Kama mtu ni msafi kwanini uogope kuhojiwa?hapo ndio anatia shaka uadilifu wake,angekuwa msafi wala usingekimbilia kuweka zuio,huyu ni sawa na mwenye makosa anavyoogopa hata kupita kituo cha polisi ,ni sawa na mhalifu anapomuona askari hukimbia au huanza kujitetea hata kabla polisi hajafungua kinywa chake.Ukiwa mwizi hata ukisikia sauti za mwizi mwizi nawe huanza kukimbia au kusema au mimi sio mwizi bila hata ya kuulizwa.Ni aibu kwa watu wa Bariadi kuwa na mbunge kama Chenge halafu anawadanganya kwa kuwapa fedha za wizi nao kwa ujinga wao wanapokea na kumpigia makofi,anayeshiriki kupokea vitu vya wizi naye ni mwizi au anayepokea rushwa naye ni mla rushwa,huwezi mbunge na msomikama Chenge kujifanya eti kutoa hivyo vijisenti eti ndio kuwaletea maendeleo watu wake wa Bariadi,hawa wezi wakiiba hukimbilia majimboni mwao na kutoa hizo hela za wizi eti huko ndio kuwaletea maendeleo watu wao,akina Prof Tibaijuka nao walifanya vivyo hivyo,walipotimuliwa wakakimbilia majimboni mwao eti kuwaletea maendeleo wananchi wao.Ndugu zangu maendeleo hayaletwi na mbunge au mtu moja mmoja maendeleo huletwa na wananchi wenyewe,tuache ujinga,hayo maendeleo ndio wanayaona leo karibu na uchaguzi,watu wa Bariadi mungemuuliza Chenge hizo hela kazipata wapi na kwa biashara gani anayoifanya?mlivyofanya ni sawa na mzazi anayepokea fedha au msaada kutoka kwa mtoto wake wakati akijua mtoto wake hana kazi yoyote ya kuleta mabilioni hapo nyumbani.