CHOMBEZO:NIFANYE NA MIMI KAKA DICK

CHOMBEZO:NIFANYE NA MIMI KAKA DICK

NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-32
JUMA HIZA

Age:18+

ILIPOISHIA.....
Kazi kubwa iliyokuwa imebakia kwa wakati ule ilikuwa ni kutafuta njia ya ziada ya kuweza kumuingilia Evadia mpaka akubali kunisaidia nia yangu ya kutoa filamu na muigizaji huyo ambaye alikuwa na urafiki naye. Ilikuwa ni kazi ngumu mno lakini niliamini kufanikiwa katika hilo.

SONGA NAYO......

Ulikuwa ni mwanzo wangu wa kuonyesha mapenzi ya dhati niliyokuwa nayo kwa Evadia, nilikuwa nikionyesha kumpenda sana kiasi kwamba kuna kipindi alikuwa akishangaa upendo ule ulikuwa unatokea wapi hasa. Kila siku sikuacha kumtafuta, nilikuwa nikimtumia ujumbe mfupi na hata pale alipoonekana kuwa kimya kwa kutonijibu ujumbe wangu niliamua kumpigia na hapo tuliweza kuzungumza mambo mengi sana kuhusiana na mapenzi yetu. Alionekana kuniamini kwa kila kitu na hiyo ndiyo ilikuwa ngao yangu kubwa ya kutimiza lengo langu kwa wakati ule.
“Baby halafu kuna kitu nataka kukuambia,” aliniambia Evadia siku moja tulipokuwa dukani kwake.
“Kitu gani?”nilimuuliza.
“Nataka uje ujitambulishe kwa wazazi wangu,” aliniambia kisha nikabaki nimeshikwa na butwaa kwa muda halafu nikajilazimisha kutoa tabasamu, nilikuwa nikitabasamu tabasamu la uwongo, sikuwa nikitegemea kama Evadia angeweza kuniambia maneno yale kwa wakati ule.
“Nini?” aliniuliza mara baada ya kuniona nikitabasamu.
“Hamna kwahiyo unataka twende lini?”
“Hata kesho mpenzi siunajua jinsi ninavyokupenda?”
“Ndiyo nafahamu ila tusifanye kesho unaonaje tukapanga siku nzuri ambayo nitaweza kwenda kujitambulisha kwa wazazi wako?”
“Sawa nimekuelewa mpenzi naamini wewe ndiyo mume wangu mtarajiwa.”
“Hata mimi naamini wewe ndiyo mke wangu wa maisha,” nilimwambia kisha tukakumbatiana.
Mapenzi yangu na Evadia yaliendelea kupamba moto kila siku, nilijitahidi sana kumfanya azidi kuwa karibu yangu kiasi kwamba hata nitakapofikia hatua ya kumueleza nia yangu asiweze kunikatalia, niliamini kulikuwa na ugumu katika kulitimiza hilo na ndiyo sababu iliyonifanya nizidi kuwa mpole.
****
Penzi la Precious bado halikufutika kichwani mwangu niliendelea kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi lakini mapenzi yetu yalikuwa ni ya kujiiba. Nilifahamu fika kuwa Precious alikuwa ni mke wa mtu, mke wa mwanaume ambaye alikuwa akipambana usiku na mchana kutafuta riziki ili aweze kuihudumia familia yake.
Kwa muda mrefu wa ndoa yake hakuwa amebahatika kupata mtoto na hii ndiyo sababu iliyomfanya apunguze mapenzi kwa mume wake. Alikuwa akiniambia mambo mengi sana na jinsi ambavyo ndugu wa mume wake walivyokuwa wakimuandama kwa maneno yaliyokuwa yakizidi kumuweka katika wakati wa maumivu kila siku, alikuwa akitamani sana kupata mtoto katika ndoa yake lakini hakubahatika.
“Ndoa yangu inanitesa sana, natesekea Dick natamani mpaka kufa,” aliniambia Precious huku machozi yakimdondoka, alikuwa akilia kwa uchungu mno.
“Hapana hutakiwi kusema hivyo unakufuru,” nilimwambia huku nikijaribu kumbembeleza, alikuwa akibubujikwa na machozi kwa wakati huo, sikutaka kuyaacha machozi yake yaendlee kumtoka mbele yangu, niliamua kumfuta.
“Dick ndugu wa mume wangu wananinyanyapaa sana kila siku ugomvi hauishi ndani ya nyumba.”
“Kwani unaishi nao pamoja?”
“Ndiyo baada ya kuona sijampatia kaka yao mtoto wameamua kunifuata na lengo lao kubwa wanataka niachike.”
“Mh! Kweli hilo ni tatizo.”
“Dick naumia sana, naumia sana,” aliniambia kwa sauti iliyogubikwa na wimbi la masikitiko makubwa.
Kila nilipokuwa namtazama alizidi kuonekana kuwa mtu mwenye shida, sura yake ya masikitiko ilizidi kunidhihirishia wazi kuwa kulikuwa na kitu alichokuwa anakihitaji kwa wakati ule, sikutaka kujifanya ajuza wa kufahamu kila kitu, niliamua kuwa mkimya nikimpa nafasi ya kutaka kujielezea na kama yalivyokuwa mawazo yangu aliniita kwa sauti ya chini huku uso wake akiwa ameuelekeza chini kisha nikamuitikia huku nikiyapa wasaa masikio yangu yaweze kumsikiliza.
“Naomba unisaidie kitu kimoja,” aliniambia.
“Kitu gani?” nilimuuliza.
“Naomba unipatie mtoto sina tatizo lolote mimi katika kizazi changu, tatizo lipo kwa mume wangu naomba unipe ujauzito na ninakuahidi ile ahadi yangu ya kukupa nyumba pamoja na mtaji wa kutoa vitabu vyako nitakupa, naomba unisaidie niondokane na fedhea hii inayoniandama katika maisha yangu,” aliniambia Precious.

Je, ni nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo ya Chombezo hili mahali hapahapa.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-33
JUMA HIZA

Age:18+

ILIPOISHIA.....
“Naomba unisaidie kitu kimoja,” aliniambia.
“Kitu gani?” nilimuuliza.
“Naomba unipatie mtoto sina tatizo lolote mimi katika kizazi changu, tatizo lipo kwa mume wangu naomba unipe ujauzito na ninakuahidi ile ahadi yangu ya kukupa nyumba pamoja na mtaji wa kutoa vitabu vyako nitakupa, naomba unisaidie niondokane na fedhea hii inayoniandama katika maisha yangu,” aliniambia Precious.

SONGA NAYO......

Kwa kweli nilibaki nikimshangaa Precious nisijue ni nini nimjibu kwa wakati ule, ni kweli nilikuwa katika mahusiano naye na pia nilikuwa nikifanya naye mapenzi sana kiasi kwamba hakukuwa na kitu kigeni ambacho nilikuwa sikifahamu katika mwili wake, nilikuwa nikimfahamukila kitu kama mume wake wa ndoa.
Kwa muda wote huo ambao niliweza kushiriki naye mapenzi nakumbuka nilikuwa makini sana, sikutaka niweze kumpa ujauzito hivyo kila golinililokuwa nikilifunga nilihakikisha nalitoa nje ama kama niliweza kulifungia ndani basi nilihakikisha hakuwa katika siku zake za hatari.
Nilifahamu kuwa Precious alikuwa ni mke wa mtu na wala sikutaka kujisahaulisha hilo, nilikuwa nikishiriki naye kila aina ya starehe lakini kichwani mwangu sikuacha kuitengeneza picha ya mume wake, nilifahamu madhaifu ya mume wake hata kile kipindi ambacho niliweza kuzungumza naye kwenye simu bado nilizidi kuujua udhaifu aliyokuwa nao.
Lilipokuja suala la mke wake na kwa uchafu ambao niliyokuwa nikimfanyia sio siri kuna kipindi nafsi yangu ilikuwa inanisuta. Ilinisuta kwa maovu niliyokuwa nikiyafanya.
Kitendo cha Precious kuniambia kuwa alikuwa akihitaji mtoto na alikuwa radhi kuubeba ujauzito wangu hakika kilikwenda kunichanganya akili yangu sana, nilihisi kupata mtihani mgumu sana japo aliniambia kuwa angeweza kunipa pesa, nyumba pamoja na mahitaji mengine lakini kwa upande wa pili wa shilingi niliingiwa na uwoga, sikutaka kujiamini sana na ni hapo ambapo nikajikuta naingia katika mgogoro dhidi ya nafsi yangu, kuna muda nilikuwa nikitamani sana pesa, nyumba nzuri, gari la kifahari lakini akili yangu ilipowaza siku ambayo ningeweza kukamatwa na mume wake hakika nilizidi kuingiwa na uwoga, niliamini nilikuwa katika harakati za kukitafuta kifo changu ambacho kilikuwa mikononi mwa mwanaume mwenye hasira kali ya kuibiwa mke wake.
“Mbona unajifikiria hivyo?” aliniuliza.
“Hapana Precious nawaza,”nilimwambia.
“Unawaza nini sasa wakati nimekuambia kama ni pesa nitakupa.”
“Tatizo sio pesa Precious.”
“Ila.”
“Kumbuka wewe ni mke wa mtu.”
“Nafahamu Dick ila naahidi kufanya iwe siri.”
“Siri?”
“Ndiyo itabaki kuwa siri kati yetu.”
“Siamini kama kuna siri hapo hivi mumeo ni mjinga kiasi gani mpaka umefikiria kuchukua uamuzi huo.”
“Dick naomba uniamini mimi hakuna kibaya chochote ambacho kitaweza kukutokea kwanza shida yangu ni kupata mtoto tu.”
“Mumeo akijua kuwa ujauzito sio wake unafikiri ni nini kitatokea?”
“Si rahisi kama unavyodhani Dick naomba unielewe basi,” aliniambia Precious kwa sauti iliyokosa kabisa uvumilivu, alikuwa amekimaanisha kile alichokuwa akikiomba, nilipomtazama na yeye alinitazama kwa macho yaliyoniambia “Nifanye Dick sasa hivi hivi.”
Nilizidi kuwaza mambo mengi sana kichwani mwangu lakini kila nilipokuwa nikijaribu kuwaza na kuwazua ajabu sikubahatika kabisa kung’amua lolote zaidi nilizidi kuona dakika zikizidi kujongea kwa kasi sana kusababisha mabadiliko ya saa. Nilizidi kupagawa.
“Dick inamaana umekataa kabisa kunisaidia?” aliniuliza Precious huku akiendelea kunitazama kimatamanio.
“Precious unaniingiza katika matatizo,” nilimwambia huku nikionekana kuzidi kutawaliwa na uwoga.
“Embu acha uwoga Dick.”
“lazima niwe na uoga kumbuka wewe tayari umeshakua mke wa mtu sasa nitaanzaje kukupa ujauzito huoni nitakuwa nakimbilia matatizo?”
“Kwanini hutaki kuniamini lakini nimekuambia hakuna kibaya kitakachokupata shida yangu ni unipe ujauzito tu,” aliniambia kwa sauti iliyoonyesha msisitizo wa kauli yake.
Baada ya maneno yale sikutaka kuwaza mara mbilimbili, nilichoamua kukifanya ni kumpa alichokuwa akikihitaji.
Nilianza kwa kumtomasa taratibu mpaka akaanza kuzichojoa nguo zake mwenyewe, haikuchukua muda na mimi nikaweza kuzichojoa zangu na kitendo kilichofuata nilianza kuutumia ulimi wangu katika kutalii sehemu mbalimbali za mwili wake laini ambao ulizidi kunisisimua kila nilipokuwa napita. Sauti na miguno ya kimahaba aliyokuwa akiitoa mahali pale iliufanya mpaka mtarimbo wangu ukawa umesimama wima halafu ukaanza kutokwa na majimaji legevu mithili ya mlenda. Sikuacha kuupeleka ulimi wangu katika vile vitongoji ambavyo vilikuwa vikisifika kwa kutoa ladha ya utamu mithili ya rojorojo za chocolate.
“Aiiiisssshhh Babyyyyyyyyyyyyyy,” alizidi kutoa miguno hapa ni baada ya kufika katika kisima cha chumvi.
“Yeees babyyyy,” nilimuitikia huku nikijaribu kuizuia mihemko iliyokwisha anza kunipanda kwa wakati huo. Nilijitoa ufahamu kisha nikawa naendelea kupasugua pale kwenye kisimi kwa kuutumia ulimi wangu.
Ulikuwa ni mchezo mdogo ambao nilikuwa nikiurudia mara kwa mara, niliamini ulikuwa ni mchezo wa utamu utamu niliyokuwa nikimpa Precious kwa wakati huo alikuwa hoi bin taabani akisubiria dozi ya mapenzi.
“Tamuuuuuu babyyy ooooooohhhh aaaaiiiishhhhhh,” alizidi kulalamika kimahaba katika namna ya sauti iliyoniweka katika wakati mgumu sana, mtarimbo wangu ulikuwa umesimama muda wote huo ukisubiria mechi.
“Inatoshaaaaaa babyyyyyy aaaaaaaahhhhh inatoshaaaaaaa ooooooohhhh,” aliniambia huku akionekana kuzidiwa.
Nilitoka chumvini na sasa nikaingia rasmi katika mgodi, nilianza kwa pupa katika kuchimba madini kiasi kwamba nilishindwa kabisa kujizuia, nikajikuta goli la kwanza nimelimwagia ndani.
“Oooooooh,” niliutoa mguno huku nikiwa nimejilaza kifuani mwa Precious, alikuwa amening’ang’ania vilivyo kwa wakati huo, hakutaka nitoke nje hata kidogo na kitendo cha goli la kwanza kulimwagia ndani alikifurahia sana, alinipokea kwa mabusu mfululizo huku akizidi kunishukuru.
“Asante mume wangu asanteeeee,” aliniambia maneno ambayo sidhani kama aliyahakiki kabla ya kunitamkia, sikua mume wake wa ndoa lakini nilishangaa akiniita jina hilo huku akiwa amenikumbatia.
Labda nikuambie kitu ni katika siku hiyohiyo ambayo niliweza kufanya mapenzi na Precious tena katika siku zake za hatari lakini ajabu alikuwa akifurahia kila bao ambalo nilikuwa nikilimwagia ndani, aliamini kuwa hitaji lake lilikuwa linakwenda kutimia. Hivyo furaha ilizidi kuchukua nafasi kubwa katika uso wake.
****
TABATA BIMA, DARESALAAM.

Ilikuwa ni siku ya jumamosi tulivu, hali ya hewa ilikuwa ni ya joto la wastani katika jjiji la Daresalaam. Siku hiyo ilikuwa ni siku ambayo Evadia aliamua kunipeleka nyumbani kwao Tabata kwa lengo la kwenda kunitambulisha.
Ilikuwa ni moja kati ya ndoto yake kubwa aliyokuwa akitamani kuitimiza siku moja, ndoto ya kumpata mpenzi ambapo wazazi wake wataweza kumfahamu.
Nakumbuka siku hiyo nilienda dukani kwake nikatafuta suti nzuri ambayo iliweza kunipendeza sana, ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuonekana katika muonekano wa vazi la suti.
“Karibu baba,” alinikaribisha Mama yake.
“Karibu kijana,” alinikaribisha Baba yake.
“Asanteni Baba na Mama,” nilijibu kwa sauti ya upole.
“Unaitwa nani?” aliniuliza Baba yake Evadia.
“Naitwa Dick,’ nilijibu kwa kujiamini.
“Unaitwa Dick! hilo ndiyo jina lako?” aliniuliza baba mtu kwa ukali wakati huo mama yake alikuwa kimya.
“Hapana Baba mimi naitwa Dickson Felix,” nilimwambia.
“Anha! Unajishughulisha na kazi gani?” aliniuliza.
“Mimi ni mwandishi wa hadithi hivyo kazi yangu kubwa ni uandishi.”
Hayo yalikuwa ni moja kati ya maswali na majibu ambayo yaliweza kunikabili siku hiyo lakini kitu ambacho nilikishukuru ni kuwa kila kitu kilikwenda vizuri, hakuna kitu kilichoweza kwenda mrama siku hiyo.
Baada ya utambulisho ule na pamoja na wazazi wake Evadia kuonekana kunikubali kwa kila kitu, nilichoamua ni kuitumia siku hiyohiyo katika kumuelezea Evadia dhamira yangu ya kutaka kutoa hadithi yangu iweze kuchezewa filamu na Irine muigizaji ambaye alikuwa ni rafiki yake.
“Usijali nitazungumza naye na kila kitu kitakwenda sawa,” aliniambia Evadia maneno yaliyonipa matumaini makubwa sana.

Je, ni nini kitaendelea?
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-34
JUMA HIZA

Age:18+

ILIPOISHIA.....

Baada ya utambulisho ule na pamoja na wazazi wake Evadia kuonekana kunikubali kwa kila kitu, nilichoamua ni kuitumia siku hiyohiyo katika kumuelezea Evadia dhamira yangu ya kutaka kutoa hadithi yangu iweze kuchezewa filamu na Irine muigizaji ambaye alikuwa ni rafiki yake.
“Usijali nitazungumza naye na kila kitu kitakwenda sawa,” aliniambia Evadia maneno yaliyonipa matumaini makubwa sana.

SONGA NAYO....

Evadia aliamua kujitoa muhanga katika kuhakikisha ndoto yangu inatimia, alijitoa sana kwangu, aliutumia muda wake mwingi sana katika kuzungumza na Irine. Aliamini katika urafiki aliyokuwa nao kwake hivyo alizidi kuniondoa hofu kuwa kila kitu kingeweza kutimia.
“Vipi imekuaje amekubali?” nilimuuliza siku moja huku nikionekana kukosa matumaini kabisa kwani ilikuwa tayari imeshapita wiki moja tangu alipoanza kufuatilia suala hilo.
“Bado usiwe na wasiwasi mpenzi atakubali,” aliniambia katika namna ya kunipa matumaini.
“Lini?” nilimuuliza.
“Atakubali tu! kikubwa unatikiwa uwe na subira kumbuka yule ameshakuwa msanii mkubwa na ana mambo mengi anayafanya lakini hata hivyo nilikumbuka kumpatia namba yako ya simu, aliniambia atakutafuta,” aliniambia Evadia kwa sauti iliyozidi kunidhihirishia wazi kuwa alikuwa akinipenda sana.
Niliendelea kuvuta subiria katika hilo, siku nazo hazikuacha kusonga mbele kwa kasi na kila ilipokuwa ikiitwa leo nilianza kumuona Evadia alikuwa ni miongoni mwa wale wasichana waongo ambao ukweli kwao ulikuwa ni mwiko. Nilihisi wenda alikuwa amenidanganja kwa kuniambia kuwa aliweza kumpa namba yangu Irine ili aweze kuwasiliana na mimi, jambo ambalo sikutaka kuliamini kabisa.
****
Siku moja nilipokuwa ndani ya chumba changu nimejilaza kitandani niliweza kupigiwa simu na namba ngeni nisiyoifahamu, nilipoitazama na kuligundua hilo sikutaka kupokea kabisa, niliamua kuachana nayo kwani nilihisi watakuwa ni wale mashabiki zangu wa Machombezo ambao kila siku walikuwa wakinisumbua.
Simu ilikata lakini iliweza kupigwa tena, niliendelea kuitazama bila kupokea lakini safari hii uvumilivu ulianza kunishinda, nikaamua kupokea huku nikionekana kuwa mvivu nikatega sikio langu vyema kusikiliza.
“Nazungumza na Dickson?” sauti nyororo ya kike ilinipokea kwa kuniuliza swali.
“Yes! Ndiyo mimi wala hujakosea,” nilijibu huku nikionekana kama nisiyejisikia kuongea kabisa, nilikuwa nikijilazimisha.
“Unajua unazungumza na nani?”
“Hapana sikufahamu.”
“Naitwa Irine Kisoka,” alijitambulisha kisha ghafla! nikainuka pale kitandani nilipokuwa nimejilaza nikakaa, nilikuwa nimeyatoa macho yangu kwa mshangao, nilikuwa siamini kabisa kama kweli Irine alikuwa amenipigia simu kwa wakati huo.
“Irine ni wewe kweli?”
“Ndiyo mimi,” alijibu kisha akanyamaza kidogo halafu akaendelea kuzungumza.
“Nimepokea taarifa kuhusu wewe kutoka kwa rafiki yangu Evadia. Ameniambia kuwa wewe ni mwandishi wa hadithi mitandaoni, nimejaribu kuzitafuta kurasa zako alizonitajia ambazo ni Facebook na Instagram na nimezipitia baadhi ya hadithi zako kwa kweli ni nzuri, kipaji unacho hongera sana,” aliniambia Irine.
“Asante sana,” nilimwambia.
“Kwahiyo unataka ufanyie filamu hadithi ipi?” aliniuliza.
“Ipo hadithi nimeiandika ambayo nimepanga kuifanyia filamu,” nilimjibu.
“Inahusu nini na inaitwaje?”
“Hadithi inaitwa BADO UNAISHI MOYONI MWANGU na inahusu mapenzi.”
“Kuna kitu gani kipya katika hadithi yako?”
“Vipo vingi sana na ndiyo maana nataka kuifanyia filamu?”
“Unajua kwanini nimekuuliza hivyo?”
“Hapana sifahamu.”
“Zipo hadithi nyingi sana za mapenzi pamoja na kazi nyingi ambazo wasanii wamekuwa wakiziingiza sokoni lakini zimekuwa hazifanyi vizuri kutokana na kufanana kwa hadithi, unakuta kisa ni kile kile kinarudiwa katika mtindo tofautitofauti.”
“Ni kweli kama unavyosema lakini hadithi hii ni ya kipekee sana.”
“Unauhakika itafanya vizuri?”
“Ndiyo ninauhakika?”
“Unaishi wapi?”
“Tandale.”
“Basi sawa kesho nitakupa maelekezo ili uweze kufika kwenye kampuni yangu na nitakukutanisha na wadau wa filamu ambao wataweza kulisimamia hilo.”
“Sawa nitashukuru sana.”
“Usijali,” alinijibu kisha akakata simu.
Kama nilivyotangulia kukusimulia hapo awali kuwa Irine alikuwa ni muigizaji maarufu sana wa filamu lakini pia alikuwa akimiliki kampuni yake ya uzalishaji filamu ambayo ilikuwa ikijulikana kama Kisoka Film Company. Ilikuwa ni moja kati ya kampuni bora ambayo ilikuwa ikiaminiwa sana katika kutengeneza filamu nzuri ambazo zilikuwa zikipendwa sana hususani filamu za kimapenzi.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane katika sehemu ijayo mahali hapahapa.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-35
Mtunzi:Juma Hiza

Age:18+

ILIPOISHIA....

