Chicago yamkataa Donald Trump

pierre buyoya

JF-Expert Member
Dec 6, 2015
476
163
Usiku wa Jana ijumaa ya Tarehe 11 Machi ulikuwa mgumu kwa Mgombea urais wa Marekani kupitia Chama cha Republican, Mfanyabiashara Donald Trump mara baada ya fujo kuibuka mji wa chicago ambapo alitakiwa akafanye kampeni.

Katika hali ya kushangaza maelfu ya wafuasi wa Donald Trump wengi wao wakiwa wazungu walikutana na kundi kubwa la wapinzani wa Mgombea huyo (mchanganyiko wa wazungu na wamarekani weusi) wakiwa tayari kumfanyia fujo akiwasili kuhutubia katika ukumbi wa chuo kikuu cha illinois.

Kutokana na hali hiyo ziliibuka vurugu kubwa kati ya Wafuasi na wapinzani wa Trump pamoja na polisi kitu kilichopelekea kuahirishwa kwa mkutano huo wa kampeni na mgombea huyo kutoweka kusikojulikana.

Kuna kampeni ya chini kwa chini za kumfanyia vurugu mgombea huyo katika majimbo yaliyobaki.

de1d98c84c8268bdb7d0ef39556b7108.jpg

cf96f475ebcbe16d15f6f8b078b7ebbb.jpg
 
W
Usiku wa Jana ijumaa ya Tarehe 11 Machi ulikuwa mgumu kwa Mgombea urais wa Marekani kupitia Chama cha Republican, Mfanyabiashara Donald Trump mara baada ya fujo kuibuka mji wa chicago ambapo alitakiwa akafanye kampeni . . .

Katika hali ya kushangaza maelfu ya wafuasi wa Donald Trump wengi wao wakiwa wazungu walikutana na kundi kubwa la wapinzani wa Mgombea huyo (mchanganyiko wa wazungu na wamarekani weusi) wakiwa tayari kumfanyia fujo akiwasili kuhutubia katika ukumbi wa chuo kikuu cha illinois . . .

Kutokana na hali hiyo ziliibuka vurugu kubwa kati ya Wafuasi na wapinzani wa Trump pamoja na polisi kitu kilichopelekea kuahirishwa kwa mkutano huo wa kampeni na mgombea huyo kutoweka kusikojulikana . . .

Kuna kampeni ya chini kwa chini za kumfanyia vurugu mgombea huyo katika majimbo yaliyobaki . . .

de1d98c84c8268bdb7d0ef39556b7108.jpg

cf96f475ebcbe16d15f6f8b078b7ebbb.jpg
Watanzania bwana kwa upotoshaji hawajambo,kwa mfano huyu jamaa anataka kutuaminisha kuwa Chicago wamemkataa Trump. Sasa kama wamemkataa hao unaotaja kuwa wafuasi wake walikuwa nao wamemkataa au? Na kama wamemkataa fujo zilitokea za nini?
Kwa nini usiseme kuwa mkutano wa Trump washindwa kufanyika Chicago,baada ya kutokea vurugu kati ya wafuasi wake na wale wanaompinga. Kuishi Tz noma sana
 
W
Watanzania bwana kwa upotoshaji hawajambo,kwa mfano huyu jamaa anataka kutuaminisha kuwa Chicago wamemkataa Trump. Sasa kama wamemkataa hao unaotaja kuwa wafuasi wake walikuwa nao wamemkataa au? Na kama wamemkataa fujo zilitokea za nini?
Kwa nini usiseme kuwa mkutano wa Trump washindwa kufanyika Chicago,baada ya kutokea vurugu kati ya wafuasi wake na wale wanaompinga. Kuishi Tz noma sana
Usichoelewa nn sasa mkuu..
 
Tunajifunza nini kwa hii post yako?
bado marekani haijakomaa kidemokrasia.. inchi iliyokomaa kidemokrasia inafanya maamuzi kupitia sanduku la kura. Sasa hawa wanaoleta vurugu kumpinga Trump inaonyesha jinsi gani Marekani haijakomaa kidemokeasia.

Hawa wachache wanampinga ila wengi wanamkubali ndo maana anaongoza majimbo mengi, naona wamesahau kanuni muhimu ya demokrasia inayosema wengi wape. Wengine wakaiita demokrasia ni udikteta wa watu wengi.

Jambo la pili tunalojifunza ni mpasuko wa chama cha Republican.Hii inavipa funzo vyama vya siasa nchini kuhakikisha vinakuwa na mshikamano wakati wa kampeni za ndani (kura ya maoni) wakati wa kuchagua mgombea urais kupitia vyama vyao. Mipasuko huku Afrika inapelekea kuongezeka kwa vyama vya siasa ambavyo si vishindani bali vinaishia kuwa vioinzani kwa vyama pinzani na sio kwa chama tawala pia inapelekea kuipa serikali mzigo mkubwa wa kuvipa ruzuku vyama hivyo . Sio kama kwa wenzetu Wazungu wao wanahubiri mfumo wa siasa ya vyama vingi ikiwa wao wanavyama vichache tuu (U.S wana viwili. ie Republican & Democratic) UK ie Labour, Conservative & Liberal Democrats) German ie CDU, SPD & CSU na vingine vidogo ambavyo vinatengeneza coalition na vyama vikubwa)
 
Back
Top Bottom