Chenji yangu konda

Chenji yangu konda

Wengi wenu mmeonekana kutomiliki magari tofauti na siku nyingine ambazo huonekana kila mtu anamiliki gari humu JF.
 
Tangu nimemiliki bodaboda sikumbuki kupanda daladala...hata nauli sizijui...kwny kumdai konda chenji hapo sina points
 
kwani mtu mwenye gari ndo hapandi daladala jamani? mh watz bwana basi mtu akipanda public bus anaonekana masikiiini kumbe kila mtu ana malengo yake jamani.ukweli mimi hupanda siku mojamoja daladala na huku arusha jamani hicho wanaita cha arusha, viroba na madawa ya kulevya vimewamaliza makonda ni wana matusiii hayooo lugha chafuu wenyewe wachafuuu sijui mikoa mingine.yaani nikipanda daladala nalipa mapema ili kama akinipa chenji nusu nipambane nae kabla ya mwisho wa kituo maana wengi hufanya makusudi ili uone aibu uwaachie.mie siachi bora wangekua na staha sio wastaarabu hata kidogo ndo maana weng wao roho zinawauma.
nakumbuka kuna siku nilipanda daladala ya kwenda mbauda mrombo mzee mmoja akatoa 500 akamwambia shusha kona nairob wakat huo ametoa nauli tangu mataa ya esso kwa wanaojua arusha.hajampa mia yake tukafika kona akaanza kusema abiria mwenye mia.akakosa akamwambia mzee si uniachie? yule mzee akamwambia toa sarafu zote mfukoni.nione kama huna mia.hahaha konda alivotoa.mia zipo kibaao akamwambia mbona unaninyima chenji yangu wakati unayo? yule mzee akaipokea kisha akaitupa kulee akamwambia kuliko nokuachie.mia yangu heri nitupe.
 
Mi nagawana nao pasu, nikipanda asiniulize nauli nakausha.

Na hii ilitokea baada ya kusahau chenji ya Shs 10,000 kwenye dala dala ya Mwananyamala - Kivukoni mwaka 2007 mpaka leo inaniuma na sina uhakika kama nilisha irudisha. Lakini najua itarudi tu.
Njia rahisi: Ukimuona konda ameshika noti nyingi za 10,000/= unapofika kituoni kwako mwambie akurudishie chenchi yako unashuka hapo tena uwe mkali kweli, ikiwezekana tafuta shahidi wa uwongo akusaidie. Kama anabisha mwambie mwende polisi.
 
Njia rahisi: Ukimuona konda ameshika noti nyingi za 10,000/= unapofika kituoni kwako mwambie akurudishie chenchi yako unashuka hapo tena uwe mkali kweli, ikiwezekana tafuta shahidi wa uwongo akusaidie. Kama anabisha mwambie mwende polisi.

Usijidanganye, jamaa wana kumbu kumbu balaa! Utaaibika.
 
Siwezi kumuachia konda chenji hata kama ni sh 10, wao ukipungukiwa hata sh 50 ni shidaa, hawana ubinadamu hata kidogo makodakta
 
Yaani mkuu siachi hata sent moja kwa konda yaani nitamkwida hadi ataitoa, niliibiwa mwenge pesa yote bahati nzuri jamaa alimuona akamnyang'anya simu hivyo nilifanikiwa kupata simu tu, daladala zima walijua hata konda mwenyewe na driver walichofanya hawakunishusha hapo kufika Buguruni shell abiria walipungua jamaa kuona bado sijashuka walichofanya ni kututeremsha wote na kusema hawaendelei na safari wote wakarudishiwa pesa zao mimi nikabaki nang'aa macho ilibidi nikanyage hadi ninapokwenda, yaani ukinikuta nagombea hiyo hamsini huwezi amini. utasikia abiria ati wanamtetea konda "yaani jinsi ulivyo hata huelekei" na mimi nawajibu tu "sielekei nini? lete hamsini yangu"
kama hana daladala haliendi.
 
Back
Top Bottom