Kama nilivyotangulia kukusimulia hapo awali kuwa Irine alikuwa ni muigizaji maarufu sana wa filamu lakini pia alikuwa akimiliki kampuni yake ya uzalishaji filamu ambayo ilikuwa ikijulikana kama Kisoka Film Company. Ilikuwa ni moja kati ya kampuni bora ambayo ilikuwa ikiaminiwa sana katika kutengeneza filamu nzuri ambazo zilikuwa zikipendwa sana hususani filamu za kimapenzi.

SONGA NAYO.......

Hakukuwa na kitu nilichokuwa nakipenda katika maisha yangu kama umaarufu, nilikuwa nikiupenda sana umaarufu. Niliamini katika umaarufu ningeweza kupata vitu vingi kwa urahisi moja ya vitu hivyo ni wanawake. Hata nilipoamua kuandika machombezo yangu katika mitandao ya kijamii kitu cha kwanza nilichokuwa nikikifikiria ni umaarufu. Naam! Katika hilo naweza kusema nilifanikiwa kwa kiasi fulani kwani licha ya kuwa na umaarufu wa mitandaoni niliweza kutembea na wanawake lukuki.
Ngoja nikuambie kitu ndugu yangu katika haya maisha kuna vitu vine vya msingi ambavyo mimi huwa naamini vikikosekana kwa mwanaume basi katika sekta nzima ya mapenzi atanyanyasika sana, vitu venyewe ni Elimu, Pesa, Umaarufu na Muonekano. Sikulazimishi uniamini haya niyasemayo ila najaribu kukuaminisha katika mkasa huu wa maisha yangu uliyonitokea.
Bado nilikuwa siamini kwamba niliweza kuzungumza na Irine ambaye aliniahidi kuhakikisha ndoto yangu ya kutoa filamu inatimia, kwa kweli nilikuwa nikijihisi furaha isiyokuwa na kifani. Niliamua kumpigia simu Evadia nyakati za usiku.
“Nimezungumza na Irine,” nilimwambia Evadia huku furaha ikiwa imenitawala kwa kiasi kikubwa.
“Anasemaje?” aliniuliza Evadia.
“Amekubali kufanya kazi na mimi.”
“Hongera mpenzi naamini utafanikiwa katika hilo.”
“Nakushukuru sana Mpenzi wangu najua bila wewe hili lisingeweza kutimia.”
“Usijali Mume wangu ni wajibu wangu kuhakikisha nafanya kila niwezalo mpaka natimiza kitu katika maisha yako.”
“Upo sahihi mpenzi wewe ndiyo daraja la mafanikio yangu.”
“Hata kwako pia wewe ndiyo kila kitu kwangu.”
“Wakati mwingine siamini kabisa.”
“Huamini nini?”
“Kama nimweza kukupata umekuwa wangu.”
“Amini nimeshakuwa wako.”
“Nakupenda sana Evadia, nakufananisha na ngozi ama damu mwilini ukiondoka mimi si kitu tena.”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kwasababu nakupenda sana, moyo wangu unauhitaji ukaribu wako, unakupenda Evadia.”
“Nakupenda pia Dick mpaka nimeamua kukutambulisha kwa wazazi wangu hivi bado huamini kuwa nakupenda, nataka kuishi na wewe.”
“Kuna siri inanitesa moyoni mwangu.”
“Siri gani?”
“Naogopa kukupa siri hii utaitangaza.”
“Ina maana huniamini?”
“Nakuamini sana.”
“Basi niambie ni siri gani hiyo?”
“Kabla sijakwambia niahidi kwanza.”
“Nikuahidi nini?”
“Kuwa hutomwambia mtu mwingine zaidi, itabaki kuwa siri yako.”
“Nakuahidi sitamwambia mtu mwingine yule itabaki kuwa siri yangu.”
“Siri yenyewe….”
“Enhe! niambie ni siri gani hiyo?”
“Nakupenda,” nilimwambia neno ambalo lilimfanya acheke sana, hakutegemea kama ningeweza kumwambia neno lile kwa wakati ule.
“Halafu sitaki uchokozi wako.”
“Hahaha!”
“We cheka tu!”
“Ndiyo umenuna?”
“Ndiyo nimenuna.”
“Usinune bhanaa.”
“Niache mimi.”
“Jamani mpenzi we mwenyewe unajua kuwa tabasamu lako limeimiliki furaha yangu sasa ukinuna unafikiri nitaishi vipi?”
“Niache nimenuna.”
“Usinune mpenzi.”
“Sitaki niachee,” aliniambia Evadia huku akijifanya kununa mnuno wa kimapenzi. Nilianza kazi ya kumbembeleza huku nikijitahidi kutumia mashairi mazuri katika kumrudisha katika hali yake ya kawaida, hahaha! Mapenzi bhanaa! Ilifikia wakati akatulia na ule mnuno wote ukamuisha. Siku hiyo iliweza kupita.
****
Niliamka katika siku nyingine ya kitofauti sana, naweza kusema ilikuwa ni miongoni mwa siku niliyokuwa nikitamani itokee katika maisha yangu. Nilipokea simu kutoka kwa Irine ambapo aliweza akunielekeza mahali nilipotakiwa kwenda kwa lengo la kupeleka Hadithi yangu.
“Kwa hiyo nikifika hapo Mori naelekea wapi sasa?” nilimuuliza.
“Utanijulisha kuna mtu atakufuata hapo,” alinijibu.
“Sawa kwahiyo naruhusiwa kuja mida hii?”
“Ndiyo.”
“Basi sawa nakuja.”
“Oky,” alinijibu na huo ndiyo ulikuwa mwisho wa mazungumzo yetu.
Sikutaka kupoteza muda niliamka nikaenda kuoga, niliporudi kutoka bafuni nilivaa nguo zangu na sasa nikawa natoka kuelekea Sinza Mori mahali ambapo nilitakiwa kwenda kwa wakati huo. Nilikumbuka kumtumia ujumbe mfupi Evadia lakini hakuweza kunijibu kwa wakati huo. Niliamua kutoka.
Wakati nilipokuwa kwenye daladala simu yangu iliingia ujumbe mfupi, nilipoitoa mfukoni na kuufungua, ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Precious, alikuwa ameniandikia kwa kuniita jina langu
“Dick!”

Je, ni nini kitaendelea?
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-36
Mtunzi:Juma Hiza

Age:18+

ILIPOISHIA....

Wakati nilipokuwa kwenye daladala simu yangu iliingia ujumbe mfupi, nilipoitoa mfukoni na kuufungua, ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Precious, alikuwa ameniandikia kwa kuniita jina langu
“Dick!”

SONGA NAYO.....

Nilikumbuka siku chache zilizokuwa zimepita katika ile siku ambayo Precious alikuwa akiniomba nifanye naye mapenzi kwa lengo la kumpa ujauzito. Alikuwa akitamani kuwa na ujauzito kwa kipindi cha muda mrefu, siku ile aliponiomba kisha nikaweza kumkubalia ombi lake hakika aliweza kufurahi sana.
Sikutaka kujiuliza mara mbilimbili kuwa kitendo cha Precious kuamua kunitafuta alimaanisha nini. Nilifahamu bila shaka nilikuwa nakwenda kupewa taarifa za ujauzito wangu aliyokuwa ameubeba. Hata hivyo sikutaka kuwaza sana, nilipozikumbuka ahadi zake alizokuwa ameniahidi nilihisi kufanikiwa katika maisha yangu.
“Precious,” niliamua kumuandikia ujumbe kwa kumuita jina lake kama yeye alivyoweza kuniita, wakati huo daladala ilikuwa imefika kituo cha Sinza Kumekucha.
“Uko wapi?” aliniuliza.
“Naelekea Sinza mara moja kuna dili nafuatilia.”
“Asubuhi hii.”
“Ndiyo.”
“Dili gani hilo?”
“Dili tu.”
“Ndiyo ni dili gani?”
“La hadithi.”
“Sawa utarudi saa ngapi?”
“Sijajua ila nitakuambia wakati nikiwa narudi.”
“Kwani utachelewa sana?”
“Hapana sio sana.”
“Ok basi utakaporudi utaniambia ili nikufuate kuna sehemu nataka nikupeleke?”
“Sehemu gani?”
“Nitakwambia.”
“Wapi?”
“Mbona maswali mwengi Dick wewe usijali muda huo mimi nitakufuata halafu tutaenda wote?”
“Sawa,” nilimjibu kisha nikashangaa mbona hakuweza kunipa taarifa zozote za ujauzito.
“Au nilifunga nje siku ile?” nilijiuliza lakini sikutaka kujipa muda wa maswali mengi ambayo sikuwa na majibu yake. Nilihisi kuukosa utajiri.
Baada ya dakika kadhaa niliweza kufika Sinza Mori, nilikumbuka kumpigia simu Irine ili niweze kumjulisha kuwa tayari nilikuwa nimeshafika lakini nilipoamua kufanya hivyo nilishindwa, simu yangu ilikuwa imeisha salio.
Sikutaka kupoteza muda haraka nikaweza kununua muda wa maongezi kupitia huduma za kifedha, nikajiunga halafu nikaweza kumpigia simu Irine. Hakuwa akipokea simu kwa wakati huo, kila nilipokuwa nikimpigia simu yake ilikuwa ikiita mpaka ikawa inakata yenyewe. Nilihisi kama kudharauliwa sana, yani mbali na kupigia simu kama mara sita bado hakuweza kupokea.
“Huyu boya anajiona mzuri sana au huo umaarufu ndiyo unamchanganya mpaka anashindwa kupokea simu yangu,” nilijiambia huku nikifyonza, nilianza kuingiwa na hasira.
Baada ya dakika kama kumi ndipo alipoweza kunitumia ujumbe mfupi.
“Umefika tayari?”
“Ndiyo nimeshafika muda tu.”
“Ooh! Sorry upo hapo Mori.”
“Ndiyo.”
“Ok kuna mtu namuagiza anakuja kukufuata hapo.”
“Ok.”
Kama alivyoweza kuniambia baada ya dakika kadhaa niliiona gari aina ya NOAH yenye rangi nyeusi iliweza kunifuata. Sikutaka kushangaa sana kwani nilifahamu mtu niliyekuwa nikiwasiliana naye alikuwa ni mtu wa namna gani hivyo kuliona gari kama lile mbele yangu wala waikuweza kunishtua hata kidogo sana sana nilikuwa makini kumuangalia huyo mtu aliyenifuata alikuwa ni nani.
“Wewe ndiyo Dick?” aliniuliza dereva huku akinitazama kwa madharau.
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikimtazama kwa kumthaminisha, alionekana kuwa mtu fulani mwenye hadhi yake.
“Panda kwenye gari,” aliniambia kisha nikafanya kama vile alivyosema, nilipopanda tukaweza kuondoka huku nikionekana kuwa mpole sana.
Hatimaye gari lilifunga breki mbele ya jengo moja kubwa ambalo nilipolizama kwa haraka niliweza kufahamu kuwa pale ni wapi. Kulikuwepo na bango moja kubwa lililokuwa limeandikwa kwa maandishi makubwa ambayo yalisomeka ‘KISOKA FILM PRODUCTION’ maneno hayo hayakuweza kunipa wakati mgumu wa kuweza kugundua kuwa pale nilikuwa sehemu gani. Nilifahamu na nilikuwa nikitabasamu muda wote.
“Karibu sana Dickson,” alinikaribisha Irine mara baada ya kuingia ofisini kwake.
“Asante sana.”
“Hivi ulisema unaishi wapi?”
“Tandale.”
“Anha! Maana nilisahau kabisa.”
“Una mambo sana.”
“Yani we acha tu! kichwa changu kinafikiria mambo mengi mpaka basi.”
“Itabidi upunguze.”
“Oooh! Umekumbuka kuja na hadithi?”
“Ndiyo nimekuja nayo.”
“Kwanza hongera unajitahidi sana kuandika.”
“Asante hata wewe nikupongeze kwa uchezaji mzuri wa filamu zako.”
“Hahahaha! asante.”
“Unaweza kuziteka hisia za mtazamaji pindi anapokutizama.”
“Mmmh! Kweli.”
“Sijawahi kumuongopea mtu wewe niamini.”
“Sawa nakuamini.”
“Hadithi ndiyo umesema inaitwa?”
“BADO UNAISHI MOYONI MWANGU.”
“Kwanini BADO UNAISHI MOYONI MWANGU na isiwe jina lingine?”
“Nadhani kisa nilichokizungumzia humo ndiyo kimenifanya niweze kuiita jina hilo.”
“Inaonekana itakuwa nzuri sana.”
“Ndiyo ni nzuri kwa ujumla,” nilimwambia huku nikimtazama usoni, alionekana kunivutia kila kiungo cha mwili wake. Si kwa macho yake, uso wake, rangi yake, midomo yake, dimpozi zake, kifua pamoja na umbo lake vyote hivi viliweza kunifanya nianze kuwaza ngono.
****
Irine aliweza kunikutanisha na baadhi ya waandaaji wa filamu aliyokuwa amewaajiri katika kampuni yake, alikuwa amedhamiria kufanya kazi na mimi kwa moyo mmoja bila kujali umaarufu aliyokuwa nao.
“Itabidi unikopie hii kazi yako kwenye hii flash ili baadae niipitie halafu nijue kama itafaa kufanyiwa filamu,” aliniambia Christopher Director mkubwa wa na Irine.
“Sawa haina tatizo mkuu,” nilimjibu kisha nikaondoka zangu huku nikiwa nimechukua namba zake za simu.
****
“Kwani wewe uko wapi?”
“Mimi niko hapa kituoni Mori.”
“Utaweza kunisubiria nikufuate?”
“Uko mbali sana?”
“Hapana.”
“Uko wapi?”
“Shekilango nakuja hapo.”
“Sawa nakusubiri.”
“Sawa honey love you.”
“Love you two.”
Zilikuwa ni chatting kati yangu na Precious ambaye alikuwa ameniahidi kuwa alikuwa anakuja kunichukua. Haikuchukua dakika nyingi aliweza kufika, nikapanda kwenye gari lake, nikambusu kisha safari ikaanzia hapo.
“Kwani tunaenda wapi?”
“Wewe wasiwasi wako ni nini?”
“Hapana ila nimeuliza tu!”
“Usijali tukifika utajua,” alinijibu kisha sikutaka tena kuzungumza, niliamua kukaa kimya.
Safari yetu ilikwenda kuishia Mbezi Beach mbele ya nyumba moja ya kifahari sana, niliitazama nyumba hiyo katika macho ya matamanio, Ilionekana kuwa ni nyumba ya kisasa ambayo ilisheheni kila kitu cha kuvutia, kama ungepata bahati ya kuitazama hakika ungeyasahili maneno yangu.

Je, ni nini kitaendelea?
Precious amedhamiria nini kumpeleka Dick katika hiyo nyumba?”
Vipi kuhusu Irine na Evadia?”
Na Je, Precious atakuwa ameshika ujauzito?
Unahisi ni nini kitatokea?”
Tukutane Jumapili mahali hapahapa.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-37
Mtunzi:Juma Hiza

Age:18+

ILIPOISHIA....

Safari yetu ilikwenda kuishia Mbezi Beach mbele ya nyumba moja ya kifahari sana, niliitazama nyumba hiyo katika macho ya matamanio, Ilionekana kuwa ni nyumba ya kisasa ambayo ilisheheni kila kitu cha kuvutia, kama ungepata bahati ya kuitazama hakika ungeyasahili maneno yangu.

SONGA NAYO.....

