tembeleh2
JF-Expert Member
- Jul 27, 2010
- 765
- 165
Source: mwananchi 29/2/2012
Wana JF hebu angalieni majibu haya ya Mh. Chiligati halafu mchangie. Mimi nafikiri hana ubavu wa kujiuzulu, nyie je?
Alipoulizwa jana kuhusu tishio lake la kutaka kujiuzulu Chiligati alisema: "Mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe." Mahojiano yake na mwandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo:
Swali: Salaam ndugu Chiligati. Kwanza heri ya mwaka mpya.
Jibu: Nzuri, nashukuru na wewe pia.
Swali: Nimesikia kuwa juzi ulitaka kujiuzulu ujumbe wa sekretarieti kutokana na kuvuja siri za kikao chenu cha juzi cha mchakato wa kura za maoni wa Arumeru Mashariki je, msimamo wako ukoje hadi sasa hivi?
Jibu: Bwana wewee! Sikia, hayo ni mambo ya ndani ya vikao. Mambo ya ngoswe mwachie ngoswe mwenyewe!
Swali: Sawa, natambua ni la vikao vya ndani vya chama, lakini huoni kuvuja kwa siri za vikao vyenu kunaonyesha sekretarieti imegawanyika?
Jibu: Nakwambia hivi, hayo ni mambo ya ndani ya vikao. Kwani wewe mbona hutuambii mambo ya nyumbani kwako na mkeo?
Swali: Hujaniuliza, ungeniuliza ningekwambia. Lakini, je, sasa kama siri zitaendelea kuvuja msimamo wako utakuwa ni upi?
Jibu: Haaah...! Wewe bwana shughulika na ya kwako, haya hayakuhusu. Haya ni sawa na mambo ya ndani ya nyumba, ni yetu wenyewe tutayazungumza kwenye vikao vyetu.
Swali: Lakini, tayari mmeweza kubaini ni vipi siri za vikao vyenu zinavuja na labda mmejua ni nani anayezivujisha?
Jibu: Nasema tuachie wenyewe, hatutaki utuingilie. Nasisitiza tena kitu kimoja, hilo halikuhusu endelea na mambo yako.
Wana JF hebu angalieni majibu haya ya Mh. Chiligati halafu mchangie. Mimi nafikiri hana ubavu wa kujiuzulu, nyie je?
Alipoulizwa jana kuhusu tishio lake la kutaka kujiuzulu Chiligati alisema: "Mambo ya Ngoswe mwachie Ngoswe mwenyewe." Mahojiano yake na mwandishi wetu yalikuwa kama ifuatavyo:
Swali: Salaam ndugu Chiligati. Kwanza heri ya mwaka mpya.
Jibu: Nzuri, nashukuru na wewe pia.
Swali: Nimesikia kuwa juzi ulitaka kujiuzulu ujumbe wa sekretarieti kutokana na kuvuja siri za kikao chenu cha juzi cha mchakato wa kura za maoni wa Arumeru Mashariki je, msimamo wako ukoje hadi sasa hivi?
Jibu: Bwana wewee! Sikia, hayo ni mambo ya ndani ya vikao. Mambo ya ngoswe mwachie ngoswe mwenyewe!
Swali: Sawa, natambua ni la vikao vya ndani vya chama, lakini huoni kuvuja kwa siri za vikao vyenu kunaonyesha sekretarieti imegawanyika?
Jibu: Nakwambia hivi, hayo ni mambo ya ndani ya vikao. Kwani wewe mbona hutuambii mambo ya nyumbani kwako na mkeo?
Swali: Hujaniuliza, ungeniuliza ningekwambia. Lakini, je, sasa kama siri zitaendelea kuvuja msimamo wako utakuwa ni upi?
Jibu: Haaah...! Wewe bwana shughulika na ya kwako, haya hayakuhusu. Haya ni sawa na mambo ya ndani ya nyumba, ni yetu wenyewe tutayazungumza kwenye vikao vyetu.
Swali: Lakini, tayari mmeweza kubaini ni vipi siri za vikao vyenu zinavuja na labda mmejua ni nani anayezivujisha?
Jibu: Nasema tuachie wenyewe, hatutaki utuingilie. Nasisitiza tena kitu kimoja, hilo halikuhusu endelea na mambo yako.