Chenge azomewa (Mwakibuga, Bariadi)

Frank Kubwera

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2014
Posts
244
Reaction score
112
Mbunge wa jimbo la Bariadi mashariki mze wavijisenti. Amekubwa na aibu ya kuzomewa na wanakijiji wa kijiji cha Mwakibuga jimboni kwake.

Dhahama hii imemkuta mbunge huyu (aliyetumbua dili ya rada 2003), alikuwa akihutubia wananchi wa kijiji hicho. Sakata lilianza pale Chenge alipowaambia wananchi waacheakushiriki harakati za Chadema. Gafla watu wakaanza kugunaguna. Naye bila kujua akarudia maelekezo yake hayo. Ndipo kundi la wanachi wakamzomea kwa sauti kubwa.
Baada ya kuzomewa chenge akawaamuru police kuwakamata wazomeaji. Hapo ndipo khali ikawaka ghafla na lolote likichelea kutokea hadi mzee chenge alipotolewa chini ya escort ya FFU.

Kwa sasa Watu wa Bariadi wameapa kutodanganyika na liCCM tena.
 
Safi sana hongereni wana bariadi, kakutana na nguvu ya umma.

Napongeza zomea zomea iwe ndio style ya kuyanyamazisha mafisadi na maccm.

Ni kwanini huwa yakiwa jukwaani lazma yaongele CHADEMA?

Hongereni bariadi, ujumbe tosha ameupata
 
Kumbe watu hawaogopi fedha siku hizi...!!!! ? Lo natamani iwe hivi dhidi ya watani zangu nchi nzima.
 
vipi round hii hakuwa kachinja Ngombe makumi au alichinja chache. Maana Chenge hua hafanyi mkuno bila kuchinja kwanza watu wanapakia Nyama wali nachuzi afu ndiyo wanaleta masipika anaanza kujisifia weeeeeeeeee.

Mafisadi bana.. nishida.
 

Kweli hakuna marefu yasiyo na ncha kwa mbaali namuona Chenge yuko Mahakamani. Shaidi mkapa. Haha.
 
wasukuma walishajitambua siku nyingi ndiyo maana wabunge wengi wa upinzani wanatoka huko, ndugu zangu hawa wamenyanyasika sana na mdudu ccm..huwa wanalazimishwa kulima pamba halafu serikali kwa kushirikiana na mafisadi ya ccm hupanga bei ya kununua...
 
inatakiwa iwe hivyo hivyo mpaka waachane na unyonyaji
 
Ni kweli nasikiq kaondolewa kwa msaada wa FFU,

Mwakibuga ni kijiji kilichopo jimboni kwake Bariadi mashariki.

Shuhuda anasema, zomea zomea ilianza chini chini na yeye akaanza kutumia lugha ya kuudhi na kuwadharau CHADEMA.

Ndipo zomea zomea ilipamba moto mbaya zaid waiozomea walikuwa wamevalia nguo za maccm za kijani kama kawaida yao.

Je!ccm imeanza kuchokwa bariadi mark ama ni Chenge mwenyewe?
 
wangempiga tuu mpuuzi mkubwa huyu wao wanawaza chadema tuu n nimeamini mti wenye matunda ndo unarushiwa mawe chadema chama makini lazma ccm wawaseke sanaa
 
Ha ha hapo ndipo ninapojivunia kuwa mnyantuzu! Majembe yale, na bado. Aende Halawa,Gibeshi, Nkindwabiye,matongo, Sapiwi,igegu, kule wanaugwadu nae tapeli yule lazma wamdunde labda aende na defender mia.....anaetaka kugombea jimbo hilo ebu tuwasiliane kwa kasanzu@live.com
 
Wanyantuzu wakighaili mpaka litakutoka povu, ni kweli Simiyu ccm imekwisha, amini au usiamini, Simiyu Yetu analifahamu hili na anajitoa ufahamu kwa makusudi
 

hivi mwakibuga ni kijiji siku hizi,maana zamani nikiona kama mkusanyiko wa nyumba hazifiki 20
 
Wakati wanalipana buk 7 sisi tunaiua ccm taaratibu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…