“Hapa ni wapi?” nilimuuliza Precious kisha akatabasamu, hakunijibu lolote badala yake alipiga honi kuashiria kuwa alikuwa nje na baada ya dakika chache geti liliweza kufunguliwa na kijana mmoja ambaye kwa macho ya harakaharaka alionekana kuwa mlinzi.
Hatimaye tukaingia ndani ya nyumba ile ya kifahari kisha Precious akaenda moja kwa moja mpaka eneo maalumu la kuegesha gari, akaliegesha vyema kisha tukashuka.
Macho yangu yalikumbana na gari la kifahari aina ya BMW 545 yenye thamani ya shilingi milioni hamsini na sita lililokuwa limeegeshwa pembeni na pale ambapo Precious alikuwa ameegesha gari lake. Sio siri nilizidi kujionea maajabu tu! kwani mpaka kufikia wakati huo Precious hakuwa ameniambia lolote lile.
“Vipi mpenzi,” aliniambia Precious kisha akanisogelea na kunishika mkono, tukaingia ndani ya nyumba hiyo iliyokuwa imekamilika kila kitu ndani, hakukuwa na kasoro yoyote.
“Unaionaje hii nyumba?” aliniuliza swali nililoliona kuwa kama la kunikejeli kwani ukweli nyumba ilikuwa ikionekana kuwa nzuri hata bila kuulizwa lolote.
“Mbaya tu!” nilimjibu huku nikijifanya kama sielewi. Alicheka kisha akajizuia.
“Baby embu acha masihara ujue mimi nakuuliza kwa kumaanisha.”
“Kiukweli nyumba ni nzuri sana inaonekana kukamilika kwa kila kitu kasoro kitu kimoja tu!”
“Kitu gani?”
“Hakuna watu,” nilijibu kisha akacheka tena.
Alionekana kuwa na furaha sana, uso wake ulitawaliwa na tabasamu mwanana lililozidi kumfanya aonekane kuwa wa aina yake.
“Dick,” aliniita baada ya ukimya mfupi kutawala.
“Niambie malkia wangu,” nilimjibu huku nikimshika kiuno chake laini kilichogawanyika mithili ya mdudu nyigu.
“Asante sana kwa zawaidi uliyoweza kunipa katika maisha yangu, siwezi kukusahau.”
“Zawadi?”
“Ndiyo.”
“Zawadi gani?”
“Mimba.”
“Unasema?”
“Nina mimba yako Dick,” aliniambia kisha nikajifanya kama nimeshtushwa na taarifa hizo ambazo sikuzitegemea.
“Nini mbona umekuwa hivyo?”
“Hamna, siamini kama nimeweza kukupa ujauzito.”
“Amini Dick, wewe ndiyo mwanaume pekee ambaye umeweza kunibadilisha jina, naamini hivi karibuni na mimi nitakwenda kuitwa mama wa mwanao, nimebeba kiumbe chako Dick,” aliniambia.
“Ujue siamini kabisa.”
“Amini Dick nina kiumbe chako tumboni.”
“Dah!”
“Ila baby usijali unakumbuka nilikuahidi nini?”
“Nini?”
“Nilikuahidi vitu vingi sana ila kubwa ni kukununulia nyumba, usafiri pamoja na kukupa mtaji utakaoanzia katika biashara yako ya vitabu.”
“Ndiyo nakumbuka.”
“Basi hivi vyote unavyoviona mbele yako kuanzia sasa vipo chini yako,” aliniambia Precious maneno ambayo nilihisi wenda alikuwa katika utani, alikuwa akinitania lakini haikuwa hivyo bali kila ambacho alichokuwa akikizungumza alikuwa akikimaanisha.
“Ina maana ile BMW na hii nyumba unataka kuniambia vyote kuanzia sasa ni mali yangu?” nilimuuliza.
“Ndiyo baby,” alinijibu Precious huku akionekana kutojali lolote lile.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa mimi kumiliki nyumba nzuri, gari la kifahari na pia kukabidhiwa kiasi cha pesa ambacho nilikitumia kama mtaji wa kutoa vitabu vyangu. Niliamua kuhama Tandale na sasa maisha yangu yakahamia Mbezi Beach.
Sikutaka kufikiria lolote kuhusu mume wa Precious pamoja na taarifa zile za ujauzito. Nilichokuwa nakiangalia kwa wakati ule ni ule utajiri wa ghafla! niliyoweza kuupata katika maisha yangu, ulikuwa ni utajiri ambao kwa kweli kama ingetokea ukaniuliza niliupata katika njia zipi, jibu pekee ambalo ningeweza kukujibu ni kuwa nilitembea na mke wa mtu kisha akaweza kunihonga wala hakukuwa na njia nyingine. Siyasemi haya ili nikushinikize na wewe unayeyasoma maandishi haya uende ukafanye kama mimi nilivyofanya lahasha! isipokuwa ipo sababu ya msingi ya kukuandikia haya kwani naamini mwisho wa siku utaweza kujifunza kitu kupitia mimi Mr. Chombezo au ukipenda unaweza kuniita Dick Mapenzi. Majina haya ndiyo yaliyoweza kuniponza Dick mimi ambaye leo naishia kusimulia tu!.
****
Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kipekee sana kwangu, kwanza nakumbuka nilimtafuta Mick simuni kisha nikamuelezea kila kitu kichokuwa kimetokea, aliweza kunishangaa sana.
“Dick ujue una michezo hatari sana,” aliniambia.
“Kwanini unasema hivyo?”
“Unajisifia kabisa umempa mke wa mtu mimba halafu kakupa nyumba unafurahi kabisa.”
“Sasa wewe ulitaka ninune au? Kwanza yeye mwenyewe ndiyo kaniletea shobo mimi nifanye nini sasa?”
“Ndugu yangu unapotea.”
“Acha uzoba wewe hapa ni mjini na mjibu kuishi ni mipango hivi unafikiri kwa maisha haya yalivyo magumu halafu anatokea mtu anakupa pesa utaanzaje kuzikataa.”
“Dick mke wa mtu sumu.”
“Hayo ni maneno tu! siku hizi tunakula mpaka vya nyongeza.”
“Unajua unafanya masihara lakini ipo siku hivyo vitu vitakutokea puani.”
“Ndugu yangu sasa naona unafika mbali kama vipi baadae ngoja leo nitafute kahaba nilale naye huku maana tayari nimeshakuwa Don,” nilimwambia kisha nikakata simu.
****’
Kitendo cha kuhamia Mbezi Beach kilikwenda kuufungua ukurasa mpya hata katika upande wa wasichana niliyokuwa nikitembea nao, sikutaka kuendelea kutembea na wasichana kama akina Helena ambao walionekana kuwa na shida, niliamini kama ningeweza kuwa nao basi hakukuwa na kitu cha ziada ambacho kingeweza kubadilika sanasana ndiyo kwanza wangezidi kunipa mawazo ya kuwahudumia wakati mimi mwenyewe nilikuwa nikihudumiwa.
Nilianza kubadilika kimavazi, kila siku nilionekana kupendeza sana hata wale wasichana waliyokuwa wakiziona picha zangu Instagram nilizokuwa nimezipost huku nikiwa nimeegemea gari langu la BMW hakika ziliwachanganya sana.
“Mbona umehama bila kuniambia?” aliniuliza Evadia usiku mmoja nilipoamua kumpigia simu.
“Nisamehe mpenzi nilisahau kukuambia,” nilimjibu.
“Umehamia wapi?”
“Sasa hivi nimehamia Mbezi ila usijali kesho lazima nikuone na utakuja kupafahamu.”
“Sawa Mume wangu nitafurahi.”
“Ukitoa wewe hakuna mapenzi tena, wewe ndiyo maana ya mapenzi yangu.”
“Umeanza na vijimaneno vyako.”
“Huo ndiyo ukweli.”
“Halafu nimekumis baby.”
“Nimekumis pia.”
“Njoo basi sasa hivi mpenzi, nauhitaji ukaribu wako.”
“Nikija siunajua nini kitatokea?”
“Haya nakuja.”
“Njoo tu! babyyy nitakupa ondoa shakaa.”
“Hodi.”
“Karibu.”
“Asante, mbona sasa hujachojoa nguo?”
“Tayari baby.”
“Sawa, sogea basi.” “Tayari baby nipeee,” aliniambia kwa sauti ya kimahaba ambayo ilinifanya akili yangu ibadilike na kuanza kufikiria ngono na kila ambacho nilikuwa nikikizungumza kwa wakati huo hakikuwa na maana nyingine zaidi ya ngono.
Kilichoendelea kusikika kwa upande wa pili ni miguno pamoja na sauti za kimahaba alizokuwa akizitoa Evadia, alikuwa akilalamika kana kwamba nilikuwa nikifanya naye mapenzi kumbe yalikuwa ni mapenzi yaliyofanyika simuni. Kutokana na uhodari wangu katika kucheza na michezo hii nilizidi kumpagawisha kwa kumpa muwashawasha uliyozidi kumuacha mpaka akawa analia kwa kuomba utamu wangu.
“Ooooooh, babbyyyyyyy nipe nipeeee ooooohhh chukuaaaa yoteeee yakoooo aaaasssshhhh ooooohhh aaaaaaah,” alitokwa na miguno wakati huo nilikuwa nikifanya naye mapenzi kwenye simu.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane Jumatano mahali hapahapa.

#Like nyingi, komenti yako pamoja na Share nyingi ndizo zitafanya Chombezo hili liweze kufika mbali.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-38
Mtunzi:Juma Hiza

Age:18+

ILIPOISHIA.....

Kilichoendelea kusikika kwa upande wa pili ni miguno pamoja na sauti za kimahaba alizokuwa akizitoa Evadia, alikuwa akilalamika kana kwamba nilikuwa nikifanya naye mapenzi kumbe yalikuwa ni mapenzi yaliyofanyika simuni. Kutokana na uhodari wangu katika kucheza na michezo hii nilizidi kumpagawisha kwa kumpa muwashawasha uliyozidi kumuacha mpaka akawa analia kwa kuomba utamu wangu.
“Ooooooh, babbyyyyyyy nipe nipeeee ooooohhh chukuaaaa yoteeee yakoooo aaaasssshhhh ooooohhh aaaaaaah,” alitokwa na miguno wakati huo nilikuwa nikifanya naye mapenzi kwenye simu.

SONGA NAYO......

Sauti pamoja na miguno ile ya kimapenzi aliyokuwa akiitoa haikukoma, aliendelea kulalamika huku akidai kuwa alikuwa akiumia. Nilifahamu fika ni maumivu gani aliyokuwa akiyapata, yalikuwa ni maumivu ya utamu aliyokuwa akiutamani kupata kutoka kwangu.
“Dick naumiaaaaaa,” aliniambia kwa sauti la kulalamika. Sikutaka kumjibu lolote, niliendelea na mchezo wangu wa kumpandisha nyege.
“Aaaahhh Dick acha bhnaaa mwenzio naumiaaaa,” alizidi kulalamika.
Nakumbuka siku hiyo niliutumia muda mwingi sana katika kufanya mapenzi na Evadia kwa njia ya simu, yalikuwa ni mapenzi fulani hivi ya kimzaha yaliyotukutanisha kihisia na kuhisi kama tulikuwa tukifanya mapenzi kiuhalisi. Naam! kama uliwahi kuucheza mchezo huu hakika utakuwa umefahamu ni nini ninachokimaanisha.
Mchezo huo uliniweka katika wakati mgumu sana, hali ya mtarimbo wangu haikuwa shwari, alikuwa katika midadi ya kuukamata utamu wa mwanadada Evadia kwa wakati huo.
“Dick…”
“Niambie Mpenzi wangu.”
“Umefanya mpaka nimechafua nguo.”
“Hahaha! Pole.”
“Sitaki.”
“Hutaki nini sasa kwani hujafurahia tendo?”
“Nimefurahia.”
“Sasa mbona usemi asante?”
“Asante Dick.”
“Mmh! Mpaka nikuombe?”
“Hapana Darling.”
“Nikuulize?”
“Ndiyo niulize.”
“Unanipenda?”
“Ndiyo nakupenda, mbona unaniuliza swali hilo?”
“Nilitaka kufahamu.”
“Dick nakupenda sana wala hakuna Mwanaume ambaye nimewahi kumpenda zaidi yako hata Ex-boyfriend wangu sijawahi kumpenda kiasi hiki.”
“Nitaamini vipi kuwa unanipenda?”
“Baby kitendo cha kukutambulisha kwa wazazi wangu nahisi ni sababu tosha ya wewe kuniamini.”
“Unaonekana kuwa mwanamke ambaye niliwahi kumuona sehemu.”
“Mwanamke yupi na ni sehemu gani ulimuona?”
“Nimekuwa nikiiamini ndoto kwa muda mrefu, niliishi maisha hayo ya kumuota msichana mrembo ambaye niliamini huyo ndiyo mwanamke wa maisha yangu, sikuwa nafahamu anafananaje sura yake, umbo lake au hata tabia yake lakini kupitia wewe nimeweza kuiamini ile ndoto. Wewe ndiyo huyo mwanamke niliyekuwa namuota kila siku.”
“Nafurahi kusikia hivyo mpenzi wangu, kila siku namuomba Mungu atujaalie kila tulilolipanga liweze kutimia.”
“Hata mimi nafanya hivyo,” nilimwambia Evadia maneno ambayo kuna kipindi nafsi yangu ilikuwa inanisuta. Sikuwa nikimaanisha kila neno nililokuwa nikilisema, kuna wakati nilikuwa nikizungumza kuwa kama sehemu moja wapo ya sanaa ya utunzi niliyokuwa nao. Maneno yangu mazuri, matamu yenye kumsisimua msichana pindi anisikiapo yaliweza kumuingia vyema Evadia.
Alikuwa akiniamini kupitiliza na hili ndiyo kosa kubwa ambalo alilokuwa amelifanya bila kujua. Nilikuwa nikizungumza na wanawake wengi sana, si kwa kuzungumza nao simuni tu lahasha! bali wengine nilikuwa nikichat nao muda mrefu kitendo ambacho kilinifanya niwe mvivu kujibu jumbe za Evadia pamoja na kupokea simu zake kwa wakati, hilo lilikuwa ni tatizo kubwa ambalo liliweza kuzua ugomvi kati yetu lakini nilipojaribu kumpigia simu yake na kuitumia fursa hiyo kumdanganya kwa mpangilio wa maneno yangu mazuri hakika aliweza kunielewa na kunisamehe.
****
Siku iliyofuata niliweza kumleta Evadia katika nyumba niliyokuwa nimehamia maeneo ya Mbezi Beach. Alionekana kushangaa kila kitu kilichokuwa mbele yake. Nilifahamu siku hiyo ningeweza kukumbana na maswali lukuki kutoka kwa Evadia ambaye asingeweza kuamini kirahisi mabadiliko yangu ya kimaisha hasa katika kipindi kama kile.
“Hii ni nyumba yako?” aliniuliza wakati nilipokuwa nikimzungusha sehemu mbalimbali za ile nyumba.
“Ndiyo,” nilimjibu huku nikitabasamu kumuonyesha kuwa hakukuwa na tatizo lolote bali kila kitu alichokuwa akikishuhudia kilikuwa ni mali yangu.
“Na lile gari je?”
“Baby vyote ni mali yangu.”
“Umewezaje kumiliki vitu hivi Dick, umefanya kazi gani mpaka uweze kumiliki mali zote hizi.”
“Evadia mjini ni mipango, kila mtu unayemuona anaishi katika mji huu basi fahamu kuwa anaishi kwa mipango. Nilifahamu kuwa utaweza kushangaa hasa kwa mali hizi ambazo nimeweza kuzimiliki lakini nikuondoe wasiwasi mimi ni mtafutaji na siku zote ulizokuwa unaniona nyuma ya pazia kulikuwa kuna mishe nazifanya na ndizo zimeweza kuzaa matunda haya.”
“Mishe! Mishe gani hizo?”
“Baby mbona kama huniamini?”
“Lazima niingiwe na hofu ujue mimi nakufahamu sana.”
“Hata kama lakini ufahamu mimi ni mwanaume na sifa kubwa ya mwanaume ni kupambana na wala si kula kama wengi wanavyoamini.”
“Umefanya kazi gani?”
“Kazi nyingi tu! ila nakumbuka kitu kilichonisaidia, nilikuwa nikiwekeza sana pesa yangu katika vitu vya msingi nah ii ndiyo siri kubwa iliyoweza kuniletea mafanikio haya unayoyaona.”
“Mmh! Dick kweli?”
“Ndiyo.”
“Hakuna chochote unachonificha?”
“Hakuna,” nilimjibu.
Uwongo ndiyo uliyokuwa umechukua nafasi kubwa katika maisha yangu, sikuwa naogopa lolote lile hasa katika uwongo niliyokuwa nikidanganya, wanawake wengi waliweza kuniamini na kunikabidhi dhamana ya maisha yao. Miongoni mwa hao wanawake Evadia alikuwa ni mmoja wao. Alizidi kuniamini sana hasa baada ya kila kitu alichokuwa akikihisi vibaya, nilipoweza kumuelezea kwa maneno yangu ya uwongo aliweza kunielewa.
Wakati ule nilipokuwa na Evadia mule ndani, simu yangu iliita, nilipoitoa mfukoni na kuitazama nilikutana na jina la Precious. Sikutaka kupokea niliamua kuiacha iite mpaka pale ilipoweza kukata yenyewe.
“Mbona hupokei simu?” aliniuliza Evadia.
“Ah! Achana naye.”
“Ni nani kwani?”
“Mjinga mmoja hivi anasumbua sana.”
“Mwanaume au mwanamke.”
“Mwanaume.”
“Kwani anasemaje?”
“Tangu jana ananitumia meseji zake, ananiambia anataka nimsaidie kumuandikia hadithi yani ni msumbufu.”
“Sawa mpenzi wangu,” alinijibu Evadia kisha hapo hapo nikambeba na kumpeleka chumbani. Kilichoendelea humo ni kufanya mapenzi tu! nilihakikisha namkuna kila sehemu vilivyo ili azidi kunikumbuka kila siku za maisha yake.
****
Hatimaye ile hadithi yangu ya BADO UNAISHI MOYONI MWANGU iliweza kuhakikiwa na wahariri wa bodi ya filamu pamoja na waandaji wa filamu kwa ujumla.
Ilikuwa ni moja kati ya Hadithi nzuri ambayo waliipenda sana. Irine hakuwa mbali katika hilo alihakikisha kila kitu kinakwenda sawa na baada ya wiki moja kupita kazi ya kushoot filamu hiyo ilikuwa tayari imeshaanza hapa ilikuwa ni baada ya kutafuta Cast za wasanii ambao wangeweza kushiriki katika filamu hiyo ambayo mhusika mkuu alikuwa ni Irine Kisoka.
Nilimtazama Irine kama mhusika mkuu katika filamu hiyo ya BADO UNAISHI MOYONI MWANGU na kwa jinsi ambavyo alikuwa akiigiza, niliamini fika ilikuwa ni filamu ambayo ingeweza kufanya vizuri sana hasa katika upande wa soko zima la filamu nchini Tanzania.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane Kesho mahali hapahapa.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-39
Mtunzi:Juma Hiza

Age:18+

ILIPOISHIA.....

Nilimtazama Irine kama mhusika mkuu katika filamu hiyo ya BADO UNAISHI MOYONI MWANGU na kwa jinsi ambavyo alikuwa akiigiza, niliamini fika ilikuwa ni filamu ambayo ingeweza kufanya vizuri sana hasa katika upande wa soko zima la filamu nchini Tanzania.

SONGA NAYO.......

“Vipi kuhusu mumeo?”
“Amefanyaje?”
“Amesemaje kuhusu huu ujauzito?”
“Hajasema kitu halafu ameamini kabisa kuwa huu ujauzito ni wa kwake.”
“Kivipi?”
“Ameamini tu!”
“Hivi siku akigundua kuwa unamchezea mchezo huu mchafu unafikiri itakuwaje?”
“Dick mbona hujiamini yani unaogopa utadhani umekuwa mtoto wa kike.”
“Hayo umesema wewe ila mimi nimekuuliza.”
“Hawezi kufanya lolote bhana embu niamini basi.”
Yalikuwa ni mazungumzo kati yangu na Precious, nilionekana kuwa muoga sana hasa baada ya kuanza kuwaza kuhusu mume wake. Niliwaza siku ambayo ingetokea mume wake akagundua kuwa mimi ndiye nilikuwa sababu ya yote yale pamoja na ukatili ambao angeweza kunifanyia.
Nilikumbuka kesi na matukio mbalimbali ambayo nimewahi kuyashuhudia na jinsi ambavyo mtu akifumaniwa na mke wa mtu kitendo anachofanyiwa. Hilo lilizidi kuniogopesha sana.
“Embu acha kuogopa uko na mimi hakuna kitakachoharibika,” aliniambia Precious tulipokuwa kitandani amejilaza mapajani mwangu akijaribu kudeka deko la kimapenzi. Wakati huo nje jua kali la saa saba lilikuwa likiangaza.
“Lazima niogope ujue mimi nawaza mambo mengi sana,” nilimwambia huku nikilipapasa tumbo lake.
“Mambo gani hayo niambie usinifiche tafadhali.”
“Ni kuhusu mume wako.”
“Kafanyaje tena?”
“Wewe hunipendi.”
“Sikupendi na nini mpenzi wangu.”
“Unataka mumeo aniue.”
“Hawezi kukuua bhana embu acha kuwa na dhana hizo za kijinga.”
“Kwahiyo hapa nazungumza ujinga.”
“Sio hivyo mpenzi wangu sasa wewe kila wakati unaongelea kitu hichohicho tu! mimi nimekuambia jiamini hakuna chochote kitakachotokea.”
“Sawa,” nilimjibu.
Precious alizidi kuniaminisha kuwa hakukuwa na kitu chochote ambacho kingeweza kutokea. Ule wasiwasi wangu uliyoanza kuniingia taratibu ulianza kupotea, nilizidi kuyaamini maneno ya Precious na hivyo sikuwa na hofu yoyote.
“Wewe kweli ni kidume,” aliniambia Precious.
“Kwanini?” nilimuuliza.
“Siamini kama leo nina ujauzito kwakweli yani Dick nitakupenda mpaka mwisho wa maisha yangu,” aliniambia.
“Na mumeo je?”
“Mume wangu wa nini sasa?” aliniuliza kwa ghadhabu kisha akanuna, nikapata kazi mpya ya kumbembeleza mpaka pale alipoamua kutulia. Hakupenda kulisikia jina la mume wake nikilitaja mbele yake.
“Kwanini unakuwa hivyo lakini?”
“Nisamehe mpenzi.”
“Mimi sipendi.”
“Najua mpenzi wangu nisamehe.”
“Niahidi kwanza.”
“Nikuahidi nini?”
“Kuwa hautarudia tena kumtajataja.”
“Ndiyo sitarudia tena kumtaja.”
“Nakupenda sana Dick wangu.”
“Nakupenda pia Mahabuba.”
“Nafurahi sana kusikia hivyo.”
“ Binafsi najivunia kukupata katika maisha yangu, umeyabadilisha maisha yangu Precious.”
“Usijali nitazidi kuyabadilisha na kila kitu ambacho unakitaka niambie nitakutimizia, mimi nipo kwa ajili yako.”
“Sawa mpenzi wangu,” nilimwambia.
****
Baada ya kupita miezi kadhaa hatimaye filamu ya BADO UNAISHI MOYONI MWANGU iliweza kukamilika na kuingia sokoni, ilikuwa ni moja kati ya filamu bora zilizokuwa zikipendwa sana hata katika upande wa mauzo iliweza kuvunja rekodi. Hakukuwa na filamu nyingine iliyokuwa ikitazamwa tena, kila mtu alibaki akitazama BADO UNAISHI MOYONI MWANGU.
Kwa kweli sikutaka kuamini kabisa kama filamu hiyo ingeweza kunifungulia milango ya mafanikio kila kukicha. Nilikuwa nikipokea simu mbalimbali kwa ajili ya kufanya kazi na makampuni makubwa yaliyoniamini kuutambua uwezo wangu katika kuandika.
Jina langu la Dick Mapenzi sasa lilizidi kuwa jina kubwa mno, kila mtu alianza kunifahamu, hakukuwa na mtu ambaye aliitaja filamu ya BADO UNAISHI MOYONI MWANGU bila kulitaja jina langu kama mwandishi.
Wasichana nao hawakuisha kujipendekeza kwangu, kila msichana ambaye alijipendekeza kwa kweli sikuacha kufanya naye mapenzi, huo ndiyo ulikuwa ugonjwa wangu haswaa!
Niliweza kutengeneza pesa nzuri sana kupitia filamu hiyo, faida nzima niliyoweza kuipata niliamua kwenda kuwekeza katika biashara mbalimbali. Sikuwa na shida yoyote kama ni nyumba nzuri nilikuwa nayo, gari la kifahamu tena BMW nilikuwa nalo, kuhusu pesa wala haikuwa ni moja ya tatizo kwangu, Precious alikuwa akinihudumia kwa kila kitu.
Sikutaka mafanikio yangu pamoja na umaarufu wangu uishie kwenye filamu tu! pamoja na kupokea sifa mbalimbali kutoka kwa watu waliyokuwa wakinifahamu. Nilitamani sana kuwa mtu maarufu na umaarufu ambao nilikuwa nikiutaka ni ule wa kuandikwa kila siku katika magazeti pamoja na kuandikwa sana katika mitandao ya kijamii. Hakukuwa na wazo lingine lililonijia kichwani mwangu kwa wakati huo zaidi ya kuamua kutembea na Irine Kisoka miongoni kati ya waigizaji ambao walishiriki kwa asilimia kubwa katika kuhakikisha lengo langu la kutoa filamu linatimia na kweli liliweza kutimia.
Alikuwa ni muigizaji aliyeongoza kwa kuandikwa vibaya katika magazeti ya udaku pamoja na mitandao ya kijamii, hii ilitokana na uzuri pamoja na umaarufu aliyokuwa nao.
Nilijisahaulisha kuhusu urafiki aliyokuwa nao na Evadia. Hata kipindi kile ambacho Evadia alikuwa akihangaika katika kuhakikisha nafanikiwa vyote nilijisahaulisha na sasa kitu nilichokuwa nimepanga ni kutoka kimapenzi na Irine Kisoka huku lengo langu likiwa ni kutafuta skendo itakayonifanya niwe maarufu zaidi mpaka nianze kuandikwa katika magazeti ya udaku na mitandao ya kijamii.

