China yazindua meli kubwa ya kubeba ndege za kivita

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
_63092241_a756ef43-d4e2-4c7c-896d-6835a5a7231f.jpg

China imetangaza kwamba imefanikiwa kuzindua manowari yake ya kwanza ya kujiundia yenye uwezo wa kubeba ndege za kivita.

Meli hiyo ya kivita ina uzani wa tani 50,000.

Hatua hiyo inachukuliwa kama ishara ya karibuni zaidi ya kujiimarisha kwa taifa hilo katika nguvu za jeshi lake la majini.

Vyombo vya habari nchini China vinasema meli hiyo, ambayo inawezesha ndege kuruka na kutua juu yake, ilisafirishwa kutoka eneo ambalo ilikuwa ikiundiwa Dalian na kuwekwa baharini.

Inatarajiwa kuanza kazi rasmi mwaka 2020.

Meli pekee kubwa ya kubeba ndege inayomilikiwa na China ni meli ya Liaonong, ambayo ni meli ya enzi za muungano wa Usovieti iliyofanyiwa ukarabati.

China ilinunua meli hiyo kutoka kwa Ukraine.

Chanzo: BBC Swahili
 
Ngoja niwangoje wale waliokua wanaponda za US kila siku kwamba zimepitwa na wakat sijui nn wakt huohuo wengine wanahangaika kua nazo. Mrusi nae kasema anatengeneza yake.
Pia kwa wale waliokua wanaponda bases za US wkt huohuo mchina nae anahangaika kujenga zake.
 
Wewe nchi yako imejenga kubwa kama hizi ngapi ? Au swli jepesi chi yako inayo meli hata ndogo ya aina hiii....? We bado mudogo saana kakojoe ukalale kama diamond
Hata Kama nchi yetu haina ndio asiseme Kama ni ndogo hata ukienda kununua simu una chaguuua wakati nchi yako haijaunda hata batani chenye sifa kipe HAJA SEMA MBAYA KASEMA NDOGO Mimi Sina nyumba ila kwenye nyumba ambayo sijaipenda sipangi
 
kiongozi samahan hiv kunahistoria yoyote inayoonyesha carrier imewahi kushambuliwa na kuzamishwa?
 
kiongozi samahan hiv kunahistoria yoyote inayoonyesha carrier imewahi kushambuliwa na kuzamishwa?
Yah... Wkt wa WWII.
4beab3f190605c7687248041a6c9ff89.jpg

Baadhi ya Carriers za US ambazo ziliharibiwa wkt wa WWII ni pamojq na USS;
LANGLEY
HORNET
WASP
YORKTOWN

Japan:
AKAGI

UK:
AVENGER, etc.

Ila carriers za zaman na ss hv zina utofaut mkubwa maana za sasa hv zina mitambo ya ulinzi dhidi ya makombora, nk.

Pia zinasindikizwa na Deatroyers ambazo zinailinda dhid ya mashambuliz mbalimbali hvyo ni ngumu kuizamisha kwa kipindi hiki.
ef9a8fa5a0be602565671fcf7dd68549.jpg
b0d8e621d296a5974db2a8868ceb5855.jpg


Mfano US katengeneza SM-6 missile system dhidi ya makombora km DF-21 Carrier killer.

ff39d5b6ca0477cd4ee5989361f6cfb8.jpg
Pia ndan yke inakua imebeba ndege mbalimbali kwa ajili ya kudetect submarines km P-8 Poseidon (sub hunter)au zile za kudetect kombora kwa umbali mrefu mfano, E2D Hawkeye inaweza kudetect kombora likiwa umbali zaid za 345miles(kama 555+km hv),na ndege nyingne za mashambuliz bila kusahau drones.
 
Yah... Wkt wa WWII.
4beab3f190605c7687248041a6c9ff89.jpg

Baadhi ya Carriers za US ambazo ziliharibiwa wkt wa WWII ni pamojq na USS;
LANGLEY
HORNET
WASP
YORKTOWN

Japan:
AKAGI

UK:
AVENGER, etc.

Ila carriers za zaman na ss hv zina utofaut mkubwa maana za sasa hv zina mitambo ya ulinzi dhidi ya makombora, nk.

Pia zinasindikizwa na Deatroyers ambazo zinailinda dhid ya mashambuliz mbalimbali hvyo ni ngumu kuizamisha kwa kipindi hiki.
ef9a8fa5a0be602565671fcf7dd68549.jpg
b0d8e621d296a5974db2a8868ceb5855.jpg


Mfano US katengeneza SM-6 missile system dhidi ya makombora km DF-21 Carrier killer.

ff39d5b6ca0477cd4ee5989361f6cfb8.jpg
Pia ndan yke inakua imebeba ndege mbalimbali kwa ajili ya kudetect submarines km P-8 Poseidon (sub hunter)au zile za kudetect kombora kwa umbali mrefu mfano, E2D Hawkeye inaweza kudetect kombora likiwa umbali zaid za 345miles(kama 555+km hv),na ndege nyingne za mashambuliz bila kusahau drones.
Ze Kokuyo, hivi carrier kubwa kabisa duniani ina uzito gani?
 
Back
Top Bottom