataendelea na mgomo wao kama ulivyopangwa na wataende Bodi ya mikopo ili kujua hatima yao.
 
Naomba Kusahihisha Wameenda Dodoma Na Sio Dar Kwani Wanataka Kuonana Na Waziri Ambae Yupo Dodoma.
Kuhusu Usalama Hilo Limekuwa Tatizo Kwani Semister Hii Wanafunzi Wamevamiwa Mara Mbili Na Kunyanganywa Simu,hela Na Nguo
Uongozi Wa Chuo Haujatoa Tamko Lolote Na Hili Suala Linatokea Kila Mwaka
 
Naomba Kusahihisha Wameenda Dodoma Na Sio Dar Kwani Wanataka Kuonana Na Waziri Ambae Yupo Dodoma.
Kuhusu Usalama Hilo Limekuwa Tatizo Kwani Semister Hii Wanafunzi Wamevamiwa Mara Mbili Na Kunyanganywa Simu,hela Na Nguo
Uongozi Wa Chuo Haujatoa Tamko Lolote Na Hili Suala Linatokea Kila Mwaka


Nadhani uongozi wa chuo utatoa Tamko siku maafa yakitokea hadi wanafunzi wafe au wadhurike sana. si unajua moto ukishazuka na kuuwa ndio hata serikali yetu huwa inanunua gazi za zimamoto?
 
Back
Top Bottom