Je, ni nini kitaendelea?
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-40
Mtunzi:Juma Hiza
Age:18+

ILIPOISHIA.....

Nilijisahaulisha kuhusu urafiki aliyokuwa nao na Evadia. Hata kipindi kile ambacho Evadia alikuwa akihangaika katika kuhakikisha nafanikiwa vyote nilijisahaulisha na sasa kitu nilichokuwa nimepanga ni kutoka kimapenzi na Irine Kisoka huku lengo langu likiwa ni kutafuta skendo itakayonifanya niwe maarufu zaidi mpaka nianze kuandikwa katika magazeti ya udaku na mitandao ya kijamii.

SONGA NAYO......

“Hongera kwa kazi nzuri uliyoifanya.”
“Asante ila nitakuwa mchoyo wa fadhila kama nisipokushukuru wewe.”
“Mbona sioni cha kunishukuru hapo wakati kila kitu umehusika.”
“Jina lako na umaarufu wako ndiyo vimefanya nikaweza kulitimiza hili kama si wewe nadhani nisingefika hapa.”
“Kweli?”
“Ndiyo.”
Yalikuwa ni mazungumzo kati yangu na Irine tulipokuwa katika moja ya hoteli kubwa hapa mjini majira ya mchana, tulikuwa tukipata chakula cha mchana lakini pia ilikuwa ni katika harakati za kupongezana baada ya filamu tuliyoitoa kufanya vizuri kimauzo.
“Imekuwa ni filamu ya kipekee sana ujue siamini kama imeweza kufanya vizuri,” aliniambia Irine.
“Hata mimi siamini,” nilimwambia.
“Unajua sana kuandika hadithi za kimapenzi.”
“Hahahaha! mbona hata wewe unajua kuigiza filamu za kimapenzi.”
“Nikwambie kitu.”
“Niambie.”
“Hii imekuwa ni filamu ya kitofauti sana kwangu na filamu zote ambazo nimewahi kuzifanya.”
“Kwanini?”
“Hadithi uliyoiandika ni ya kipekee sana yani kwa kipaji ulichonacho hukustahili kuwa hapa,” aliniambia Irine maneno yaliyonifanya nitoe tabasamu.
“Mbona unacheka?”
“Umenifurahisha.”
“Huo ndiyo ukweli.”
“Kila siku huwa najiambia mwenyewe kuwa kama nisingebahatika kukutana na wewe sijui ni lini ningeweza kuitimiza ndoto yangu.”
“Hapana usiseme hivyo ila unachotakiwa ni kumshukuru Mungu halafu pia nadhani usimsahau Evadia maana nadhani yeye ndiye amekuwa msaada mkubwa sana kwako.”
Nilionekana kuwa mwenye furaha wakati wote wa mazungumzo lakini alipofikia kulitaja jina la Evadia na kuniambia kuwa nilitakiwa kumshukuru kiukweli nilibadilika, sikutaka kulisikia jina la Evadia mahali pale.
Mabadiliko yangu kwa wakati ule yalimshangaza Irine, aliponiangalia usoni alionyesha kuwa na maswali juu ya hali yangu ile, hilo nililifahamu nikajaribu kuwahi kuliunda tabasamu bandia ili niweze kumficha hali niliyokuwa nayo lakini haikuwa kama nilivyowaza aliwahi kuniuliza na hapo nikawahi kutafuta jibu la kumzugia.
“Nini mbona umebadilika ghafla!” aliniuliza Irine, wakati huo macho yangu yalikuwa yakikitazama kifua chake ambacho alikisitiri kwa vazi la wazi lililojaribu kukidhihaki na niliitumia nafasi hiyo kumtazama kwa macho ya uwizi.
“Hapana hakuna kitu,” nilimjibu kisha nikajifanya kuwa bize na sahani ya chakula ambacho nilikuwa nikiendelea kukila.
Kila nilipokuwa nikimtazama Irine na kwa jinsi alivyokuwa ameumbika kiukweli nilizidi kumtamani sana, kuna muda nilitamani kumwambia lakini niliogopa, hapa ni baada ya kuzikumbuka zile skendo za kutembea na wanaume tofautitofauti, nilibaki nikimtazama na kula kwa macho ya uchu.
Kila siku alikuwa akiandikwa vibaya magazetini, alikuwa akiandikwa kuwa alikuwa akitembea na wanaume tofautitofauti ambao wengi wao walikuwa ni watu wenye wadhifa fulani, hilo lilizidi kuniogopesha.
“Kuna kitu unataka kuniambia?” aliniuliza.
“Hapana,” nilimjibu huku nikiweweseka na jibu langu, nilikuwa nimeshapagawa.
“Niambie usiogope au bado unahisi hujanizoea?” aliniuliza huku akiendelea kula chakula katika mpangilio uliyozidi kupendeza, hakuonekana kuwa na makuu hata kidogo na kila nilipokuwa nikiendelea kumtazama mapigo ya moyo wangu yalizidi kwenda kwa kasi kuhofia uwepo wa Irine. Kwa wakati huo nilikuwa tayari nimeshamsahau Evadia na Precious mwanamke ambaye alikuwa akinihudumia kwa kila kitu.
Nilichoamua kufanya kwa wakati huo ni kuchukua maamuzi, nikayapanga maneno yangu vyema halafu neno moja nikaliunganisha na lingine kisha nikatiririka katika kumpangilia vina, nakumbuka kuna baadhi ya maneno nilikuwa nikiyatoa katika dayaloji ya machombezo yangu ambayo niliamini yangeweza kumvutia kiasi kwamba akawahi kunikubalia na huo ndiyo ungekuwa mwanzo wa umaarufu wa kuandikwa magazetini na kwenye mitandao ya kijamii.
“Hapana Irine unajua kuna vitu vinaniweka katika wakati wa mawazo sana.”
“Vitu gani hivyo?”
“Uzuri wako,” nilimwambia kisha akatabasamu.
“Unajua unavituko Dick sasa uzuri wangu umefanyaje?”
“Irine wewe ni mwanamke mzuri sana una kila sifa za kumvutia mwanaume yoyote yule, ujue mpaka sasa hivi siamini kama zile habari unazoandikwa magazetini ni za kweli au?”
“Dick unajua mimi ni staa na kama unajua maisha yetu sisi mastaa kuchafuliwa na kuandikwa kila aina ya mabaya mitandaoni, magazetini ni sehemu moja wapo ya maisha yetu.”
“Ina maana unataka kuniambia hakuna ukweli wowote kuhusu ile habari niliyoisikia?”
“Habari gani?”
“Kuhusu unatembea na kigogo.”
“Hapana hazina ukweli wowote.”
“Kuna kitu nataka kukuambia ila nahisi nafsi inasita.”
“Kitu gani niambie usiogope.”
“Irine sijui kama utaweza kukubali.”
“Kwanini nisikubali wewe niambie kuwa huru.”
“Irine nakupenda,” nilimwambia.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane Kesho mahali hapahapa.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-41
Mtunzi:Juma Hiza
Age:18+

ILIPOISHIA.....

“Kuna kitu nataka kukuambia ila nahisi nafsi inasita.”
“Kitu gani niambie usiogope.”
“Irine sijui kama utaweza kukubali.”
“Kwanini nisikubali wewe niambie kuwa huru.”
“Irine nakupenda,” nilimwambia.

SONGA NAYO......

“Unanipenda?” aliniuliza swali nililolitegemea kwa wakati ule, sikutaka kung’atang’ata maneno, nikaanza kumchombezo.
“Ndiyo nakupenda sana Irine wala siwezi kukuficha hilo,” nilimwambia.
“Unanipenda kwasababu mimi ni maarufu au?”
“Nakupenda jinsi ulivyo wala sijakupendea huo umaarufu wako.”
“Nitaamini vipi hayo unayoyasema kuwa ni kweli?”
“Amini tu! ila labda nikuulize swali?”
“Niulize?”
“Hivi unaweza kumuamini daktari akikuambia kuwa mgonjwa wako anasumbuliwa na ugonjwa fulani?”
“Ndiyo naweza kumuamini.”
“Kwanini?”
“Kwasababu yeye ni daktari na ni kazi yake.”
“Kwanini hutaki kuniamini mimi shuhuda wa hisia zangu.”
“Dick siwezi kukuamini kirahisi hivyo.”
“Kwani uko na mtu?”
“Ofcourse nilikuwa naye ila kwa sasa tumeachana.”
“Ni nani huyo au ni…”
“Huyo huyo.”
“Nani sasa?”
“Juma Hiza.”
“Unaweza kuniambia kwanini mliachana?”
“Unajua katika mapenzi hasa kwa sisi mastaa kuna vitu vingi sana huwa vinatokea ila naweza kusema ilifikia wakati kila mapenzi hayakutakiwa yaendelee.”
“Kwani bado unampenda?”
“Sidhani kama kuna ukweli katika hilo na kama ningekuwa nampenda ungetuona tuko pamoja.”
“Nini kilitokea kati yenu?”
“Hee! Dick mbona maswali mengi kama mwandishi wa habari.”
“Inamaana umesahau kuwa mimi ni mwandishi wa hadithi?”
“Sijasahau.”
“Lakini kumbuka kiu yangu ni kutaka kufahamu ukweli kuhusu wewe.”
“Ukweli gani ambao unataka kuufahamu?”
“Ukweli kuhusu mapenzi yako.”
“Nafikiri ukweli wangu ni ndiyo huo na kuhusu kutoka kimapenzi katika maisha yangu nimewahi kutembea na mwanaume mmoja ambaye ni huyo Juma Hiza na baada ya hapo sijawahi kujihusisha na mapenzi na mwanaume mwingine.”
“Kweli?”
“Ndiyo sioni sababu ya kukudanganya Dick na kama kiu yako ni kutaka kuufahamu ukweli nadhani tayari umeshafahamu.”
“Na yale magazeti yanayoandika habari kuwa unatembea na wanaume tofautitofauti vipi?”
“Dick mimi ni staa na mambo kama hayo ya kuandikwa vibaya ni kawaida.”
“Asante kwa kuwa mkweli kwangu hata hivyo najivunia kukufahamu, unaonekana kuwa tofauti na wanawake wengine.”
“Asante Dick.”
“Usijali.”
“Ila kuna kitu Dick nataka kukuuliza.”
“Kitu gani?”
“Samahani lakini kwa kukuuliza swali hili ila inanibidi nikuulize.”
“Bila samahani niulize tu.”
“Hivi katika maisha yako umewahi kutoka na wanawake wangapi?”
“Nimetembea na mwanamke mmoja tu na tena aliwahi kuniumiza.”
“Kivipi?”
“Sikuwa na pesa hivyo wenye pesa walinipiku.”
“Pole sana.”
“Nishapoa na maumivu nimeshaanza kuyasahau.”
“Unaweza kuniambia ulimpenda kiasi gani?”
“Kwa kweli naweza kusema nilimpenda mithili ya nafsi na mwili kimoja kikikosekana basi hakuna maana ya uzima.”
“Una maneno Dick.”
“Hapana najitahidi kukuweka uwe karibu yangu lakini umekuwa kama ndege naona unakwea matawi tu.”
“Hahaha.”
“Niambie kitu kimoja.”
“Dick tatizo mimi sikuamini.”
“Kwanini huniamini?”
“Sijui hata.”
“Au bado unampenda Juma Hiza?”
“Hapana,” alinijibu Irine huku akiwa ameyaelekezea macho yake chini.
Kwa kweli ilikuwa ni kazi kubwa sana katika kumshawishi Irine msichana maarufu ili aweze kuwa na mimi kimapenzi, niliutumia ulimi wangu vyema katika kupangilia maneno, ndoano niliyokuwa nikiitupa baharini ya kumnasa samaki upendo kuna muda nilikata tamaa nikahisi kukosa kila kitu.
Juma Hiza huyu ndiye mwanaume aliyekiri kutoka naye kimapenzi, alikuwa ni miongoni kati ya wanamitindo wakubwa hapa nchini, kipindi cha nyuma mapenzi yao yalionekana kukolea, kila kona walikuwa wakisikika wao tu. Kwenye magazeti hakukuwa na habari nyingine zilizoandikwa zaidi ya mapenzi yao lakini mwisho wa siku penzi lao liliweza kufa.
Umaarufu wa mwanaume huyo pamoja na nguvu kubwa aliyokuwa nayo ilizidi kuniogopesha lakini nilijivika vazi la ujasiri kisha nikaendelea kuamini kumpata Irine. Nilitofautiana naye kwa vitu vingi sana hivyo sikutaka kukubali kuona mapungufu yoyote.
Niliendelea kubembeleza penzi kila siku, nililia kwa kudanganya, nikafanya kila niwezalo, visa vyote nikafanya mpaka Irine akaweza kunikubalia.
“Dick naomba unipende kweli, usicheze na hisia zangu, nimekukubalia ombi lako,” aliniambia Irine maneno yaliyonifanya nizidi kujiona gwuji wa mchezo huu hatari wa mapenzi na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa penzi jipya na yeye. Lilikuwa ni penzi lililonipa umaarufu ambao sikujua kama mwisho wa siku ungeweza kunipa funzo katika maisha yangu.

Je, ni nini kilitokea?
KwaninI Dick anasema umaarufu ulimpa funzo?
Ni funzo gani hilo?
Vipi kuhusu Evadia, Precious na ujauzito wake?
Hatma ya Chombezo hili ni nini?
Usikose sehemu ijayo mahali hapahapa.

#Like nyingi, komenti yako pamoja na Share nyingi ndizo zitafanya Chombezo hili liweze kufika mbali.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-42
Mtunzi:Juma Hiza
Age:18+

ILIPOISHIA.....

“Dick naomba unipende kweli, usicheze na hisia zangu, nimekukubalia ombi lako,” aliniambia Irine maneno yaliyonifanya nizidi kujiona gwiji wa mchezo huu hatari wa mapenzi na huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa penzi jipya na yeye. Lilikuwa ni penzi lililonipa umaarufu ambao sikujua kama mwisho wa siku ungeweza kunipa funzo katika maisha yangu.

SONGA NAYO.....

Nilianza kubadilika baada ya kufanikiwa kumpata Irine kimapenzi, nilijiojna kuwa zaidi ya kila kitu hata kwa upande wa mapenzi niliyokuwa nayo kwa Evadia nilianza kuyapunguza. Sikuwa tena ni mtu wa kumtafuta kama ilivyokuwa kawaida yangu, nilisubiri mpaka yeye ndiyo anianze kisha mimi niendelee.
Niliamua kufanya hivyo kwasababu nilijua wazi kuwa alikuwa akinipenda sana kuliko kitu chochote kile, alikuwa akinipenda kiasi kwamba kuna kipindi nilivyokuwa nikikaa kimya nilikuwa nikimuumiza.
“Kwanini siku hizi umebadilika hivyo?” aliniuliza siku moja alipokuja nyumbani kwangu ghafla! majira ya mchana, alikuwa ameshindwa kuvumilia ukimya ule ambao ulikuwa umetawala kati yetu siku zote hivyo aliamua kunifuata kwa lengo la kutaka kujua ni nini kilichokuwa kinanifanya mpaka nikae kimya kiasi kile, kwa akili ya harakaharaka alihisi kwa ujio wake ule angeweza labda kunifumania na mwanamke mwingine lakini haikuwa hivyo, alinikuta peke yangu tena kwa wakati huo nilikuwa sebuleni nikiandika hadithi kwenye laptop yangu.
“Nimefanyaje kwani?” nilimuuliza huku nikionekana kuwa bize na kuandika.
“ina maana hujanisikia au?” aliniuliza kwa sauti ya kunifokea kisha nikamtazama, alionekana kuwa na hasira kupitia uso wake aliyokuwa ameukunja mithili ya ngozi ya bibi kizee.
“Evadia kwani kosa langu ni lipi?” nilimuuliza.
“Kosa lako hulifahamu?” aliniuliza
“Kama ningelifahamu hivi ningekuuliza kweli?” nilimuuliza.
“Dick hivi kwanini siku hizi unanidharau sana,” aliniambia.
“Nakudharau kivipi mbona sikuelewi?” nilimuuliza.
Nilijikuta naanza kupoteza mapenzi kwa Evadia, kila nilipokuwa nikimtazama nilihisi kumchukia sana, kila sehemu ya kiungo cha mwili wake nilipokitazama sikuhisi msisimko wowote, nilikuwa nimeshamkinai japo sikumwelieza ukweli wa jambo hilo lakini kupitia visa na mikasa niliyokuwa namfanyia nilihisi wenda angeweza kung’amua lolote kuwa nilikuwa nikimchukia kupita maelezo na hivyo hakutakiwa tena kuishi na mimi. Nilijisahaulisha yale yote ambayoaliwahi kunifanyia katika maisha yangu, nilichokuwa nikikitazama kwa wakati huo ni mapenzi niliyokuwa nayo kati yangu na Irine.
“Dick siko hapa kwa ajili ya ugomvi na wewe,” aliniambia huku akinitazama kwa macho ya huba, niliamua kuamka pale kwenye kochi nilipokuwa nimekaa nikasimama kisha nikaanza kumogelea taratibu.
“Kwahiyo kama haupo hapa kwa ajili ya ugomvi umefuata nini sasa?” nilimuuliza swali ambalo niliamini lilikwenda kumuumiza moyoni mwake lakini sikutaka kujali lolote.
“Dick hivi kwanini unanichukia?” aliniuliza.
“Hicho ndiyo ulichokifuata?”
“Hapana ila nataka kufahamu kwanza.”
“Unataka kufahamu nini?”
“Dick au kisa nimekupa moyo wangu wa mapenzi unaumiliki na umegundua kuwa nakupenda kwa dhati ndiyo sababu unanifanyia haya?”
“Mbona sioni tatizo lolote huo ni wasiwasi wako.”
“Hapana Dick naomba uniambie.”
“Evadia unajua sikuelewi.”
“Dick nikuulize?”
“Ndiyo niulize lakini usiniulize maswali ya shule ya msingi.”
“Unanipenda?”
“Aaaggghh! Hivi hatuelewani au? Nimekuambia sitaki uniuliza maswali ya kitoto sasa hilo ni swali gani?”
“Naomba unijibu Dick.”
“Jibu unalo wewe mimi siwezi kukujibu.”
“Dick unasemaje?”
“Swali lingine?”
“Hivi kweli una mpango wa kufunga ndoa na mimi kweli?”
“Sahau kabisa kuhusu ndoa tena futa kabisa katika ufahamu wako. Kwasasa sipo na mipango hiyo.”
“Unasemaje?”
“Sina mpango wa kuoa kabisa kama unaona unaharaka na ndoa nenda kaolewe na wanaume wengine nimekukubalia sawa,” nilimwambia maneno ambayo yalimtoa machozi, hakutaka kuamini kama mimi ndiye ambaye nilikuwa nikimwambia maneno yale yaliyokuwa na mkuki wenye sumu kali uliyokwenda kukika katika kuta za moyo wake. Machozi yalikuwa yakimbubujika mfululizo.
“Hajafa mtu hapa tafadhali usiniletee uchuro sawa wewe kahaba,” nilimwambia kisha nikaanza kumtolea maneno machafu ambayo kiukweli mengine nafsi ilikuwa ikinisuta pindi nilipokuwa nikiyatamka, sikupanga kumfanyia yale ambayo nilikuwa nikimfanyia lakini nilijikuta tu! nikifanya bila kutarajia.
“Dick umenifanya niwachukie waandishi wote wa hadithi mitandaoni,” aliniambia Evadia huku akiyafuta macho yake.
“Sasa ulitumwa unipende embu chukua time ondokaaa.”
“Dick.”
“Sikutaki Evadia naomba tuachane.”
“Unasemaje?”
“Sikutakii.”
‘Dick hivi ni wewe kweli?”
“Sasa kama si mimi utakuwa unaongea na nani?”
“Nini kimekupata?”
“Natumia lugha adhimu kabisa ya Kiswahili, nimesema sikutaki na naomba uondoke nyumbani kwangu sawa,” nilimwambia kisha nikaanza kumfukuza bila huruma. Huo ndiyo ulikuwa mwanzo na mwisho wa penzi langu na Evadia, mwisho ambao niliweza kumpa maumivu ambayo hayakutarajia kuyapata.
****
Baada ya kupita miezi tisa hatimaye Precious aliweza kujifungua mtoto wa kiume, alikuwa ni mtoto ambaye aliyefanana na mimi kila kitu, Precious hakuacha kuniambia kuwa ilitakiwa kubaki kuwa siri kati yetu kwani mpaka kufikia wakati ule mume wake alikuwa bado hafahamu lolote lile, niliutumia udhaifu wa mume wake katika kujivika vazi la ubaba kwa mwanamke ambaye alikuwa ni mke wa mtu, naweza kusema katika hilo nilikuwa kipofu.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane Kesho mahali hapahapa.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-43
Mtunzi:Juma Hiza
Age:18+

ILIPOISHIA.....

