Chonde chode mliokatwa amani yetu ni muhimu

Chonde chode mliokatwa amani yetu ni muhimu

Stroke

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2012
Posts
38,611
Reaction score
49,009
Kwa hali hii ya vugu vugu la hamaki kwa baadhi ya watia nia kuhama baada ya kukatwa.

Ingawa hakuna dalili ya ushindi kwa namna yoyote ile....

Uelekeo baada ya kuhama na kushindwa katika uwanja wa ushindani ni kwa wahusika kuelekeza nguvu zao msituni.

Dalili za kushindwa zipo kwa viashiria vya kuonesha azma ya wazi kabisa ya ung'an'ganizi, uliowashtua wengi.

Kila mwenye akili zake anauliza, huko kuna nini mpaka nguvu zote hizo zitumike....

Si ajabu sana, hata baada ya nafasi kupatikana kwa kushindana na waliowakata, endapo wakishindwa kugeuza uhasama wa moja kwa moja.

Ni rai yetu sisi kina kamchape, ambao hatujui sababu za kukatana, na kwanini kina flani wakahama, kuachiwa amani yetu ambayo ndio zawadi pekee tuliyobakiwa nayo baada ya rasilimali zetu kuendelea kuwanufaisha wachache.

Mnaposuguana, msituharibie vimkate vyetu. Bado tunahitaji amani....

Hatutawaunga mkono mkitaka kwenda msituni...
 
hutawaunga mkono ww na nani??????????? sisi watanzania tumejikamilisha mwaka huu na tuko tayari kwa lolote kama hutaki pita hivi
 
Nawashauri watia nia ya Urais waliokatwa majina yao na CCM wahamie CHADEMA kuliko na utulivu na amani na vyeo watapata kwenye Serikali ya Ukawa.
 
Lakini mbona hatujaona Chadema ikufungua milango kwa wanachama wengine wachukue fomu? Wamemuandaa EL pekee ... hiyo ndiyo demokrasia kweli? Mnasema CCM haina demokrasia mbona hata Chadema siioni? maamuzi yote yalifanywa na wachache juu. Mimi siyo mwanachama wa chama chochote ila naangalia mambo yanavyokwenda
 
KWa jinsi ikulu inavyotafutwa kwa hali na mali.
Vita ileee inanukiaa.....Arusha itawaka moto..Dar hapatakalika tena....Mwanza kutakua na msuguano wa kutosha
watakaopoteza maisha ni wananchi viongozi wote watakua salama
 
angalia hapo chini uwone maamuzi magumu ya lowasa na ucomment.
 

Attachments

  • 1438263651872.jpg
    1438263651872.jpg
    22.3 KB · Views: 141
kungia chama cha wapiga dili ni maamuzi magumu kwelikweli ingawa sio ya busara!Hata majambazi hufanya maamuzi magumu
 
Wakuu,tarehe22 kampeni zinaanza na Leo EL kakanidhiwa form na CHADEMA na HUENDA UKSWA wakamteua kwa vyovyote vile.SASA kazi ni kazi, twende kazi.maana huu Allah karim
 
Lakini mbona hatujaona Chadema ikufungua milango kwa wanachama wengine wachukue fomu? Wamemuandaa EL pekee ... hiyo ndiyo demokrasia kweli? Mnasema CCM haina demokrasia mbona hata Chadema siioni? maamuzi yote yalifanywa na wachache juu. Mimi siyo mwanachama wa chama chochote ila naangalia mambo yanavyokwenda
Utakuwa umemezeshwa hivyo na kina Nape. Kama unasifa nenda kachukue fomu ndugu milango ipo wazi
 
Lakini mbona hatujaona Chadema ikufungua milango kwa wanachama wengine wachukue fomu? Wamemuandaa EL pekee ... hiyo ndiyo demokrasia kweli? Mnasema CCM haina demokrasia mbona hata Chadema siioni? maamuzi yote yalifanywa na wachache juu. Mimi siyo mwanachama wa chama chochote ila naangalia mambo yanavyokwenda
Ulienda kuchukua ukakataliwa?
 
Back
Top Bottom