Baada ya kupita miezi tisa hatimaye Precious aliweza kujifungua mtoto wa kiume, alikuwa ni mtoto ambaye aliyefanana na mimi kila kitu, Precious hakuacha kuniambia kuwa ilitakiwa kubaki kuwa siri kati yetu kwani mpaka kufikia wakati ule mume wake alikuwa bado hafahamu lolote lile, niliutumia udhaifu wa mume wake katika kujivika vazi la ubaba kwa mwanamke ambaye alikuwa ni mke wa mtu, naweza kusema katika hilo nilikuwa kipofu.

SONGA NAYO......

“Hongera mpenzi kwa kujifungua salama,” nilimwambia Precious wakati nilipokuwa nimempigia simu kwa lengo la kumpongeza. Wakati huo alikuwa bado yupo hospitalini.
“Asante yani Dick nina furaha,” aliniambia kwa sauti iliyoonyesha kufurahishwa.
“Najua furaha uliyonayo inaletwa na nini,” nilimwambia.
“Hatimaye nimekuzalia dume,” aliniambia.
“Tena Dume haswaa!”
“Dick asante kwa kunifanya nimekuwa mama sasa hivi,” aliniambia.
“Precious asante na mimi kwa kunifanya nimekuwa baba sasa hivi,” nilimwambia maneno ambayo nilimuiga kwa kubalidili neno baba. Alicheka sana.
“Mbona unacheka?” nilimuuliza huku na mimi nikicheka.
“Dick unanifanya nakuwa mwenye furaha sana,” aliniambia kwa sauti ya upole.
“Kwanini?” nilimuuliza.
“Sijui hata kwanini.”
“Nikwambie kwanini?”
“Ndiyo niambie.”
“Ni kwasababu moyo wangu na wako umeendana na laiti kama usingeendana nafikiri leo hii tusingekuwa pamoja.”
“Ni kweli mpenzi wangu yani sio siri nakupenda sana.”
“Hata mimi nakupenda pia?”
“Halafu nilitaka kusahau kitu.”
“Ulitaka kusahau nini tena malkia wangu?”
“Jina la mtoto?”
“Ina maana mpaka kufikia muda huu bado hana jina?”
“Ndiyo.”
“Ulikuwa unasubiri nini sasa?”
“Nilikuwa namsubiria baba yake ili aweze kumpa jina,” aliniambia kisha nikacheka.
“Usicheke embu mpe jina mwanangu tafadhali.”
“Tumuite Mzigo wa kuni Tabu Tupu.”
“Heee! Ndiyo jina gani hilo sitaki Dick, naomba mwanangu umpe jina zuri.”
“Ok basi tumuite Nickson.”
“Hahaha kwanini Nickson?”
“Ili isound sawasawa na jina la Baba yake yani Nickson Dickson.”
“Jamani nimelipenda bure.”
“Basi tumuite hivyo.”
“Unataka mwanao aje afanye kazi gani akiwa mkubwa?”
“Nataka nay eye aje kuwa mwandishi wa hadithi kama Baba yake.”
“Unataka na yeye atoe filamu?”
“Ndiyo wanasema maji yanafuata mkondo.”
“Nitafurahi kama ikiwa hivyo.”
“Usijali kila kitu kinawezekana.”
“Sawa Mume wangu,” aliniambia Precious.
Katika mazungumzo yetu sikutaka kabisa kugusia suala la mume wake wala kuhusu ndugu zake, nilifahamu fika kuwa walikuwa wakizifahamu habari zile za Precious, nilijitoa ufahamu na hakukuwa na mada nyingine ambayo nilitaka kuzungumza zaidi ya mada iliyonihusu mimi na mtoto.
Nilifanya hivyo ni katika harakati za kutomfanya Precious achukie, nilifahamu vyema kuwa alikuwa ni mwanamke wa aina gani, hakupenda pindi tulipokuwa katika mazungumzo neno au jina la mume wake alisikie, hilo nililifahamu na ndiyo sababu sikutaka kumuuliza lolote kuhusu mume wake wala ndugu zake. Nilijifanya kuwa jasiri nikiamini kuwa kwa kufanya hivyo nilikuwa natengeneza mazingira ya kusifiwa kuwa hakika nilikuwa kidume haswaa, furaha yangu ilikuwa nikuona nasifiwa kila wakati na Precious hasa katika kitendo kile cha kumfanya kuwa na mtoto.
****
“PENZI LA DICK MAPENZI LAMTEKA IRINE.”, “IRINE HAONI WALA HASIKII KWA PENZI LA DICK.” , “MWANDISHI WA HADITHI FACEBOOK DICK NA IRINE SASA MAPENZI HADHARANI.”
Hivi vilikuwa ni baadhi ya vichwa vya habari vya magazeti ya udaku ambayo nilikuwa nikiyapekuwa kupitia Application ya simu yangu kwa siku hiyo. Sikutaka kuamini kama kile nilichokuwa nikikisoma kilikuwa ni kweli au lah! macho yangu yalirudiarudia kuvisoma vichwa vile mara mbilimbili kana kwamba nilikuwa sioni vizuri.
Moyo wangu ulikuwa katika furaha isiyokuwa na kifani kwa siku hiyo, kama ilivyokuwa ndoto yangu ya hatimaye iliweza kutimia. Katika hali ya kushangaza siku hiyo Mick aliweza kunitafuta lakini alionekana kuwa tofauti kwa kila kitu.
“Niambie ndugu yangu,” nilimwambia huku nikiachia tabasamu la furaha.
“Naona ndoto yako imetimia,” aliniambia.
“Ndoto ipi tena?” nilimuuliza huku nikijifanya sifahamu lolote lile lililokuwa likiendelea.
“Umefanikiwa kuwa na Irine kimapenzi.”
“Irine?”
“Ina maana unajifanya hujui?”
“Hahaha! Ndugu yangu nilikwambia lakini kuwa lazima nimpate umeona?”
“Dick una hatari ujue.”
“Hatari ipi?”
“Umeanza kuandikwa kwenye magazeti, hivi unafikri Evadia au huyo mke wa mtu akiona itakuwaje?”
“Evadia yupi?”
“Evadia mpenzi wako.”
“Mbona nimeshaachana naye muda tu hata sijui habari zake.”
“Dick.”
“Naam.”
“Evadia umeachana naye?”
“Ndiyo.”
“Mbona mapema sana kwani amefanya nini?”
“Mimi ndiyo nimezingua.”
“Dick ipo siku maamuzi yako utayajutia.”
“Mick kila siku umekuwa ni mtu wa kunipa ngonjera tu hivi kwanini usifurahi rafiki yako tayari nimeshakuwa staa, muda wa kutengeneza pesa umefika halafu nina habari nzuri kwako.”
“Habari gani?”
“Precious amejifungua.”
“Dick unapotea.”
“Wewe baki na maneno yako mimi nazidi kutusua tu.”
“Dick hivi kwanini hutaki kubadilika?”
“Unataka niwe vipi sasa?”
“Dick embu badilika huo uhuni wala hautakupeleka popote.”
“Acha niendelee kutengeneza pesa.”
“Sawa ila utakuja kujuta,” aliniambia Mick.
Katika mafanikio na pesa ambazo nilikuwa nikizipata sikutaka ziwe zangu peke yangu, nilikuwa nikimpatia na Mick kiasi cha pesa ambacho niliamini kiliweza kumsaidia katika kutatua matatizo yaliyokuwa yakimsibu katika maisha yake.
****
“Asante Dick kwa kunipotezea muda wangu ila pia nashukuru kwa yote uliyonifanyia. Kumbe visa vyote vile ulivyokuwa unanifanyia shida yako ilikuwa utembee na Irine rafiki yangu. Asante sana Mungu akujaalie maisha marefu ya mapenzi yenu.”
Huo ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Evadia aliyokuwa amenitumia, nilipousoma nilitabasamu kisha nikaufuta, sikutaka kumjibu lolote.

Je, ni nini kitaendelea?
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-44
Mtunzi:Juma Hiza
Age:18+

ILIPOISHIA.....

“Asante Dick kwa kunipotezea muda wangu ila pia nashukuru kwa yote uliyonifanyia. Kumbe visa vyote vile ulivyokuwa unanifanyia shida yako ilikuwa utembee na Irine rafiki yangu. Asante sana Mungu akujaalie maisha marefu ya mapenzi yenu.”
Huo ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Evadia aliyokuwa amenitumia, nilipousoma nilitabasamu kisha nikaufuta, sikutaka kumjibu lolote.

SONGA NAYO.......

Nilikuwa nikimchukia Evadia kuliko kitu chochote kile, Laiti kama ingetokea ukaniuliza kuwa Evadia alinifanya nini na kwanini namchukia kwa kweli sitaweza kukupa jibu sahihi, hakuwahi kunifanyia kitu kibaya katika maisha yangu lakini nilijikuta namchukia tu bila sababu.
Tamaa ya pesa na umarufu ndiyo iliyoweza kuniponza mpaka nikamsahau Evadia pamoja na wema wake wote aliyoweza kunionyesha kwangu. Sikufikiria kuhusu Mama yake wala Baba yake ambao walitokea kunipenda sana na walitamani siku moja niweze kufunga ndoa na mtoto wao. Kila kitu nilichokuwa nikikifanya nilikifanya bila kufikiria mara mbilimbili, naweza kusema nilikurupuka kuchukua maamuzi.
****
“Dick mbona sielewei?” aliniuliza Precious kwa sauti iliyoonekana kugubwikwa na jazba. Wakati huo alikuwa amenipigia simu.
“Huelewi nini?” nilimuuliza huku kichwani mwangu nikianza kukumbuka kama kulikuwa kuna kosa lolote ambalo nilikuwa nimelifanya kwake, hakukuwa na kosa lolote, hali hiyo ilinifanya niingiwe na shauku ya kutaka kufahamu ni nini kilichokuwa kimetokea. Yalikuwa ni majira ya usiku.
“Hiki nilichokiona hivi ni kweli au macho yangu yananidanganya?” aliniuliza.
“Kitu gani?”
“Unatoka kimapenzi na Irine?”
“Umeona wapi?”
“Nimeona wapi wakati kwenye magazeti wameandika na kwenda mitandao naona zenu zinasambaa kila mtu anasema unatoka kimapenzi na yeye….Hivi Dick ni kitu gani umekosa kwangu eeeeh niambie ni nini umekikosa kwangu mpaka umeamua kutembea na Irine au kisa ni supa staa?” aliniuliza huku sauti yake ikiashiria kukosa uvumilivu katika hilo, alikuwa akilia.
“Embu tulia Mpenzi sawa acha kulia kwanza nikuambie kitu sawa,” nilimwambia huku nikianza kupanga maneno ya kumdanganya, Kila kitu alichokuwa akiniambia kilikuwa kina ukweli ndani yake.
“Uniambie nini Dick unahisi utakuwa ni kitu gani cha kunishawishi mimi mpaka nikakuelewa,” aliniambia huku akiendelea kulia kwa sauti ya kwikwi.
“Precious jaribu kunielewa basi mpenzi wangu,” nilimwambia kwa sauti ya upole.
“Unataka kuniambia nini, unataka kuniambia nini Dick?” aliniuliza kisha akawa kama mtu aliyenyamaza kulia, akawa ananisikiliza kwa umakini.
“Najua umejisikia vibaya baada ya kuona hivyo lakini unatakiwa kunisikiliza Darling kumbuka mimi ndiyo ninayeufahamu ukweli sasa usiponipa nafasi utakuwa hunitendei haki,” nilimwambia.
“Hivi ni nafasi gani ambayo unataka nikupe, Dick sema ukweli tu! ni nafasi ipi unataka nikupe? Nimekupa nyumba, nimekupa gari, pesa lakini umeona vyote havitosha bado unaamua kunisaliti,” aliniambia maneno ambayo kimoyomoyo yalinifanya nicheke, nilijichekesha kwasababu Precious alikuwa ni mke wa mtu na kwa maneno ambayo alikuwa akiyazungumza laiti kama mume wake angemsikia sio siri ule ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha yake, angeanguka chini kwa presha.
“Unajua mimi ni mwandishi na mpaka sasa tayari nimeshafanya kazi na mtu maarufu,” nilimwambia.
“Kwahiyo ukifanya kazi na mtu maarufu ndiyo?” aliniuliza kwa sauti ya kunikejeli.
“Najua unashindwa kunielewa kwasababu moyo wako tayari umeamini kile ambacho umekiona katika magazeti lakini kama utaweza kuuruhusu moyo wake walau uniamini japo kwa sekunde moja basi huwezi kunifanyia hiyo,” nilimwambia.
“Dick unajua ni jinsi gani ninavyokupenda sana nadhani unautumia udhaifu huo kuniadhibu kwakuwa unajua siwezi kwenda mbali,” aliniambia.
“Precious mbona sasa unakwenda mbali mimi nia yangu ni kukuelezea ukweli na si vinginevyo,” nilimwambia.
“Unataka kunielezea ukweli upi?” aliniuliza.
“Kuhusu hizo habari ulizozisoma katika magazeti pamoja na kwenye mitandao.”
“Kwahiyo hazina ukweli?”
“Precious unapokuwa maarufu lazima utakutana nanyo, skendo ni moja ya adui mkubwa sana kwa watu maarufu na mpaka unaona vitu kama hivyo ujue tayari nimeshakuwa staa.”
“Dick niambie ukweli kama unatoka na Irine,” aliniambia huku sauti yake akiwa ameielegeza.
“Hakuna ukweli katika hilo embu naomba uniamini basi hata kwa kuniigizia,” nilimwambia.
“Sawa nimekuelewa ila mimi sipendi kuona au kusikia habari hizo,” aliniambia.
“Hatuwezi kuwakataza waandishi wa habari waache kufanya kazi yao….acha waendelee kuniandika vibaya lakini kitu ambacho nakihitaji kutoka kwako ni uaminifu, nataka uniamini kutoka moyoni mwako,” nilimwambia.
“Sawa nimekuamini,” alinijibu kisha akaweza kuniaga na kukata simu. Precious alionekana kunipenda sana kuliko kitu chochote kile.
****
Niliutumia umaarufu niliyozidi kuupata katika kuendelea kuandika hadithi mbalimbali ambazo nilikuwa nikizichapisha katika mitandao ya kijamii. Zilizidi kupendwa sana na kila siku nilizidi kujiongezea mashabiki wengi waliyoonekana kunipenda na kuzipenda kazi zangu.
“Hello Dick Mapenzi.”
“Yes Hello Alice.”
“How are you?” (Habari yako?)
“Fine, how about you?” (Nzuri, vipi kuhusu wewe?)
“Everything is good, where are you? (Kila kitu kipo vizuri, uko wapi?)
“Tanzania and you?” (Tanzania na wewe?)
“Kenya.”
“Tell me?” (Niambie.)
“Ireally like reading your stories is very good.” (Napenda sana kusoma hadithi zako ni nzuri sana.”
“Thank you so much and I am glad to hear that.” (Asante sana na pia nafurahi sana kusikia hivyo.)
“Ok.” (Sawa.)
“What story didi you like?” (Hadithi ipiumeipenda?)
“CHUMBA CHA MASAJI.)
“Ok.” (Sawa.)
“Ok.” (Sawa.)
Nilimaliza kuchat Instagram na Alice shabiki yangu kutoka Kenya msichana ambaye alionekana kuvutiwa na hadithi zangu.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane sehemu ijayo mahali hapahapa.

#Like nyingi, komenti yako pamoja na Share nyingi ndizo zitafanya Chombezo hili liweze kufika mbali.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-45
Mtunzi:Juma Hiza
Age:18+

Niliendelea kujizolea umaarufu kila siku, umahiri wangu katika kutunga na kuandika Hadithi za kimapenzi ulinifanya nizidi kupendwa sana huku wengi wao wakiwa ni wanawake ambao ndiyo walikuwa wakizifuatilia sana kazi zangu. Mpaka kufikia muda huo sikuwa nimefanikiwa kucheza filamu yoyote lakini nilibahatika kuandika hadithi iliyochezewa filamu na mtu maarufu ambaye pia nilikuwa nikitoka naye kimapenzi.
Lengo langu kubwa la kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Irine ilikuwa ni kuutafuta umaarufu wa kuandikwa magazetini na kweli katika hilo nilifanikiwa.
Mchezo wangu wa kuchat na watu haukuishia kwa Alice kutoka Kenya bali uliendelea mpaka baadhi wa Wazungu wakawa wananitafuta. Nilifahamu yote yale yaliletwa na umaarufu ambao nilikuwa nao hivyo kila kitu kilichokuwa kikiendelea hakikuweza kunitisha wala kunishangaza, nilitegemea kila kitu kilichokuwa kikitokea.
Waandishi wa habari nao hawakuwa mbali katika kutafuta habari, nilikuwa nikipata Interview nyingi kutoka katika vituo tofautitofauti vya habari ambavyo vilikuwa na lengo la kutaka kufahamu historia yangu ya maisha mpaka ikatokea nikawa katika mahusiano na Irine.
Kwa kweli lilipofikia suala la kuwaeleza ukweli wa mahusiano yangu niliamua kuficha, sikutaka kufanya ule ni ukweli ambao kila mtu angeweza kuufahamu. Nilipoulizwa swali hilo niliweza kukanusha na kudai kuwa zilikuwa ni skendo za magazeti ambayo yaliamua kuandika kwa lengo la kuyauza magazeti yao.
“Kama unavyojua tena ndugu mwandishi mtu ukishapata jina kidogo lazima mengi yatatokea. Ni kweli nimeona na nimesikia mengi kuhusu mimi na Irine lakini yote yatabaki kuwa ni maneno tu. Magazeti nayo yananichafua sana jina langu la Dick linaonekana kuwa kama la kihuni kitu ambacho si kweli. Hakuna kitu kingine kinachoendelea nyuma yangu na Irine zaidi ya kazi tu,” haya yalikuwa ni maneno yangu niliyopenda kuyatamka kila nilipokuwa nikiulizwa na waandishi wa habari kuhusu kuhusishwa kuwa kimapenzi na Irine.
Sikutaka kuyaweka wazi mahusiano yangu na Irine hasa katika kipindi kile ambacho Precious alikuwa amejifungua na tayari alikuwa ameshapata wasiwasi juu ya habari alizokuwa akizisikia kuhusu Irine.
Nilikuwa makini sana tena zaidi ya kuwa makini, kumbukumbu hazikunipotea, nilikuwa nikikumbuka kila kitu nilichokuwa nikikizungumza, sikutaka kung’atang’ata maneno, nilizungumza ukweli wa kile ambacho niliamini kisingeweza kuniumbua baadae.
****
Maisha yaliendelea huku nikiendelea kuuficha ukweli wa mahusiano yangu na Irine. Nilijaribu kumshirikisha juu ya kile nilichokuwa nikikifanya na kumuuliza kama nilikuwa sahihi au la. Alionekana kufurahishwa sana, hakutegemea kama ningeweza kufanya hivyo, hilo ndilo lililozidi kumfurahisha kiasi kwamba akazidi kunipenda kupita kawaida.
“Ujue mimi sikutegemea kama ungeweza kufanya hivyo,” aliniambia nilipokuwa nyumbani kwake Tegeta majira ya usiku, tulikuwa chumbani, wakati huo nilikuwa nimevaa bukta huku juu nikiwa kifua wazi na yeye alikuwa katika vazi la kanga laini aliyokuwa amejifunga mpaka kifuani ndani yake hakuwa amevalia chochote. Alikuwa amekilaza kichwa chake kwenye mapaja yangu.
“Hukutegemea nini sasa?”nilimuuliza huku nikimpapasa uso wake laini ambao haukuwa na chunusi hata moja.
“Mimi nilijua ungeitumia nafasi hiyo kutafuta kiki,” aliniambia kwa sauti nyororo iliyogubikwa na wimbi la jinamizi la mapenzi lililokuwa linataka kuniingia hasa kwa mapema kiasi kile, niliwahi kulikemea.
“Irine sipo na wewe kwa lengo la kutafuta umaarufu bali nipo na wewe kwa lengo moja tu,” nilimwambi kisha nikanyamaza, nikamtazama, alionekana kuwa na shahuku ya kutaka kufahamu lengo langu. Akanyanyua kichwa chake kutoka katika mapaja yangu kisha na yeye akanitazama, tukatazamana.
“Lengo gani?” aliniuliza hapa ni baada ya uvumilivu wa kutazamana kumshinda.
“Nataka kutengeneza maisha bora na wewe na si bora maisha,” nilimwambia.
“Maisha bora?” aliniuliza.
“Ndiyo Mpenzi, natamani vitu vingi sana nifanye na wewe na vyote haviwezi kutimia bila ya kitu kimoja.”
“Kitu gani?”
“Upendo yani mapenzi ya dhati.”
“Unamaanisha nini?”
“Namaanisha bila upendo hakuna maisha bora, bila upendo hakuna familia bora ambayo nitaweza kutengeneza na wewe, bila upendo siwezi kufunga pingu za maisha na wewe, bila upendo siwezi kufanya lolote na ndiyo maana nikakuambia natamani vitu vingi sana lakini ukikosekana upendo nitashindwa.”
“Mume wangu.”
“Niambie.”
“Kitu gani unatamani kutoka kwangu.”
“Natamani mengi sana lakini kikubwa natamani mtoto.”
“Hilo tu?”
“Ni miongoni kati ya ninavyotamani kutoka kwako.”
“Usijali mimi nitakuzalia tena sio mtoto ni watoto.”
“Nitafurahi sana nahisi ndoto yangu itakuwa imetimia.”
“Ndoto yako gani?”
“Kuwa na mtoto yani mrithi wa mali zangu.”
“Usijali Mpenzi nimeumbwa kwa ajili yako yote unayotaka nitakutimizia kama ni mtoto pia nitakupatia.”
“Kweli?”
“Ndiyo Hubby sioni sababu yoyote ya kukudanganya.”
“Mimi nafurahi na tena najivunia kukupata katika maisha yangu umekuwa mwanamke wa kitofauti sana kwangu.”
“Inamaana hao wengine walikuwaje?”
“Vivuruge tu yani pasua kichwa.”
“Hahaha! Lakini kwangu je?”
“Kwako Napata burudisho la moyo pumziko la ubongo.”
“Kwa maneno sikuwezi.”
“Huo ndiyo ukweli,” nilimwambia.
Kwa muda ambao tulimaliza mazungumzo, mikono yangu haikuacha kutulia sehemu moja, ilikuwa ikitalii sehemu mbalimbali za mwili wa Irine, kuna muda nilikuwa nikizichezea nywele zake mara nikashuka shingoni nikaitomasa, nikashuka kifuani na hatimaye nikaangukia mapajani mwake, nilikuwa katika weweseko la mapenzi, sikutulia sehemu moja kama mlinzi aliyekuwa malindoni, kila sehemu ya mwili wake ilikuwa imeumbwa ikaumbika haswaa!, hakukuwa na sehemu nilipopashika kwa muda ule kisha akawa amenyamaza kimya kama sanamu, alikuwa akitoa mguno kuashiria alikuwa akipata msisimko.
“Unataka nini tenaaaaaaa umeanzaaaa,” aliniambia kwa sauti iliyoanza kukosa uvumilivu.
“Baby nipe kidogo,” nilimwambia huku nikiifungua kanga yake, alikuwa ameifunga kizembe hivyo sikupata kazi sana ya kuifungua kilaini tu ilifunguka na sasa macho yangu yakawa ana kwa ana na vya siri alivyokuwa amevificha kangani.
Sikutaka kubaki kumshangaa kama bongo movie isipokuwa niliianza kazi yangu ya kucheza na bustani yake. Nilihakikisha mpaka anazidiwa vya kutosha ndipo ambapo niliweza kuingia mchezoni, sikutaka kumpa nafasi ya kuichezea mashine yangu ambayo na yenyewe ilikuwa tayari imezidiwa, nilimlaza chali kisha nikaanza kuingiza mashine taratibu.
“Aaaaaaiiiishhhhhh ooooooohhhh jamaniiiiii Dickkkk mbona tamu hivyooooo aaahhhhh ooooohhh,” aliniambia huku akitoa miguno mara baada ya kuingiza mashine yangu. Ilipoingia sikutaka kuipotezea muda wake ilianza kufanya kazi yake. Niliendelea kulisakata kabumbu mpaka pale wazungu weupe waliponibishia hodi, walikuwa wakitaka kutoka.
“Dick mwagia ndani tu…mwagiaaaa aaaahhhhh,” aliniambia huku akiendelea kutoa miguno ya kimahaba.
“Mmmmmhhhh ooooooooohh,” nilianza kutoa miguno wakati ambao wazungu walikuwa njiani kutoka nje.
“Mwagia babyyyyy babyyyyy babyyyyyy aaaaaahhhh oooooooh tamu baby tamuuuuu,” alizidi kutoa miguno huku akiwa amening’ang’ania, wakati huo nilikuwa tayari nimeshatoa wazungu weupe.
Tuliendelea kuucheza mchezo huo, tulipochoka tulipumzika, tulipopata nguvu mpya tuliendelea mpaka pale ilipofikia mwisho wa mchezo wetu wa utamu. Irine alinishukuru kwa kumridhisha usiku ule. Tulikwenda bafuni kuoga, tuliporudi tulijitupa kitandani kisha usingizi mzito uliweza kutupitia.
****
Niliamka katika siku ambayo naweza kusema ilikuwa ni siku mbaya sana kwangu, siku hiyo Magazeti yaliandika habari mbaya sana kuhusu mimi, sijui ni nini kilitokea au ni nani alitokea na kwenda kuzipeleka habari zile kwa waandishi wa habari ila nilijikuta tu! nikikumbana na skendo ambayo kwa upande wa pili wa shilingi ilikuwa na ukweli ndani yake na ni katika hiyo skendo iliweza kunipa funzo.

Je, ni nini kitaendelea?
Tukutane sehemu ijayo mahali hapahapa
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-46
JUMA HIZA
+18

ILIPOISHIA........

Niliamka katika siku ambayo naweza kusema ilikuwa ni siku mbaya sana kwangu, siku hiyo Magazeti yaliandika habari mbaya sana kuhusu mimi, sijui ni nini kilitokea au ni nani alitokea na kwenda kuzipeleka habari zile kwa waandishi wa habari ila nilijikuta tu! nikikumbana na skendo ambayo kwa upande wa pili wa shilingi ilikuwa na ukweli ndani yake na ni katika hiyo skendo iliweza kunipa funzo.

SONGA NAYO.........

Ilikua ni siku ambayo magazeti yaliandika habari kuwa nilikuwa nikitembea na mke wa mtu ambaye nilibahatika kuzaa naye mtoto na kibaya zaidi waliandika kuwa hata nyumba ambayo nilikuwa nikiishi ni ya huyo Mwanamke ambaye alinihonga mara baada ya kufanikiwa kumpa ujauzito. Kwa kweli habari hizo ziliniweka katika mshangao wa hali ya juu, sikujua ni nani ambaye alihusika katika hilo, mtu wa kwanza ambaye nilimfikiria kwa wakati huo alikuwa ni Precious, niliamini Precious ndiye mtu pekee ambaye alikuwa akiufahamu ukweli huu tena aliniahidi kuwa itabaki kuwa siri kati yetu.
Sasa kwanini anisaliti?
Hili ndiyo lilikuwa swali kubwa ambalo nilijiuliza lakini sikuweza kupata jibu lolote. Kichwa changu kilitawaliwa na maswali lukuki.
“DICK KAZAA NA MKE WA MTU.”, “UKWELI KUHUSU DICK KUWA NA MTOTO.”
Hivi vilikuwa ni baadhi ya vichwa vya habari vya magazeti ya udaku yaliyopamba moto kwa habari hizo siku hiyo.
“Dick utaniambia nini kuhusu hili?”
“Hakuna kitu.”
“Hakuna kitu wakati huu ndiyo uchafu unaoufanya?”
“Irine mimi hata sielewi naona mapichapicha.”
“Mapichapicha wakati kila kitu kinaonekana hapa au unataka kuniambia waandishi wa habari ni waongo?”
“Irine hakuna ukweli wowote ulioandikwa hapa niuwongo mtupu.”
“Dick usinifanye mimi mtoto mdogo sawa naelewa kila kitu.”
“Irine huo ndiyo ukweli ambao naufahamu sina ukweli mwingine.”
“Dick kumbe na wewe haujatulia?”
“Mpenzi wangu kwanini hutaki kuniamini?”
“Sitaki kukuamini na sitakuamini Dick, najutia maamuzi yangu ya kuwa na wewe kumbe nyuma ya pazia una mtoto halafu umezaa na mke wa mtu?”
“Irine nielewe mpenzi hakuna chochote ninachokifahamu kwanza mimi mwenyewe nashangaa sijui ni nani amepanga kunichafua.”
“Unashangaa? Inamaana unataka kujifanya hujui kinachoendelea?”
“Sijui Irine kweli tena yani nimechanganyikiwa.”
“Umechanganyikiwa wakati hiyo ndiyo tabia yako. Hivi Dick ni kitu gani umekosa kwangu, ni nini ambacho umekikosa kwangu.”
“Hakuna kitu nilichokosa kwako.”
“Dick naomba uniache, niache Dick.”
“Irine mpenzi wangu nipe nafasi basi nijieleze.”
“Nikupe nafasi gani Dick, nimekupa moyo wangu lakini tayari umeshaumiza naomba uniache Dick.”
“Irine.”
(Alinyamaza kimya) huku machozi yakimdondoka.
“Irine mpenzi wangu.”
(Alinyamaza kimya)
“Nipe nafasi mpenzi wangu nijieleze,” nilimwambia lakini hakujibu lolote, alinyamaza kimya kana kwamba alikuwa bubu, nilijitahidi kumsemesha kadri niwezavyo lakini hakuna nilichoambulia zaidi ya machozi yake aliyokuwa akibubujikwa.
Nilikumbuka usiku wa siku hiyo tulitoka kufanya mapenzi tena hakukuwa na tofauti yoyote kati yetu lakini nilishangaa tukiamka katika asubuhi ya tofauti, asubuhi ambayo ilibadilisha kila kitu katika mapenzi yetu.
Tulikuwa katika ugomvi ambao uliletwa na skendo ambayo ilinihusu kwa asilimia kubwa wala hakukuwa na cha kuficha kwani kila kitu kiliwekwa wazi.
Nilijitahidi kudanganya kama ilivyokuwa kawaida yangu lakini uwongo wangu uligonga mwamba. Hakukuwa na uwongo niliouzungumza kisha ukaenda kumuingia Irine ambaye alionekana kuwa mwenye hasira sana hasa baada ya kugundua kuwa sikuwa muaminifu katika mapenzi, nilimdanganya vya kutosha.
Kitendo cha kugundua kuwa nilizaa na mwanamke mwingine nje tena mke wa mtu kilimuumiza sana, hakujua ni kwa jinsi gani alitakiwa kunieleza ili niyagundue mamivu aliyokuwa nayo. Kupitia machozi yake pamoja na ukimya alioamua kukaa baada ya kushindwa kuzungumza lolote, nilifahamu alikuwa katika wakati wa hasira, alibaki akinitazama muda wote.
“Nijibu basi mpenzi,”nilimwambia kisha nikamtazama, alionekana kuwa mwenye hasira sana.
“Naomba Dick uende, niache na maisha yangu,” aliniambia maneno ambayo alimaanisha.
Sikutaka kuwa king’ang’anizi sana kwa wakati ule kwani Irine alikuwa tayari ameshagundua ukweli wa kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Niliamua kuondoka nyumbani kwake kisha nikaelekea nyumbani kwangu huku kichwa changu kikiwa na maswali lukuki ambayo yaliniweka katika wakati wa mawazo.
Nilikuwa nikiwaza mambo mengi sana lakini mpaka nafanikiwa kufika nyumbani kwangu sikuwa nimeng’amua lolote lile, nilionekana kuchanganyikiwa kutokana na kile ambacho kilikuwa kimetokea. Sikujua ni nani ambaye alikuwa akinifuatilia undani wa maisha yangu.
Nilianza kupata mashaka na mtu ambaye nilikuwa nikimtilia mashaka alikuwa ni Precious, nilihisi yeye ndiye alikuwa amehusika kwa asilimia kubwa katika kuzisambaza habari zile kwa waandishi wa habari ili aweze kujitengenezea umaarufu.
Niliamua kumpigia simu huku nikiwa mwenye hasira sana, nilitamani kumtukana lakini alipopokea ajabu nilishindwa kufanya hivyo, alikuwa akilia na yale aliyonieleza yalizidi kunichanganya kabisa akili yangu.

Je, ni nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo mahali hapahapa.

Usiache kutoa maoni kuhusu Chombezo hili. Tuambie ni nini unahisi kitatokea baadae katika maisha ya Dick?
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-47
JUMA HIZA
+18

ILIPOISHIA......

Niliamua kumpigia simu huku nikiwa mwenye hasira sana, nilitamani kumtukana lakini alipopokea ajabu nilishindwa kufanya hivyo, alikuwa akilia na yale aliyonieleza yalizidi kunichanganya kabisa akili yangu.

SONGA NAYO....

“Dick mume wangu, mume wangu Dick,” aliniambia mara baada ya kupokea simu, sauti yake ilinidhihirishia wazi kuwa alikuwa katika kilio kwa wakati huo, kilio chake kikazidi kunichanganya.
“Sasa unalia nini na mume wako amefanyaje?” nilimuuliza.
“Kwanini umeamua kunichafua kwenye magazeti kwanini Dick, mume wangu akijua huoni utaniletea matatizo kwenye ndoa yangu?”
“Precious mbona unanichanganya?”
“Nakuchanganya na nini Dick, umeamua kunichafua magazetini kwanini umenifanyia hivyo?”
“Inamaana unataka kuniambia wewe hauhusiki kabisa na tukio hili?”
“Tukio gani?”
“La kuwaambia waandishi wa habari kuhusu usiri wa jambo hili.”
“Simjui mwandishi hata mmoja hivi nitaanzaje kwenda kutangaza wakati najua kuwa hii ni siri tena tumepanga ibaki kuwa siri kati yetu,” aliniambia Precious maneno ambayo kiukweli yalizidi kuniweka katika wakati wa mawazo, mpaka kufikia wakati huo sikujua ni nani ambaye alihusika katika kuzitangaza habari zangu kwa waandishi wa habari. Nilikuwa katika wakati mgumu sana kwani ni muda mfupi ulikuwa umepita tangu nilipoweza kugombana na Irine kiasi kwamba akaamua kunifukuza nyumbani kwake.
Nilizidi kupagawa baada ya Precious kuniambia kuwa hakuhusika na lolote katika habari zile kwani kwa upande wake alikuwa katika mshangao na muda wote alikuwa akilia kwa kumuhofia mume wake endapo angeweza kuziona au kuzisikia habari zile.
“Kwani mume wako yuko wapi?” nilimuuliza swali ambalo sikumbuki kama niliwahi kumuuliza siku za karibuni, ni muda mrefu ulipita sikutaka kuzisikia habari za mume wake, niliamua kufanya hivyo kutokana na sababu za Precious kutopendelea kusikia habari za mume wake pindi anapokuwa na mimi.
“Yupo,” alinijibu kwa sauti iliyochanganyika na uwoga.
“Sasa unaogopa nini?” nilimuuliza.
“Dick mume wangu namjua na endapo akizisikia habari hizi sijui uso wangu nitauweka wapi?”
“Precious kila kitu nahisi imeharibika na sijui itakuwaje?”
“Dick kwani ni nani ameenda kuwaeleza waandishi wa habari?”
“Mimi sijui yani nimechanganyikiwa Precious.”
“Mungu Wangu.”
Mpaka kufikia hapo nilikuwa nimechanganyikiwa, nilihisi kuwa na nuksi katika siku hiyo, akili yangu haikuwa sawa na kila nilichokuwa nikikifikiria nilihisi kukosea hivyo vyote nilivipuuzia.
Kwa wakati ule nilipokuwa nikizungumza na Precious na kutoambulia lolote nilichoamua ni kukata simu. Sikuwa sawa hata kidogo. Nilikumbuka kulitafuta gazeti ambalo lilikuwa limeandika habari iliyonihusu na hapo niliamuakulitafuta jina la mwandishi aliyehusika kuiandika habari ile. Isack Mwakyonya ndiyo jina nililokutana nalo la mwandishi wa habari hiyo, niliamini kwa asilimia kubwa ukweli wa maswali yote yaliyokuwa yakinizonga akilini mwangu majibu yake alikuwa nayo yeye, niliamini kama yeye hakuhusika katika kudadisi ukweli ule basi alikuwepo mtu wa pembeni ambaye alihusika kuzitoa habari hizo kisha nay eye akaweza kuziandika. Niliinakili namba yake ya simu kisha sikutaka kupoteza muda niliamua kumpigia, simu yake ilionekana kuwa bize lakini sikukata tama, niliendelea kupiga kila mara mpaka pale nilipobahatika kumpata. Alipopokea niliwahi kujitambulisha kwa jina ambalo haikuwa rahisi kwa yeye kuweza kunifahamu.
“Nazungumza na nani?” aliniuliza kwa sauti iliyoonekana kuwa bize kiasi kwamba hata kitendo cha kupokea simu kilikuwa kikimkwaza.
“Naitwa Akilimali Kazipesa.”
“Akilimali?”
“Ndiyo.”
“Ok Akilimali niambie nikusaidie nini?”
“Bila shaka nazungumza na Isack mwandishi wa habari gazetini?”
“Ndiyo mimi bila shaka hujakosea vipi una dili la habari nini?”
“Ndiyo tena ni zaidi ya dili la habari.”
“Nipe sasa ndugu tupige pesa mjini hapa.”
“Ni kweli lakini kwa habari hii itabidi tuonane ili niweze kukueleza kila kitu.”
“Habari yenyewe inamuhusu Staa au?”
“Ndiyo tena staa wa bongo movie.”
“Ok niambie kwahiyo unataka tukutane wapi?”
“Labda wewe ndiyo uniambie unataka tukutane sehemu gani?”
“Nafikiri maeneo ya Beach itapendeza zaidi.”
“Beach gani?”
“Tukutane Sunrise Beach Resort.”
“Kwa leo itawezekana?”
“No, maybe we do tomorrow.” (Hapana, labda tufanye kesho.)
“Muda gani?”
“Mchana.”
“Sawa,” nilimjibu kisha na huo ndiyo ulikuwa mwisho wa mazungumzo yetu.
Kwa maongezi ambayo nilizungumza na Isack Mwakyonya alionekana kuwa mtu wa kupiga dili kupitia habari za mastaa, nililifahamu hilo baada ya kugundua kuwa na mimi nilikuwa ni miongoni kati ya wateja ambao walikuwa wakimpelekea habari za udaku jambo ambalo halikuwa na ukweli wowote. Sikutaka kuufikiria ule umbali uliyokuwepo kati ya Mbezi Beach na Mji Mwema, Kigamboni ambapo ndipo ilipokuwa Sunrise Beach Resort bali nilichokuwa nikikifikiria kwa wakati huo ni kukutana na Isack kisha niitumie nafasi hiyo katika kumbaini mtu aliyehusika katika kunichunguza kiasi kwamba akaamua kunichafua magazetini.
****
Picha zangu pamoja na Precious ziliendelea kusambaa mitandaoni, kila mtu alikuwa na lake la kuandika kwa siku hiyo. Wapo waliyoitumia siku hiyo katika kunitukana na wengine waliitumia kama sehemu moja wapo ya kujiingizia kipato kupitia blog mbalimbali za kijamii.
Nilianza kupigiwa simu na waandishi wa habari kutoka sehemu tofautitofauti ambao walikuwa na lengo la kunifanyia interview kuhusu skendo ile iliyokuwa ikinikabili magazetini. Wote sikutaka kuzungumza nao, niliamini kwa kufanya hivyo nilikuwa naendelea kulilinda jina langu ambalo tayari lilikuwa limeanza kuchafuliwa na magazeti ya udaku.

Je, ni nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo mahali hapahapa.

Usiache kutoa maoni kuhusu Chombezo hili. Tuambie ni nini unahisi kitatokea baadae katika maisha ya Dick?
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-48
JUMA HIZA
+18

ILIPOISHIA.......

Nilianza kupigiwa simu na waandishi wa habari kutoka sehemu tofautitofauti ambao walikuwa na lengo la kunifanyia interview kuhusu skendo ile iliyokuwa ikinikabili magazetini. Wote sikutaka kuzungumza nao, niliamini kwa kufanya hivyo nilikuwa naendelea kulilinda jina langu ambalo tayari lilikuwa limeanza kuchafuliwa na magazeti ya udaku.

SONGA NAYO.........

Laiti kama ingetokea kama ungekutana na mimi kwa wakati ule kisha ukaniuliza kuhusu hadithi au kitu kinachohusu kazi yangu kwa kweli nisingeweza kukujibu jibu fasaha. Akili yangu haikuwa sawa hata kidogo, nilikuwa nikiwaza kitu kimoja tu! ambapo nikukutana na huyo Mwandishi wa habari na niweze kumfahamu huyo mhusika ambaye alikuwa ananifuatilia. Kuna muda nilianza kupata mashaka juu ya huyo mwandishi wa habari, nilihisi kuna mchezo alikuwa akiufanya dhidi yangu na kwa maana hiyo nisingeweza kuufahamu ukweli kwani nilikuwa naenda kukutana na mhusika mwenyewe. Hilo lilizidi kuniweka katika wakati wa mawazo, nikakumbuka ule mchezo mchafu ambao ulikuwa ukifanywa na waandishi wa habari wenye lengo la kukuchafua halafu baadae wanakuambia ili wasikuchafua inabidi uwalipe kiasi cha pesa ambapo wataweza kuipotezea habari.
Bado sikutaka kuamini kirahisi kuwa nilikuwa katikamhuo mchezo, kila nilichokuwa nikikiwaza nilikiona kuwa na uwongo ndani yake.
“Kama kweli nia yake ni kutafuta pesa kupitia hiyo skendo mbona sasa hajanitafuta?” nilijiuliza swali lililonifanya nipuuzie lile wazo lililokuwa limenijia. Kwa wakati mmoja nilikuwa nikiwaza mambo mengi sana, sikuacha kumuwaza Irine msichana ambaye alihusiika kwa asilimia kubwa katika kunipa umaarufu ambao kwa muda ule ulikuwa ukinitesa, maisha yangu yalibadilika na kuwa kama ya mnyama digidigi. Kuna muda nilijilazimisha tabasamu usoni mwangu, nikataka kutabasamu kinafki lakini tabasamu halikuja, sikuhitaji kutabasamu kwa wakati huo hivyo nilikuwa katika mkunjo wa sura.
Nilimpigia simu Irine, simu yake ilikuwa ikiita tu! bila kupokelewa, niliamini kuwa aliamua kufanya kusudi kunipokelea kutokana na tatizo lililokuwa limetokea. Wakati nikiendelea kumpigia Irine bila mafanikio akili yangu ikaanza kumuwaza Precious, sikujua alikuwa katika wakati wa aina gani wala sikujua kama mume wake alizipata habari hizi au la. Hilo sikutaka kujisahaulisha, habari ile ilikuwa ni habari mbaya lakini ilisambaa kila kona ya nchi na niliamini mpaka kufikia wakati ule hakukuwa na mtu ambaye alikuwa hafahamu kile kilichokuwa kikiendelea.
Kitendo cha kuendelea kumuwaza Precious ambaye alikuwa akilia na akimuhofia mume wake kilikuwa kikizidi kuniweka katika wakati wa maumivu, sikutakiwa kuwa katika hali hiyo kwa wakati huo. Niliamua kuacha kumuwaza japo ilikuwa ni ngumu kufuta kumbukumbu za mtu ambaye tayari alikuwa akilini mwako, nikajitoa ufahamu kisha nikampigia simu rafiki yangu Mick, alipopokea simu yangu sikutaka akuzungumza lolote zaidi ya kumwambia kuwa nilihitaji kuonana naye.
“Kuna nini?” aliniuliza.
“Nataka tuonane nitakwambia,” nilimwambia.
“Sasa tukutane wapi?” aliniuliza.
“Njoo hapa nyumbani kwangu mida hii kaka,” nilimwambia.
“Sawa nakuja,” alinijibu.
Baada ya kupita dakika kadhaa Mick aliweza kufika nyumbani kwangu, nilimkaribisha kwa kumpa juice hapa ni baada ya kudai kuwa alikuwa ameshiba chakula kisha sikutaka kupoteza muda nikaanza kumwambia kile nilichokuwa nimemuitia.
“Nimekuita hapa ndugu yangu nina tatizo.”
“Tatizo gani tena au kuna demu wa kishua umempata nini?”
“Acha masihara ndugu yangu ina maana unataka kuniambia hujasoma magazeti leo?”
“Hapana ujue mimi sio mpenzi sana na hayo magazeti hasa ya udaku nikisoma labda nimekosa kazi ya kufanya. Vipi kwani kuna nini?”
“Aisee ndugu yangu mambo yameharibika.”
“Mambo yameharibika! Mambo gani tena.”
“Waandishi wahabari tayari wameshaufahamu ukweli wangu.”
“Ukweli wako upi tena?”
“Wameniandika kuwa nimezaa na Precious yule mke wa mtu.”
“Duh! Sasa ni nani ambaye ameenda kuwaeleza waandishi wa habari.”
“Yani mimi mwenyewe sielewi hapa nimechanganyikiwa.”
“Na Irine naye imekuwaje?”
“Irine amekataa kabisa kunielewa baada ya kuziona habari hizi yani hapa ninavyokwambia hataki kabisa kuniona.”
“Umejaribu kuongea naye vizuri?”
“Yani nimeongea naye kila aina ya lugha lakini hataki kabisa kunisikia wala kuniona.”
“Duh! Sasa itakuwaje?”
“Sielewi Mick yani akili yangu imechoka.”
“Lakini rafiki yangu mimi nilikwambia huo mchezo wako unaoufanya kuna siku utakugharimu sasa umeona jinsi unavyotaabika wakati kazi ilikuwa ni ndogo tu!”
“Kazi gani?”
“Kazi ilikuwa ni kutulia na demu mmoja tena Evadia yote haya yasingekukuta.”
“Mick nimekuita hapa kwa ajili ya ushauri na si unikumbushie kuhusu huyo Malaya Evadia.”
“Evadia ndiyo Malaya au wewe mbona sijakuelewa hapo.”
“Mick embu tuachane na hiyo mada, tuongelee haya ambayo yanatuhusu.”
“Mimi kwa ushauri wangu hapo itabidi umtafute huyo mwandishi aliyeandika hiyo habari kisha fanya kuzungumza naye kirefu nadhani anaweza akakueleza ukweli kuhusu mtu au lengo la yeye kuiandika habari hiyo.”
“Tayari nimeshafanya mawasiliano naye.”
“Anasemaje?”
“Bado sijazungumza naye ila tumepanga kukutana sehemu kwa ajili ya mazungumzo.”
“Una uhakika?”
“Ndiyo.”
“Mnaenda kukutana wapi?”
“Sunrise.”
“Mimi naamini endapo ukikutana na huyo mwandishi wa habari kila kitu kitaenda sawa hivyo jiamini.”
“Imani imepotea Mick yani nimekuwa mpole nauona mwisho wangu kwa kweli.”
“Nadhani katika hili kwako litakuwa ni funzo na tena utajifunza haswaa!” aliniambia Mick maneno yaliyopenya vyema na kuniingia akilini.
Nilimuamini sana Mick na kila ambacho alichokuwa akiniambia nilikishikilia kama ngao ambayo nilihakikisha inanikinga na kila baya ambalo lilikuwa linakwenda kunitokea. Maneno yake machache yaliyojawa na ukarimu yaliniongoza vyema japo kuna kipindi nilikuwa mkaidi nikaona ufahari kwa kubadilisha wanawake kama nguo lakini hakuacha kunisihi kuacha tabia niliyokuwa nayo.
Nilifanya yale kwa sababu ya umaarufu wangu, tangu nilipokuwa maarufu Facebook na Instagram kupitia Machombezo yangu na hatimaye nilikuwa maarufu katika kiwanda cha filamu na kuwa kama mwandishi bora wa filamu niliyekuwa napendwa zaidi.
****
Siku iliyofuata nilikwenda kukutana na Isack Mwakyonya mwandishi wa habari tuliyeahidiana kukutana Sunrise, nilipofika nilimtafuta na kumjulisha kuwa tayari nilikuwa nimeshafika lakini ajabu simu yangu hakuwa akipokea hata pale nilipomtumia ujumbe mfupi wa kumtaarifu kuwa nilikuwa nimeshafika hakuweza kunijibu lolote. Hilo lilizidi kunishangaza, nikaangalia vyema kama pale nilikuwa Sunrise kweli au la. Naam! Nilikuwa ndani ya Sunrise lakini mtu ambaye niliahidiana kukutana naye pale hakuweza kunipa ushirikiano wowote, sijui niseme katika lugha ipi ili muweze kunielewa vyema labda niseme alinidanganya au aliniuza kwa maana nyingine. Nilimsubiri eneo lile huku nikitegemea wenda angeweza kunijibu lakini haikuwa hivyo. Ukweli ni kwamba alinidanganya na baada ya kukaa masaa kadhaa bila mafanikio yoyote niliamua kuondoka.
Barabarani nilionekana kukasirishwa sana na tukio lile, sijui ni nini ila nilihisi kudharauliwa mno. Ni bora angenieleza ukweli kuliko kunidanganya. Hilo lilizidi kuniweka katika wakati wa mawazo na lawama nilizokuwa nikizitoa kama mwendawazimu.
Nakumbuka nilipofika kivuko cha Kigamboni Ferry, nilipokea ujumbe kutoka kwenye namba nisiyoifahamu, iliniandikia hivi,
“PRECIOUS AMEJIUA YEYE PAMOJA NA MTOTO WAKE.”
Nilipousoma ujumbe huo uliweza kunitatanisha, ghafla! mwili ukaanza kunyong’onyea nikaishiwa nguvu.

Je, ni nini kitaendelea?
Mambo yanazidi kuwa mambo..
Dick atafanya nini baada ya hapo?
Unahisi ni nini kitatokea?
Usikose sehemu ijayo mahali hapahapa.

Je unaihitaji yote Chombezo hili ili kumuunga mkono mwandishi wako?

Jumanne ya leo kuna ofa. Iisome Chombezo hili kwa shilingi 1500 tu! mwanzo mpaka mwisho.
Mwisho wa ofa hii ni saa sita za usiku baada ya hapo itauzwa katika bei yake ya shilingi 3000. Nicheck WhatsApp kwenye namba 0712988278

Tumuunge mkono mwandishi kwa kununua kazi yake, kama una subiri vipande vijavyo mahali hapahapa vya NIFANYE NA MIMI KAKA DICK, usijali itaendelea na itaendelea hadi mwisho...
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-49
JUMA HIZA
+18

Kwa kweli nilikuwa nimeshaanza kuchanganyikiwa, akili yangu haikuwa sawa kabisa. Nilichoamua kukifanya ni kutafuta mahali ambapo niliweza kuegesha gari halafu nikautumia muda huo katika kuwaza kile nilichokuwa nimetumiwa katika ujumbe mfupi. Kuna muda nilijaribu kuyafumba macho yangu na kuhisi wenda nengeweza kuamka katika usingizi wa ndoto lakini haikuwa hivyo, nilikuwa katika maisha halisi, maisha ambayo tayari nilikuwa nimeanza kuyaona machungu.
“Amejiua?” nilijikuta nikijiuliza swali ambalo sikujua hata nilitakiwa kujijibuje, ni hapa ambapo nilihisi kuchanganyikiwa kabisa. Nikaichukua simu yangu kisha nikaifungua na kuingia katika kitabu cha kuhifadhi majina. Nilianza kupitia jina moja baada ya lingine, kwa wakati huo sikuwa najua hata nilikuwa natafuta nini. Nilikuwa nimeshapagawa ndugu msomaji. Niliwaza mambo mengi sana kila nililokuwa nikiliwaza sikulipatia ufumbuzi mwisho nilizidi kujiumiza kichwa.
Ghafla! Mick akawa ananipigia simu, haraka nikapokea kisha nikanyamaza kimya kumsikiliza kwa umakini.
“Dick ndugu yangu umeona sasa maisha yako ulivyoyaharibu, Aagghh! Ona sasa nimesikia yule mke wa mtu uliyezaa naye amejiua halafu sijui nani Precious kitu kama hicho yani Dar imechafuka kila kona ni habari kuhusu wewe,” aliniambia Mick maneno yaliyonifanya niingiwe na uwoga wa hali ya juu.
“Sasa ndugu yangu hapo tunafanyaje, eeehh! Utanisaidiaje ndugu yako niondokane na janga hili?” nilimuuliza Mick, yani hata sikuwa najua ni nini nilichokuwa nakizungumza. Akili yangu haikuwa kabisa pale.
“Yani hata sijui nitakusaidiaje,” aliniambia kisha akanyamaza kidogo halafu akaendelea kuzungumza.
“Kwani uko wapi sasa hivi?” aliniuliza.
“Nipo huku Ferry Kivukoni,” nilimjibu.
“Vipi yule mwandishi tayari umeshakutana naye na anasemaje?”aliniuliza.
“Hakuna nilichoambulia, ameniuza nimekuja mpaka huku nampigia simu ajabu hapokei wala hataki kujibu meseji zangu,” nilimwambia Mick kwa sauti ya kipole iliyoambatana na uwoga ndani yake.
“Dah! aisee pole sana ndugu yangu,” aliniambia Mick.
“Asante kwahiyo tunafanyaje?” nilimuuliza.
“Wewe si unarudi huku?”
“Ndiyo kaka.”
“Fanya tuonane ili tuzungumze kitu.”
“Mick nimekwama ndugu yangu sijui kama utaweza kunisaidia ili niweze kuondokana na fedhea hii iliyonikuta.”
“Kila kitu kitawezekana ila fanya tukutane pale Bamaga.”
“Bamaga?”
“Ndiyo.”
“Hapana Mick unajua wazi kabisa sasa hivi habari zangu zimesambaa kila kona sasa tukikutana hapo bamaga huoni itakuwa kama najiuzisha vile na waandishi wa habari wananitafuta kila kona.”
“Sasa wewe unataka tukutane wapi?”
“Mimi nafikiri tungekutana nyumbani kwangu tu.”
“Kweli basi tufanye hivyo,” aliniambia Mick.
Nilianza kuhisi Mick ndiye alikuwa mtu wa pekee ambaye angeweza kunisaidia kuondokana na janga hili ambalo lilikuwa limenipata, hofu yangu bado ilikuwa katika habari ambayo niliipata kuhusu kifo cha Precious, niliamini kwa asilimia kubwa kulikuwa kuna tukio lililokuwa linafuata baada ya hapo. Nikaanza kumfikiria mume wa Precious, sikujua kuwa alikuwa katika hali gani. Nilijaribu kuyapima yale maumivu ambayo angeweza kuyapata kipindi ambacho angeweza kusikia kuwa nilikuwa nikitembea na mke wake ambaye nilizaa naye mtoto aliyekuwa akimlea huku akiamini kuwa alikuwa ni mtoto wake wa damu, sikuacha pia kupima yale maumivu ya kufiwa na mke ambaye tena aliamua kujiua kwa kukiikimbia fedheha. Kwa kweli nilizidi kuziona siku za uhai wa maisha yangu zikupungua taratibu, nilikuwa nikikiona kifo changu mbele ya macho yangu.
Nilipofika nyumbani kwangu nilimkuta Mick akiwa tayari ameshafika, alionekana kunisubiria muda mrefu sana bila kuchoka. Niliposhuka kwenye gari mlinzi aliweza kunifuata na kuniletea habari nyingine ngeni kabisa. Aliniambia kulikuwa na watu watatu ambao walikuja kuniulizia, kati yao alikuwepo mwanamke mmoja aliyekuwa amembeba mtoto, mwanaume pamoja na mama mtu mzima.
Aliponiambia hivyo nikakumbuka kama kulikuwa na watu ambao nilipanga kukutana nao kwa siku hiyo, hakukuwa na mtu ambaye nilipanga kukutana naye, nikazidi kuchanganyikiwa aliponiambia kuwa kati ya hao watu pia alikuwepo mwanamke ambaye alikuwa amembeba mtoto. Kwa kweli nikazidi kuchanganyikiwa sana, sikujua ni nini kilichokuwa kikiendelea. Akili yangu ilikuwa imechoka, nikaamua kuingia ndani na Mick.
“ Vipi ndugu yangu,” aliniambia Mick.
“Dah! we acha ndugu yangu nahisi kufakufa,” nilimwambia Mick kisha akawa anacheka kwa sauti.
“Na utakufa kweli kwa huu mchezo unaoendelea aisee usipokuwa makini tunakwenda kukusahau,” aliniambia.
“Mchezo…Mchezo kivipi na kwanini useme nitakwenda kusahaulika?”
“Usijifanye huelewi kitu Dick, usijitioe ufahamu.”
“Sielewi kitu ndugu yangu ndiyo maana nauliza, sipo sawa kabisa.”
“Sasa ukisikia ukubwa au yale maneno sijui kuwa uyaone ndiyo haya, wanawake wanakwenda kukutoa roho.”
“Dah! yani nimekoma ndugu nimekomaa.”
“Huwezi kukoma bila funzo inabidi kwanza upate funzo halafu ndiyo ukome.”
“Unamaanisha nini unaposema hivyo.”
“Muda mfupi kabla hujaingia niikuwa nafuatilia habari katika website fulani hivi…nimekuta wameandika kuwa unahusikakwa namna moja ama nyingine na kifo cha Precious ambacho kimewaacha watanzania kinywa wazi….kila mtu haamini kwa kilichotokea, sijui hata utasema nini hapo.”
“Lakini..”
“Hakuna cha lakini hapo inabidi ukubaliane na kila kitu kilichotokea.”
“Siwezi, siwezi Mick lazima nipambane katika hili.”
“Huwezi nini sasa na utapambanaje kwa kitu ambacho ni kweli kinakuhusu….ukweli ni kwamba wewe ni Malaya na umalaya wako leo unakwenda kukugharimu maisha.”
“Mick.”
“Niambie Dick Mapenzi.”
“Mi naona kama hunishauri kitu hapo na lengo la mazungumzo haya ni unishauri nini nifanye ili niondokane na fedheha hii.”
“Cha kukushauri nini ufanye kwa kweli nitakudanganya labda nikwambie kitu kimoja.”
“Kitu gani?”
“Subiri dunia ikufunze kwanza maana umeshachelewa.”
“Mick unajua sikuelewi kabisa.”
“Huwezi kunielewa kwasababu akili yako haipo hapa..inawaza mambo mengi kwa wakati mmoja, sasa utawezaje kunielewa hapo,” aliniambia Mick.
Maneno ya Mick yalizidi kunifanya niiingiwe na hasira hasa baada ya kuwa nilikuwa nikimtazama wakati alipokuwa akizungumza, kuna muda nilitamani hasira zangu zote nizimalizie kwake kwa kumpiga lakini nilihisi kukosea kufanya hivyo. Nikabaki kuwa mpole nikiendelea kumsikiliza.
Sijui ni nini kilitokea ila nilishangaa Mick akakurupuka kutoka kwenye sofa alilokuwa amekaa na kuja upande niliyokuwepo huku akiwa ameishika simu yake, alikuwa akinionyesha mahojiano yaliyokuwa yakifanyika Live kupitia Application ya Hiza Tv, yalikuwa ni mahojiano kati ya mwanaume mmoja ambaye alikuwa akihojiwa na waandishi wa habari.
“Unamfahamu huyu mwanaume?” aliniuliza Mick.
“Hapana simfahamu,” nilimjibu.
“Aiisee wewe mwehu kweli inamaana hata kusoma huwezi,” aliniambia kisha nikayasoma yale maandishi ambayo yalikuwa yameandikwa kwa chini, yalikuwa ni maandishi makubwa yaliyoandikwa kwa rangi nyeusi na yalikuwa yakisomeka,
“MUME WA MWANAMKE ALIYEJIUA KISA SKENDO CHAFU.” Maneno hayo yaliambatana na picha ya Precious.

Je, ni nini kitaendelea?

Lipia shilingi 1500 tu! usome Chombezo hili mwanzo mpaka mwisho.
Wasiliana nami kwenye namba 0712988278 au nitumie ujumbe mfupi ili nikutumie Facebook au WhatsApp inbox.
 
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-50
JUMA HIZA
+18

Sikutaka kuamini kuwa Martine Deus jina ambalo liliandikwa pale ndiye alikuwa mume wa Precious. Moyo wangu ulizidi kuwa katika maumivu makali mno, kila nilipokuwa nikimuona Martine Deus nilihisi kuchanganyikiwa.
“Tunafanyaje?”nilimuuliza Mick.
“Hapa hakuna cha kufanya zaidi ya kutoroka, inabidi uende mbali sana ukajifiche maana inaonekana mpaka sasa unatafutwa,” aliniambia Mick kisha nikakubaliana na maneno yake. Niliamini kama ningeweza kuondoka na kwenda kujificha mbali nisingeweza kukamatwa.
“Sasa natakiwa kwenda wapi?”
“South Africa.”
“South Africa?”
“Ndiyo huko ndiyo kwenye usalama wako.”
“Naenda kufikia kwa nani?”
“Kuna ndugu yangu mmoja yuko huko nitafanya mazungumzo naye kwa njia ya Email halafu kila kitu kitakuwa sawa.”
“Una uhakika?”
“Niamini,” aliniambia Mick.
Siku iliyofuata Mick alianza kunihangaikia mipango ya kusafiri kwenda South Africa. Ilikuwa ni safari ya ghafla! na nilikuwa nikienda kwa kuzamia. Hakukuwa na njia nyingine niliyoiona kuwa na usalama kwangu zaidi ya kuondoka na kwenda huko mahali ambapo niliamini kulikuwa na usalama wa maisha yangu.
Hatimaye siku ya safari ikawadia, nikaenda Airport kwa kujifichaficha, Mick alikuwa akinisindikiza lakini kitu cha kushangaza tulipofika Airport tulikamatwa na watu waliyojitambulisha kuwa walikuwa ni polisi. Walikuwa na lengo la kunikamata na kunipeleka polisi, sikutaka kubisha wala kupingana na lolote lile kwa wakati huo, safari ya kwenda South Africa iliishia hapo na sasa nikakamatwa na wale watu waliojitambulisha kuwa walikuwa ni polisi, wakaniingiza katika gari lao kisha tukaondoka eneo lile. Mick tulimuacha Airport, sikutaka kujiuliza mara mbilimbili kwanini tulimuacha. Ajabu wale watu waliyojitambulisha kuwa ni polisi nilishangaa wakinipeleka sehemu nisiyoijua, ilikuwa ni sehemu tofauti na kituo cha polisi kama ambavyo waliniambia hapo awali. Tulitoka nje kidogo na jiji la Daresalaam, tuliingia katika moja ya pori ambalo kiukweli mpaka kufikia muda huo sikuwa najua lolote lililokuwa linakwenda kutokea.
“Shukaaaa,” aliniambia jamaa mmoja baada ya gari kusimama pembeni na pori lile.
“Kuna nini jamani?” niliwauliza.
“Wewe unajifanya kidume subiri sasa uoneshwe kuwa hapa mjini kutembea na mke wa mtu ni hatari,” alisema yule jamaa maneno ambayo yalinishtua sana, nilifahamu kuwa wale hawakuwa polisi kama walivyokuwa wamejitambulisha. Nilikuwa nimetekwa na wale watu nisiowafahamu kabisa, niliposhuka na wao wakashuka. Kuna muda nikatamani kukimbia eneo lile lakini nilishindwa. Wale watu walionekana kuwa katika miili iliyojengeka kimazoezi, walionekana kutisha mno kutazama na ni hapa ambapo niliamini ule ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha yangu.
Baada ya dakika kadhaa mara likatokea gari aina ya Hummer, lilikuja na kupaki pembeni na pale ambapo nilikuwa nimesimama kisha akashuka mtu aliyevalia mavazi ya suti nyeusi, alionekana kuwa mtu nadhifu sana, nilipomtazama sura yake haikuwa ngeni, niliwahi kumuona sehemu. Alikuwa ni yule mume wa Precious. Alionekana kutawaliwa na hasira sana, uso wake ulihifadhi chuki, alionekana kunichukia sana aliponitazama.
“Ulidhani utanikimbia?” aliniuliza kisha akawa anajilazimisha kucheka kwa sauti kubwa sana huku akiwa ananipigia makofi ishara kama ya kunipongeza jambo fulani.
“Hongera sana Dick, hongera kwa kufanikiwa kummiliki mke wangu tena kwa kuuonyesha ukidume wako ukadiriki mpaka kuzaa naye,” aliniambia maneno ambayo yaliniumiza sana.
“Nadhani ulifikiri kwa mpango aliyokushauri rafiki yako ungeweza kuwa salama, ulipanga kuondoka sasa ona uko sasa hivi?” aliniuliza swali la kunikejeli kisha nikajaribu kuyalinganisha na maneno ya Mick. Kulikuwa na uhusiano, niliamini bila shaka Mick alikuwa ameniuza na kweli alifanikiwa katika hilo.
Yule mume wa Precious hakutaka kuwa muongeaji sana, alipanga kufanya vitendo kwa wakati ule. Kitu ambacho nakikumbuka aliniuliza swali moja tu, swali ambalo majibu yake yaliweza kunigharimu.
“Umetembea na mke wangu, amekuhonga nyumba, gari na kila kitu ulichokuwa unakihitaji. Hilo siwezi kukudai wala kuhusu nyumba na gari nimeamua vibaki kuwa kama zawadi yako lakini kwa muda huu nataka uchague kati ya vitu hivi vitatu ili uweze kuyaokoa maisha yako,” aliniambia.
“Vitu gani hivyo?” niliuliza huku nikionekana kuwa na hofu, wale watu waliyokuwa wamenikamata kwa wakati huo walikuwa wamenizunguka halafu mimi pamoja na mume wa Precious tulikuwa katikati.
“Chagua Kati ya kifo yani tukuue, tukuingilie kinyume na maumbile yako au tukuchome sindano ya kuua nguvu zako za kiume?” aliniuliza swali ambalo jibu lake lilikuwa gumu.
Kwa muda ambao nilikuwa nikifikiria tayari Martine alikuwa ameitoa bastola na kuninyooshea, alikuwa amedhamiria kuniua.
“No! No! usiniue,” nilimwambia kwa sauti ya uwoga kisha nikanyamaza kidogo kiasi cha kumeza fundo la mate halafu nikaendelea kuzungumza.
“Ni bora unichome sindano tu, ndiyo nipo tayari,” nilimwambia kisha akaonekana akiwapa ishara wale watu waliyokuwa wamenizunguka. Haikupita sekunde wakanikamata na kunichoma sindano.
Kwa kweli niliyasikia maumivu makali mno, nilijitahidi kuvumilia lakini uvumilivu ulinishinda mwisho nikapitiwa na usingizi wa nusu kifo.
****
Niliamka na kujikuta nipo hospitalini, sikujua niliwezaje kufika eneo lile. Waandishi wa habari walikuwa wamenizunguka kila kona. Nilipopata fahamu kila mmoja alitaka kuzungumza na mimi.
Nilijaribu kuzungumza nao ukweli wa kila kitu, sikutaka kuficha lolote na kitu kikubwa ambacho nilikizungumza ni tuhuma za kutembea na mke wa mtu, hilo niliweza kukiri wala sikutaka kuficha lolote.
Majibu ya daktari aliyokuja kunipa yaliweza kunipa wakati mgumu sana hasa wa kuweza kuamini. Nilikuwa nimepoteza nguvu za kiume, mishipa yangu ya sehemu za siri ilionekana kudhurika kwa kiasi kikubwa sana hasa baada ya sindano ya sumu niliyochomwa, nilikuwa hanithi kwa maana nyingine.
Dah!
Nayaandika haya huku machozi yakinilengalenga machoni. Najua sitakuwa na uwezo tena wa kupata mtoto hata yule ambaye nilibahatika kumpata kwa mke wa mtu hivi sasa ni marehemu yeye pamoja na mwanaye. Uhuni wa kuwatumia wanawake kama chombo cha starehe umeweza kuniacha na funzo kubwa sana katika maisha yangu. Naweza kusema haikupangwa mimi kuchagua kifo, au kuingiliwa kinyume na maumbile na wanaume wenzangu kwa kosa la kutembea na mke wa mtu. Ilipangwa yote haya yanifike ili siku moja niwe shahidi ambaye nitakusimulia kitu kilichowahi kunitokea katika maisha yangu kisha na wewe kijana mwenzangu mwenye tabia kama zangu uweze kujifunza.
Leo mimi nimekuwa hanithi na hakuna kitu kilichoniweka katika hali hii kama sio wanawake, wanawake wamenipa funzo kubwa sana katika maisha yangu.
Nimeamua kuandika kitabu changu kilichobeba uhalisia wa maisha yangu, nimekipa jina la NIFANYE NA MIMI KAKA DICK, naomba vijana wakisome ili wajifunze kitu kupitia mimi. Najua sina muda mrefu wa kuishi tena hapa duniani ile sumu imeweza kuniathiri kwa kiasi kikubwa sana na mpaka hivi ninavyokuandikia nimekutwa na Kansa ya ini. Najua naenda kufa lakini nakufa huku nikiacha elimu tosha kwa vijana. Naomba nisiwe mfano bora wa kuigwa.

NB: Evadia aliweza kuolewa na mwanaume mwingine na baadae walibahatika kupata mtoto mmoja wa kike.

Irine na yeye aliamua kurudiana na Juma Hiza na mapenzi yao yanaendelea mpaka leo.
MWISHO.

Nashukuruni sana kwa kulifuatilia Chombezo hili. Mungu awabariki.

Chombezo hili pia linapatikana WhatsApp na Facebook kwa shilingi Elfu Tatu 3,000/=Tsh tu!
Nicheck kwa namba 0712988278
 
😎🙄🙄 very very baddest end of the story OMG
NIFANYE NA MIMI KAKA DICK-50 JUMA HIZA
+18
Sikutaka kuamini kuwa Martine Deus jina ambalo liliandikwa pale ndiye alikuwa mume wa Precious. Moyo wangu ulizidi kuwa katika maumivu makali mno, kila nilipokuwa nikimuona Martine Deus nilihisi kuchanganyikiwa.
“Tunafanyaje?”nilimuuliza Mick.
“Hapa hakuna cha kufanya zaidi ya kutoroka, inabidi uende mbali sana ukajifiche maana inaonekana mpaka sasa unatafutwa,” aliniambia Mick kisha nikakubaliana na maneno yake. Niliamini kama ningeweza kuondoka na kwenda kujificha mbali nisingeweza kukamatwa.
“Sasa natakiwa kwenda wapi?”
“South Africa.”
“South Africa?”
“Ndiyo huko ndiyo kwenye usalama wako.”
“Naenda kufikia kwa nani?”
“Kuna ndugu yangu mmoja yuko huko nitafanya mazungumzo naye kwa njia ya Email halafu kila kitu kitakuwa sawa.”
“Una uhakika?”
“Niamini,” aliniambia Mick.
Siku iliyofuata Mick alianza kunihangaikia mipango ya kusafiri kwenda South Africa. Ilikuwa ni safari ya ghafla! na nilikuwa nikienda kwa kuzamia. Hakukuwa na njia nyingine niliyoiona kuwa na usalama kwangu zaidi ya kuondoka na kwenda huko mahali ambapo niliamini kulikuwa na usalama wa maisha yangu.
Hatimaye siku ya safari ikawadia, nikaenda Airport kwa kujifichaficha, Mick alikuwa akinisindikiza lakini kitu cha kushangaza tulipofika Airport tulikamatwa na watu waliyojitambulisha kuwa walikuwa ni polisi. Walikuwa na lengo la kunikamata na kunipeleka polisi, sikutaka kubisha wala kupingana na lolote lile kwa wakati huo, safari ya kwenda South Africa iliishia hapo na sasa nikakamatwa na wale watu waliojitambulisha kuwa walikuwa ni polisi, wakaniingiza katika gari lao kisha tukaondoka eneo lile. Mick tulimuacha Airport, sikutaka kujiuliza mara mbilimbili kwanini tulimuacha. Ajabu wale watu waliyojitambulisha kuwa ni polisi nilishangaa wakinipeleka sehemu nisiyoijua, ilikuwa ni sehemu tofauti na kituo cha polisi kama ambavyo waliniambia hapo awali. Tulitoka nje kidogo na jiji la Daresalaam, tuliingia katika moja ya pori ambalo kiukweli mpaka kufikia muda huo sikuwa najua lolote lililokuwa linakwenda kutokea.
“Shukaaaa,” aliniambia jamaa mmoja baada ya gari kusimama pembeni na pori lile.
“Kuna nini jamani?” niliwauliza.
“Wewe unajifanya kidume subiri sasa uoneshwe kuwa hapa mjini kutembea na mke wa mtu ni hatari,” alisema yule jamaa maneno ambayo yalinishtua sana, nilifahamu kuwa wale hawakuwa polisi kama walivyokuwa wamejitambulisha. Nilikuwa nimetekwa na wale watu nisiowafahamu kabisa, niliposhuka na wao wakashuka. Kuna muda nikatamani kukimbia eneo lile lakini nilishindwa. Wale watu walionekana kuwa katika miili iliyojengeka kimazoezi, walionekana kutisha mno kutazama na ni hapa ambapo niliamini ule ndiyo ulikuwa mwisho wa maisha yangu.
Baada ya dakika kadhaa mara likatokea gari aina ya Hummer, lilikuja na kupaki pembeni na pale ambapo nilikuwa nimesimama kisha akashuka mtu aliyevalia mavazi ya suti nyeusi, alionekana kuwa mtu nadhifu sana, nilipomtazama sura yake haikuwa ngeni, niliwahi kumuona sehemu. Alikuwa ni yule mume wa Precious. Alionekana kutawaliwa na hasira sana, uso wake ulihifadhi chuki, alionekana kunichukia sana aliponitazama.
“Ulidhani utanikimbia?” aliniuliza kisha akawa anajilazimisha kucheka kwa sauti kubwa sana huku akiwa ananipigia makofi ishara kama ya kunipongeza jambo fulani.
“Hongera sana Dick, hongera kwa kufanikiwa kummiliki mke wangu tena kwa kuuonyesha ukidume wako ukadiriki mpaka kuzaa naye,” aliniambia maneno ambayo yaliniumiza sana.
“Nadhani ulifikiri kwa mpango aliyokushauri rafiki yako ungeweza kuwa salama, ulipanga kuondoka sasa ona uko sasa hivi?” aliniuliza swali la kunikejeli kisha nikajaribu kuyalinganisha na maneno ya Mick. Kulikuwa na uhusiano, niliamini bila shaka Mick alikuwa ameniuza na kweli alifanikiwa katika hilo.
Yule mume wa Precious hakutaka kuwa muongeaji sana, alipanga kufanya vitendo kwa wakati ule. Kitu ambacho nakikumbuka aliniuliza swali moja tu, swali ambalo majibu yake yaliweza kunigharimu.
“Umetembea na mke wangu, amekuhonga nyumba, gari na kila kitu ulichokuwa unakihitaji. Hilo siwezi kukudai wala kuhusu nyumba na gari nimeamua vibaki kuwa kama zawadi yako lakini kwa muda huu nataka uchague kati ya vitu hivi vitatu ili uweze kuyaokoa maisha yako,” aliniambia.
“Vitu gani hivyo?” niliuliza huku nikionekana kuwa na hofu, wale watu waliyokuwa wamenikamata kwa wakati huo walikuwa wamenizunguka halafu mimi pamoja na mume wa Precious tulikuwa katikati.
“Chagua Kati ya kifo yani tukuue, tukuingilie kinyume na maumbile yako au tukuchome sindano ya kuua nguvu zako za kiume?” aliniuliza swali ambalo jibu lake lilikuwa gumu.
Kwa muda ambao nilikuwa nikifikiria tayari Martine alikuwa ameitoa bastola na kuninyooshea, alikuwa amedhamiria kuniua.
“No! No! usiniue,” nilimwambia kwa sauti ya uwoga kisha nikanyamaza kidogo kiasi cha kumeza fundo la mate halafu nikaendelea kuzungumza.
“Ni bora unichome sindano tu, ndiyo nipo tayari,” nilimwambia kisha akaonekana akiwapa ishara wale watu waliyokuwa wamenizunguka. Haikupita sekunde wakanikamata na kunichoma sindano.
Kwa kweli niliyasikia maumivu makali mno, nilijitahidi kuvumilia lakini uvumilivu ulinishinda mwisho nikapitiwa na usingizi wa nusu kifo.
****
Niliamka na kujikuta nipo hospitalini, sikujua niliwezaje kufika eneo lile. Waandishi wa habari walikuwa wamenizunguka kila kona. Nilipopata fahamu kila mmoja alitaka kuzungumza na mimi.
Nilijaribu kuzungumza nao ukweli wa kila kitu, sikutaka kuficha lolote na kitu kikubwa ambacho nilikizungumza ni tuhuma za kutembea na mke wa mtu, hilo niliweza kukiri wala sikutaka kuficha lolote.
Majibu ya daktari aliyokuja kunipa yaliweza kunipa wakati mgumu sana hasa wa kuweza kuamini. Nilikuwa nimepoteza nguvu za kiume, mishipa yangu ya sehemu za siri ilionekana kudhurika kwa kiasi kikubwa sana hasa baada ya sindano ya sumu niliyochomwa, nilikuwa hanithi kwa maana nyingine.
Dah!
Nayaandika haya huku machozi yakinilengalenga machoni. Najua sitakuwa na uwezo tena wa kupata mtoto hata yule ambaye nilibahatika kumpata kwa mke wa mtu hivi sasa ni marehemu yeye pamoja na mwanaye. Uhuni wa kuwatumia wanawake kama chombo cha starehe umeweza kuniacha na funzo kubwa sana katika maisha yangu. Naweza kusema haikupangwa mimi kuchagua kifo, au kuingiliwa kinyume na maumbile na wanaume wenzangu kwa kosa la kutembea na mke wa mtu. Ilipangwa yote haya yanifike ili siku moja niwe shahidi ambaye nitakusimulia kitu kilichowahi kunitokea katika maisha yangu kisha na wewe kijana mwenzangu mwenye tabia kama zangu uweze kujifunza.
Leo mimi nimekuwa hanithi na hakuna kitu kilichoniweka katika hali hii kama sio wanawake, wanawake wamenipa funzo kubwa sana katika maisha yangu.
Nimeamua kuandika kitabu changu kilichobeba uhalisia wa maisha yangu, nimekipa jina la NIFANYE NA MIMI KAKA DICK, naomba vijana wakisome ili wajifunze kitu kupitia mimi. Najua sina muda mrefu wa kuishi tena hapa duniani ile sumu imeweza kuniathiri kwa kiasi kikubwa sana na mpaka hivi ninavyokuandikia nimekutwa na Kansa ya ini. Najua naenda kufa lakini nakufa huku nikiacha elimu tosha kwa vijana. Naomba nisiwe mfano bora wa kuigwa.
NB: Evadia aliweza kuolewa na mwanaume mwingine na baadae walibahatika kupata mtoto mmoja wa kike.
Irine na yeye aliamua kurudiana na Juma Hiza na mapenzi yao yanaendelea mpaka leo.
MWISHO.
Nashukuruni sana kwa kulifuatilia Chombezo hili. Mungu awabariki.
Chombezo hili pia linapatikana WhatsApp na Facebook kwa shilingi Elfu Tatu 3,000/=Tsh tu! Nicheck kwa namba 0712988278
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom